Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

KURA ZA WATANZANIA KUAMUA KAZI 294 ZILIZOFUZU SAMIA KALAMU AWARDS 2026

 Na. Mohammed Ulongo Katika kutambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari nchini, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), zimetangaza kuwa jumla ya kazi 294 zimefuzu hatua ya mwisho ya Tuzo za Uandishi wa Habari na Makala za Maendeleo za Samia Kalamu Awards 2026. Akizungumza leo Septemba 3, 2026 jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Samia Kalamu Awards 2026, Mhandisi Peter P. Mwasalyanda, amesema mkutano huo na waandishi wa habari ulikuwa na lengo la kuwaeleza wananchi namna ya kushiriki katika zoezi la kupiga kura kwa ajili ya kuwapata washindi wa tuzo hizo. Mhandisi Mwasalyanda amesema katika hatua za awali, waandaaji walipokea jumla ya kazi 3,003 zilizowasilishwa na waombaji 985 kutoka maeneo mbalimbali nchini, ambapo baada ya kupitia mchakato wa tathmini, majaji walifanikiwa kuteua kazi 294 ambazo sasa zimefika hatua ya kupigiwa kura na wananchi. Amesema zoezi l...

MWIGULU: TUWAWEZESHE WATANZANIA KUSHIKA UCHUMI WAO

 Mkuu wa Mwigulu Nchemba, Dkt. Mwigulu Nchemba, ametoa wito wa kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira, kukuza sekta binafsi, kuongeza mapato na kupunguza umaskini nchini. Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo, Alhamisi Septemba 3, 2026, wakati akifungua Kongamano la Tano la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati na Uwekezaji, lililofanyika Dodoma. Amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira ya kisera, kisheria na kiutendaji yatakayowawezesha Watanzania kushiriki moja kwa moja katika uchumi. “Tuwawezeshe Watanzania kushika uchumi wao. Hii ndiyo njia ya kuongeza ajira, kuongeza vyanzo vya mapato na kujenga sekta binafsi yenye nguvu,” amesema. Amesema lengo la kuwawezesha Watanzania si kuwazuia wawekezaji wa nje, bali kuongeza uwezo wa kampuni na wananchi wa ndani ili nao wanufaike na fursa zinazotokana na rasilimali na miradi mbalimbali ya maendeleo. Katika hatua nyingine...

JUWATA, UTPC KUSHIRIKIANA KUTETEA HAKI, MASLAHI YA WAANDISHI WA HABARI

 JUKWAA Huru la Wahariri Tanzania (JUWATA) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) wamekubaliana kuimarisha ushirikiano katika kulinda uhuru wa vyombo vya habari, kutetea haki na maslahi ya waandishi wa habari pamoja na kuhakikisha jamii inapata habari sahihi na kwa wakati. ‎‎Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao cha pamoja cha viongozi wa JUWATA na UTPC kilichofanyika katika ofisi za UTPC zilizopo Barabara ya Aboud Jumbe, Mtaa wa Kazembo, eneo la Uzunguni jijini Dodoma. ‎Katika kikao hicho, viongozi hao walijadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya habari, ikiwemo umuhimu wa kuwa na mshikamano miongoni mwa wadau wa habari katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini. ‎Aidha, walisisitiza umuhimu wa taasisi hizo kushirikiana katika kutetea uhuru wa vyombo vya habari, haki za waandishi wa habari na maslahi yao, huku wakitambua nafasi muhimu ya wanahabari katika kuhabarisha, kuelimisha na kuwajibika katika jam...

MAKAMU WA RAIS AMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, UTOAJI WA TUZO ZA PYMA.*

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya utoaji wa tuzo za 19 za Rais za Wazalishaji Bora Viwandani, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Super Dome, Masaki Jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu wa Rais ametoa wito kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na wazalishaji wa saruji nchini, kuhakikisha wanatafuta suluhu ya haraka ili kurejesha bei ya kawaida ya saruji kwa wananchi. Amesema maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona wananchi wanaweza kununua mfuko wa saruji kwa gharama nafuu hivyo ni lazima kuoanisha uzalishaji wa malighafi zote zinazochangia katika uzalishaji wa saruji ili bidhaa hiyo ipatikane kwa urahisi. Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema ni muhimu kufanya tathimini ya ukuaji wa viwanda hapa nchini ili kutambua ukuaji huo kama unaviwezesha viwanda kuwa na ushindani wa masoko katika kanda, Afrik...

SHIRIKA LA NYUMBA KUJIPANGA KUKABILIANA NA ONGEZEKO LA WATU TANGA.

   Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Shirika la Nyumba Nchini (NHC) limejipanga kuendelea kutoa huduma ya makazi bora kwa wananchi  sambamba na kukabiliana na ongezeko la watu kutokana na kasi ya maendeleo na uhitaji uliopo Kwa sasa. Hayo yamesemwa na meneja wa  Shirika la Nyumba 'NHC' mkoa wa Tanga Mhandisi Mussa Kamendu alipokuwa akizungumza na waandshi wa habari ofisini kwake ambapo amesema kuwa  kutokana na kasi ya maendeleo inayochangiwa na uwepo wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ikiwepo Maboresho ya Bandari pamoja na ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi.  "Kazi yetu ni kujenga nyumba na kukarabati nyumba ambazo tunazo tayari,kwahiyo tumejinga vizuri kukabiliana na ongezeko la watu na ndio maana kuna miradi mingine ya nyumba inaendelea na pia tunashirikiana na sekta binafsi kwani shirika pekee yet hatuwezi kumaliza changamoto hii ya makazi ", alisema Mhandis. Kamendu  Aidha Mhandisi Kamendu amesema mpaka sasa kuna mradi wa nyumba 20 za makazi...

SHIRIKA LA NYUMBA KUJIPANGA KUKABILIANA NA ONGEZEKO LA WATU TANGA.

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Shirika la Nyumba Nchini (NHC) limejipanga kuendelea kutoa huduma ya makazi bora kwa wananchi  sambamba na kukabiliana na ongezeko la watu kutokana na kasi ya maendeleo na uhitaji uliopo Kwa sasa. Hayo yamesemwa na meneja wa  Shirika la Nyumba 'NHC' mkoa wa Tanga Mhandisi Mussa Kamendu alipokuwa akizungumza na waandshi wa habari ofisini kwake ambapo amesema kuwa  kutokana na kasi ya maendeleo inayochangiwa na uwepo wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ikiwepo Maboresho ya Bandari pamoja na ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi.  "Kazi yetu ni kujenga nyumba na kukarabati nyumba ambazo tunazo tayari,kwahiyo tumejinga vizuri kukabiliana na ongezeko la watu na ndio maana kuna miradi mingine ya nyumba inaendelea na pia tunashirikiana na sekta binafsi kwani shirika pekee yet hatuwezi kumaliza changamoto hii ya makazi ", alisema Mhandis. Kamendu  Aidha Mhandisi Kamendu amesema mpaka sasa kuna mradi wa nyumba 20 za makazi unaoen...