Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mutasingwa Asema Miradi Ya Kimkakati Kuibeba Ccm Bukoba Mjini

 Na Angela Sebastian; Bukoba Mgombea ubunge wa jimbo la Bukoba mjini Mhandisi Johnston Mutasingwa ametaja sababu za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kuomba ridhaa ya kuongoza jimbo hilo ambapo ni kutokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati aliyotekeleza Rais Dk.Samia Suluhu Hassan. Mutasingwa amesema katika jimbo la Bukoba mjini Dk.Samia ametekeleza miradi mbalimbali katika idara ya elimu,Afya,barabara,maji,standi kuu ya mabasi sambamba na soko kuu la Bukoba ambalo lilikwama kwa muda mrefu kutokana na sababu za kisiasa na kiutendaji.  Ameeleza hayo leo katika mkutano wa adhara wakati akiomba kura kwa wananchi wa kata ya Kibeta ambapo uliudhuliwa na mamia ya wananchi,wakeleketwa na wanachama wa CCM wa jimbo jilo. "Kwa heshima na taadhima nawaomba Oktoba 29 mwaka huu tumpe kura nyingi za shukrani Rais wetu ili aendelee kutekeleza miradi hii ya kimkakati aliyoianzisha na kutuletea mingine mipya ambayo itapandisha mara dufu maendeleo yetu" amesema Mutasingwa ...

Tanzania Yang’ara Uwekezaji Katika Elimu Kwa Rasilimali za Ndani

📌 Dkt. Biteko asema tafiti zaonesha elimu bora huchangia asilimia 20-30 ya ukuaji wa uchumi 📌 Walimu milioni 17 wa shule za msingi na sekondari wahitajika Afrika ifikapo 2030 📌 Bajeti ya elimu yaongezeka kwa trilioni 1.44 tangu mwaka 2020/21 Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopiga hatua katika  matumizi ya rasilimali za ndani na kuwekeza katika sekta ya elimu kwa maendeleo endelevu. Amesema hayo Septemba 24, 2025 jijini Dar es salaam wakati akifungua Kongamano la Tano la Kimataifa la Elimu Bora lililoongozwa na kauli mbiu inayosema “Kuimarisha mifumo na uwekezaji: Kusonga mbele katika Uhamasishaji wa Rasilimali za Ndani kwa ajili ya Elimu Jumuishi, Bora na Endelevu Barani Afrika”. Dkt. Biteko ametaja hatua zilizochukuliwa na Serikali kuwa ni pamoja na kutunga na kuboresha Sera, Sheria na miongozo mbalimbali ya elimu, kuongeza kiwango cha bajeti ya elimu kutok...

Dkt Samia Aweka Shada la Maua Katika Kaburi la Mzee Benjamin Mkapa

 Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua katika Kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu Hayati Benjamin William Mkapa, Lupaso, Masasi mkoani Mtwara tarehe 24 Septemba, 2025.

Dkt.Nchimbi Alivyohitimisha Kampeni Zake Mkoa wa Njombe

PICHA za matukio mbalimbali za mkutano wa hadhara wa kampeni wa Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dk Emmanuel Nchimbi  uliofanyika mjini Makambako, mkoani Njombe alipokuwa akihitimisha mikutano yake kampeni mkoani humo leo Septemba 24, 2025. Mara baada ya kuwahutubia Wanachi katika mkutano huo,Dkt.Nchimbi pia alitumia nafasi hiyo kumnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Makambako Ndugu Daniel Godfrey Chongolo pamoja na Madiwani. Dk Nchimbi naendelea kusaka kura za Mgombea urais wa chama hicho, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wabunge na madiwani pamoja na kunadi Ilani ya CCM ya mwaka 2025 - 2030

Kamishna Kuji Atoa Wito Tanapa Kuwa na Saccos Moja

Na. Edmund Salaho - Tanga Kamishna wa Uhifadhi TANAPA  CPA Musa Nassoro Kuji ambaye pia ni mlezi wa HIFADHI SACCOS LTD ametoa wito kwa watumishi wote wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania kujiunga pamoja na kuanzisha SACCOS moja kwa watumishi wote wa TANAPA itakayoitwa TANAPA SACCOS LTD. Kamishna Kuji ameyasema hayo leo Septemba 24, 2025 katika Mkutano Mkuu wa mwaka 2025 wa HIFADHI SACCOS unaofanyika Jijini Tanga. "Ninafahamu kuwa kulikuwa na timu maalum ya uhamasishaji ambayo ilipita katika vituo vyote vya kazi kuhamasisha watumishi kufahamu faida za kuwa na SACCOS moja na kuwaomba watumishi wawe tayari kuunga mkono suala hilo muhimu. Mimi pia katika ziara zangu katika vituo vyote katika Shirika nimewasihi watumishi kukubali wazo la kuwa na SACCOS moja. Katika maeneo yote niliyopita, watumishi wamenihakikishia kuwa wazo hilo ni wazo jema na wapo tayari kuliunga mkono wakati ukifika". Akitaja faida chache zitakazopatikana kwa kuwa na SACCOS moja, Kamishna Kuji alibainisha k...