Na Angela Sebastian, Ngara Baadhi ya wakazi wa Kata ya Ngara mjini, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, wameeleza kuwa ujenzi wa barabara ya Magereza–Kabalenzi kwa kiwango cha lami utarahisisha usafiri na usafirishaji wa mazao kwenda sokoni, hatua wanayoamini itachochea shughuli za kiuchumi na kuongeza kipato cha wananchi pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa. Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 0.55 imejengwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Ngara kwa gharama ya zaidi ya Shilingi milioni 316. Mbali na kuboresha mandhari ya mji, wananchi wameitaja kuwa ni fursa muhimu ya kurahisisha usafirishaji wa bidhaa, ikiwemo mazao yanayopelekwa katika nchi jirani ya Burundi hivyo kuongeza mzunguko wa biashara katika eneo hilo. Meneja wa TARURA Wilaya ya Ngara, Mhandisi Mokoro Magori, akisoma taarifa ya mradi huo kwa kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa 2026a amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Oktoba 2024 na unalenga kuboresha miundombinu ya barabara pamoj...
Marato tv - Sauti ya Jamii