Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

PBPA YADHAMILIA KULINDA AFYA ZA MAMA LISHE NA KUTUNZA MAZINGIRA NCHINI.


 Na Mwandishi wetu Jovina Massano

Ili kulinda  afya za baba na mama lishe pamoja na kuhifadhi mazingira hapa nchini  Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) yahamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia Kurasini.

Hamasa hiyo ya matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kampeni za uhifadhi wa mazingira imetolewa na Mkurugenzi  wa Uendeshaji wa PBPA,Mhandisi Bruno Tarimo.

Mhandisi Tarimo amewahimiza mama na baba lishe kuachana na matumizi ya kuni na mkaa wa kawaida na kuhamia katika nishati safi ya kupikia ili kulinda afya zao sambamba na kuhifadhi mazingira lengo ikiwa  kuongeza ufanisi wa biashara zao.

Septemba 3, 2026,PBPA imetoa mafunzo ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa mama na baba lishe wa Kikundi cha Jitihada, yaliyofanyika Kurasini jijini Dar es Salaam na kuwakabidhi mama na baba lishe 70 jumla ya tani 1.7 za mkaa mbadala.

Mhandisi Tarimo ambae amemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa PBPA amesema mafunzo hayo ni sehemu ya ushiriki wa Wakala katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa miaka 10, uliozinduliwa mwaka 2024 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mkakati huo unalenga kuhakikisha kuwa, ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania watakuwa wamehama kutoka katika matumizi ya nishati zisizo safi na salama na kuanza kutumia nishati safi ya kupikia.

Amesema" Tumekuja kushirikiana na mama na baba lishe pamoja na watoa huduma wa teknolojia za nishati safi ili kuwapatia elimu kuhusu matumizi yake na kuwasaidia kuachana na nishati zisizo safi na salama".

Aidha ameeleza kuwa PBPA imeanza na mama na baba lishe wa Kurasini kwa sababu eneo hilo lina makampuni mengi ya mafuta ambayo ni miongoni mwa wadau wakuu wa Wakala.

Ameendelea kufafanua kuwa Wafanyakazi wa makampuni hayo hupata huduma za chakula kutoka kwa mama na baba lishe wanaofanya biashara katika maeneo ya Kurasini na Kigamboni.

“Wafanyakazi wanapokuja kula wataona chakula kimepikwa katika mazingira safi, hakina moshi na kina ladha nzuri. Wanaweza pia kuifikisha elimu hii kwa ndugu, jamaa na marafiki. Kwa namna hiyo, tunaendelea kuchangia utekelezaji wa lengo la kuwafikia asilimia 80 ya Watanzania,” amesema.

Katika mafunzo hayo, washiriki walipata fursa ya kuona na kujifunza matumizi ya majiko ya kisasa ya umeme, majiko banifu na mkaa mbadala. Pia walishuhudia kwa vitendo namna teknolojia hizo zinavyoweza kutumika kupika chakula kwa haraka, bila kutoa moshi mwingi wala kuchafua vyombo vya kupikia.

Matumizi ya kuni na mkaa wa kawaida yana madhara kwa afya za watumiaji, hususan mama na baba lishe ambao hukaa karibu na moshi kwa muda mrefu. Aidha, matumizi ya nishati hizo yanachangia uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji wa miti.

PBPA pia inaendelea kuzihamasisha taasisi zinazohudumia au kuandaa chakula kwa zaidi ya watu 100 kwa siku kuhamia katika matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia.

Kampeni hiyo inatarajiwa kuendelea katika maeneo mengine yenye mama na baba lishe wanaotoa huduma za chakula kwa wadau wa PBPA.

Nae Mwenyekiti wa Kikundi cha Jitihada, Bw. Lugano Mwaiswelo, amesema mafunzo hayo yamewapatia washiriki maarifa yatakayowasaidia kulinda afya zao na kuboresha mazingira katika maeneo ya biashara zao.

Hakusita kutoa shukrani Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia kwa kuwakumbuka mama na baba lishe kupitia jitihada za kuhamia katika nishati safi ya kupikia inasaidia kuboresha mazingira na kulinda afya zao.

"Tumepokea elimu hii kwa furaha, tutazingatia tuliyofundishwa na tutakuwa mfano kwa vikundi vingine kwa kutumia majiko banifu, mkaa mbadala na majiko ya umeme,” amesema Bw. Mwaiswelo.

Hata hivyo Bi. Joyce Benjamin Mtweve mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo amesema maonesho ya upishi yaliyofanyika yamewathibitishia kuwa matumizi ya nishati safi yanaweza kurahisisha kazi zao na kuboresha mazingira ya biashara.

“Tumefurahi sana kwa ujio wenu na kwa kutuonesha majiko ya nishati safi yakipika vizuri, bila moshi na bila kuchafua sufuria hivyo tupo tayari kuunga mkono juhudi hizi,” amesema Bi. Mtweve.

Akimalizia Rais wa Mama Lishe Tanzania, Bi. Latifa Habibu Masasi, amesema upatikanaji wa gesi, majiko ya umeme, majiko banifu na mkaa mbadala umewapa mama lishe fursa ya kuchagua teknolojia inayolingana na mahitaji pamoja na uwezo wao.

“Nishati safi ni muhimu sana na teknolojia hizi zinaongeza thamani katika mnyororo wa biashara ya chakula kwa sababu zinawawezesha mama lishe kupika kwa haraka, kwa wakati na katika mazingira salama zaidi,” amesema Bi. Masasi.

Mafunzo hayo yanaashiria kuanza kwa kampeni ya PBPA ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia miongoni mwa mama na baba lishe nchini.






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...