Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mavunde Azindua Rasmi Shughuli za Ujenzi wa Mgodi Mkubwa wa Madini ya Kinywe Mahenge

▪️Rais Samia apongezwa kwa mazingira wezeshi ya biashara ▪️Aitaka Kampuni ya Faru Kutoa Kipaumbele cha Ajira kwa wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi, ▪️Ni Uwekezaji wa zaidi ya Tsh Trilioni 1.3. ▪️Serikali kuvuna zaidi ya shilingi trilioni 7 kama mapato. ▪️Ni Mradi Mkubwa zaidi kuwahi kutokea Mkoa wa Morogoro. 📍 Mahenge, Morogoro.  Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Peter Mavunde (MB), amezindua rasmi shughuli za ujenzi wa mgodi wa madini  ya Kinywe(Graphite), unaotekelezwa na kampuni ya Faru Graphite Corporation kwa ubia kati ya Serikali ya Tanzania (hisa 16%) na Black Rock Mining Limited (hisa 84%) ikiwa ni hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya sekta ya madini nchini. Akizungumza katika hafla iliyofanyika leo tarehe 9 Oktoba 2025 katika eneo la Mahenge, Wilaya ya Ulanga, Mkoa wa Morogoro, Mhe. Mavunde amesema uzinduzi huo ni ishara ya kasi mpya ya uendelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati katika Sekta ya Madini, kutokana na maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Sa...

Dkt.Nchimbi Aendelea Kusaka Kura za Ushindi wa Kishindo za Ccm Rufiji, Pwani

  PICHA  za matukio mbalimbali za Mgombea mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwahutubia Wananchi kwenye mkutano wake wa hadhara wa kampeni katika Uwanja wa Soko la Tasaf, Kata ya Nyamwage, Wilaya ya Rufiji mkoa wa Pwani, leo Alhamisi Oktoba 9,2025. Katika Mkutano huo Dkt.Nchimbi alimuombea kura za ushindi wa kishindo  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu pamoja na Wabunge na Madiwani. Katika hatua nyingine Dkt.Nchimbi pia alipata nafasi ya kumnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Rufiji,Ndugu Mohammed Mchengerwa na Madiwani. Dkt.Nchimbi anafikia mkoa wa 19 (Tanzania Bara)  akizunguka nchi zima kunadi sera na Ilani ya CCM ya 2025-2030,huku akiwahimiza Wananchi kuichagua serika ya  CCM kwa miaka mingine mitano,itakayolenga kuwaletea maendeleo Wananchi.

Edwin Soko atoa tathimini ya utendaji wa Vyombo vya habari kwenye kampeni

  Mwandishi wetu Mwanza Mwandishi wa habari Mwandamizi na Mtetezi wa haki za binadamu Edwin Soko amesema kuwa, mazingira ya utendaji kazi wa Vyombo vya habari kwenye mikutano ya kampeni za wagombea yamekuwa rafiki  kuelekea uchaguzi  mkuu wa Oktoba 29,  2025. Soko amesema hayo kwenye mahojiano na Vyombo vya habari Leo Jijini Mwanza juu ya tathimini  ya  utendaji kazi wa Vyombo vya habari kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 " kuanzia Agosti 28 , 2025 hadi kufikia sasa hatujapata taarifa zozote za madhila Kwa Vyombo vya habari au waandishi wa habari yeyote yule hali inayoashiria kuimarika Kwa  usalama wa Waandishi wa Habari na haki ya waandishi wa habari kufanya kazi bila kubuguziwa  wakati huu wa kampeni za wagombea kwenye ngazi za Urais , Ubunge na  Udiwani" Alisema Soko. Soko pia aliongeza kuwa, amekuwa akifuatilia taarifa za utendaji kazi wa Vyombo vya habari tangia kampeni zianze Agosti 28  na kushuhudia uwajibikaji mkubwa wa waand...

Wasira:Atahadharisa Watu Wachache Kutumia Mitandao kuleta chokochoko

*Amesema ni kikundi cha watu wachache* *wasioridhika* *Ataka wananchi wasiwasikilize, waendeleze umoja, mshikamano* *Amhakikishia Dk. Samia mamilioni ya Watanzania wanamuunga mkono* Na Mwandishi Wetu,  BUNDA MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, ametoa tahadhari kwa wananchi dhidi ya kikundi cha watu wachache wanaoleta chokochoko katika mitandao ya kijamii. Amesema kikundi hicho ni miongoni mwa watu wachache wasioridhika, hata hivyo kamwe hawatotimiza dhamira yao ovu. Akizungumza katika mkutano wa kampeni za urais uliohutubiwa na Mgombea Urais kupitia CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan, mjini Bunda, alisema amani na utulivu utaendelea kutawala nchini. "Zipo chokochoko nyingi ambazo hazipo kwa watu, zipo kwa wacheche wanaotumia mitandao ya kijamii. Naomba msome ile mitandao kwa makini sana. Kuna watu hawaridhiki. "Kinamama wanaopika maharage wanafahamu yapo maharage hata ukiyapika vipi yatatokea machache yakielea. Hayo hayaivi na ndiyo watu wanaosumbua...

Dkt.Nchimbi Awasalimia Wananchi Wa Kibiti Akielekea Mkuranga

Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwasalimia na kuzungumza na wananchi wa jimbo la Kibiti wakati akielekea kwenye mkutano wake wa hadhara wa kampeni wilaya ya Mkuranga jioni ya leo Oktoba 9,2025 mkoani Pwani.

Dkt Samia Aomba Kura Kwa Wananchi wa Lamadi Mkoani Simiyu

 Mgombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM na Mwenyekiti wa Chama cha Mapindzii CCM Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Wananchi, Wanachana na Wapenzi wa CCM wa Lamadi (Busega) katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama hicho Mkoani Simiyu tarehe 09 Octoba 2025.