Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAHITIMU VYUO VIKUU SASA WAKIMBILIA VETA


 Dhana kwamba elimu ya ufundi stadi ni kwa watu waliokosa fursa za elimu ya juu inaendelea kupotea, huku wahitimu wenye vyeti, stashahada, shahada na hata shahada za uzamili wakijitokeza kujiunga na mafunzo ya ufundi stadi ili kuongeza ujuzi na kukidhi mahitaji ya soko la ajira.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), CPA Anthony Kasore, amesema katika kipindi cha mwaka 2022/2023 hadi 2025/2026, jumla ya waombaji 794 wa mafunzo ya ufundi stadi walikuwa tayari na elimu za juu katika taaluma mbalimbali.

Amesema kati yao, 522 walikuwa na vyeti vya taaluma nyingine, 120 walikuwa na stashahada, 151 walikuwa na shahada na mmoja alikuwa na shahada ya uzamili.

Kasore ameyasema hayo leo, Septemba 4, 2026, jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu nafasi ya VETA katika kujenga Taifa lenye wananchi wenye ujuzi.

Amesema ongezeko hilo linaonesha mabadiliko makubwa katika mtazamo wa jamii kuhusu elimu ya ufundi stadi, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikihusishwa na watu waliokosa nafasi ya kuendelea na elimu nyingine.

“Uelewa wa umma kuhusu thamani ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi unazidi kukua, huku dhana ya ufundi stadi kuwa ni kwa ajili ya kundi fulani lililokosa fursa zingine za kielimu ukizidi kupungua,” amesema Kasore.

CPA Kasore amesema sambamba na kuongezeka kwa mahitaji ya ujuzi, VETA imeendelea kuongeza nafasi za mafunzo nchini, ambapo udahili katika vyuo vinavyomilikiwa na mamlaka hiyo umeongezeka kutoka wanachuo 69,347 mwaka 2022/2023 hadi 116,468 mwaka 2025/2026.

Amesema ongezeko hilo limechangiwa kwa kiasi kikubwa na kuanza kwa shughuli za vyuo vipya 33 vya VETA katika ngazi za mikoa na wilaya.

"Serikali inaendelea kukamilisha ujenzi wa vyuo vipya 65 vya VETA, ambavyo vinajumuisha vyuo 64 vya wilaya na chuo kimoja cha Mkoa wa Songwe". Amesema

Vyuo hivyo vinatarajiwa kuanza kutoa mafunzo Januari 2027 na vinatarajiwa kuongeza uwezo wa VETA kudahili wanafunzi wapya 130,892 katika mwaka huo.

Katika hatua nyingine, CPA Kasore amesema VETA imeendelea kurasimisha ujuzi wa mafundi waliojifunza kupitia uzoefu, uanagenzi na mazingira ya kazi bila kupitia mfumo rasmi wa mafunzo.

Kupitia Mpango wa Utambuzi na Urasimishaji Ujuzi uliopatikana Nje ya Mfumo Rasmi wa Mafunzo (RPL), jumla ya mafundi 18,008 wamerasimishiwa ujuzi wao kupitia Programu ya Mama Samia ya Utambuzi na Urasimishaji Ujuzi.

Amesema katika kipindi cha 2022/2023 hadi 2025/2026, pia jumla ya mafundi 426 wenye elimu za juu waliomba kurasimishiwa ujuzi wao.

Kati yao, 82 walikuwa na vyeti vya taaluma nyingine, 167 stashahada, 170 shahada na saba shahada za uzamili.

Kwa mujibu wa Kasore, takwimu hizo zinaonesha wazi kuwa ujuzi wa ufundi stadi sasa unatambuliwa kama nyenzo muhimu ya kuongeza ushindani katika ajira na uzalishaji.

Kasore ametoa wito kwa jamii kubadili mtazamo kuhusu elimu ya ufundi stadi na kuacha kuichukulia kama chaguo la mwisho kwa mwanafunzi anayeshindwa kuendelea na elimu nyingine.

Amesema Tanzania inayolenga kujenga uchumi wa viwanda, kukuza sekta ya madini, kilimo cha kisasa, TEHAMA, ujenzi na uchumi wa buluu inahitaji mamilioni ya Watanzania wenye ujuzi wa vitendo.

“Tusimwambie mtoto wetu, ‘ukifeli shule utasoma ufundi.’ Tumwambie, ‘ukitaka kuwa na ujuzi wa kujenga maisha na kujenga Taifa, soma ufundi stadi,’” amesema.

Amesema VETA imejipanga kuongeza ubora wa mafunzo, kupanua fursa za mafunzo, kuimarisha miundombinu na vifaa, kutumia TEHAMA, kuendeleza utafiti na ubunifu pamoja na kuimarisha ushirikiano na waajiri na viwanda.

CPA Kasore amesema katika kipindi kijacho, VETA inalenga kuhakikisha ongezeko la udahili linaenda sambamba na ubora wa mafunzo, mahitaji ya waajiri pamoja na uwezo wa wahitimu kupata ajira au kujiajiri.

"Mafunzo yataelekezwa zaidi katika sekta zenye mahitaji makubwa ya nguvu kazi, ikiwemo kilimo na uchakataji wa mazao, ujenzi, madini, nishati, TEHAMA, usafiri na usafirishaji, uzalishaji viwandani na uchumi wa buluu". Amesema.

Aidha, kupitia Programu ya Elimu na Ujuzi kwa Ajira zenye Tija (ESPJ II), VETA inalenga kuimarisha miundombinu, vifaa vya kisasa, matumizi ya teknolojia za kidijitali na ujuzi wa wakufunzi.

CPA Kasore amesema lengo kuu ni kuhakikisha mfumo wa ufundi stadi unaunganisha udahili, mafunzo, umahiri, ajira au kujiajiri, tija na uzalishaji, ili wahitimu wawe sehemu muhimu ya ujenzi wa uchumi wa Taifa.

Amesisitiza kuwa safari ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 haiwezi kufanikiwa kwa kutegemea rasilimali pekee, bali inahitaji pia rasilimali watu yenye ujuzi, ubunifu, nidhamu na uwezo wa kutumia teknolojia.

“Tanzania ya viwanda inahitaji mafundi; Tanzania ya madini inahitaji mafundi; Tanzania ya TEHAMA inahitaji mafundi; Tanzania ya kilimo cha kisasa inahitaji mafundi; na Tanzania ya Dira 2050 inahitaji mamilioni ya Watanzania wenye ujuzi,” amesema Kasore.




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...