Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

SERIKALI NA TARI VYASHIRIKIANA KATIKA KUPAMBANA NA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU


 Na AngelaSebastian, Bukoba

Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Tanzania Relief Initiative (TARI) pamoja na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi imefanikiwa kuwaokoa jumla ya wahanga 160 wa usafirishaji haramu wa binadamu katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026.

Kati ya wahanga hao, 126 waliokolewa ndani ya mipaka ya Tanzania, huku 34 wakiokolewa kutoka nje ya nchi, hatua inayodhihirisha kuimarika kwa ushirikiano wa kitaifa na kimataifa katika kupambana na uhalifu huo.

Takwimu hizo zimetolewa na Afisa kutoka Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Joseph, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wasimamizi wa sheria mkoani Kagera.

Mafunzo hayo yamewakutanisha askari wa Polisi, Maafisa Uhamiaji, Waendesha Mashtaka wa Serikali na Mahakimu, yakilenga kuwaongezea uelewa wa namna ya kutambua, kuchunguza na kushughulikia kesi za usafirishaji haramu wa binadamu kwa ufanisi zaidi.

Joseph alisema Serikali imeelekeza nguvu zake katika maeneo manne muhimu ili kuhakikisha Watanzania pamoja na watu wote waliopo nchini wanakuwa salama dhidi ya mtandao wa usafirishaji haramu wa binadamu.

Alitaja maeneo hayo kuwa ni kuzuia uhalifu huo kupitia utoaji wa elimu kwa jamii, kuimarisha mfumo wa sheria, kuwalinda na kuwaokoa wahanga pamoja na kuhakikisha wahusika wanachukuliwa hatua za kisheria kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za Serikali, sekta binafsi na nchi washirika.

"Serikali imejipanga kuhakikisha hakuna Mtanzania anayejihusisha na usafirishaji haramu wa binadamu. Tunafanya hivyo kwa kutoa elimu, kuimarisha sheria, kuwaokoa na kuwalinda wahanga, kuwafikisha wahusika mahakamani na kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ndani na nje ya nchi," alisema Joseph.

Alifafanua kuwa Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu (The Anti-Trafficking in Persons Act Na. 6 ya mwaka 2008) imefanyiwa maboresho mara kadhaa, huku marekebisho ya hivi karibuni yakifanyika mwaka 2026 ili kuimarisha mapambano dhidi ya uhalifu huo.

Kwa mujibu wa Joseph, sheria hiyo inaweka adhabu kali kwa watakaobainika kujihusisha na usafirishaji haramu wa binadamu, ikiwemo faini ya kati ya Shilingi milioni 50 hadi milioni 300, kifungo cha hadi miaka 30 jela au adhabu zote mbili kwa pamoja, kutegemeana na uzito wa kosa.

Alisisitiza kuwa mafanikio ya mapambano hayo yanategemea ushirikiano wa wananchi, vyombo vya dola na wadau mbalimbali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanzania Relief Initiative (TARI), Edwin Mugambila, alisema mafunzo hayo yamelenga kuboresha uwezo wa wasimamizi wa sheria ili kuongeza ubora wa uchunguzi, ukusanyaji wa ushahidi na uendeshaji wa mashauri mahakamani.

Alisema takwimu zinaonyesha kuwa baadhi ya kesi zimekuwa zikiharibika kutokana na mapungufu katika upelelezi na ukusanyaji wa ushahidi, jambo linalowanyima haki wahanga wa uhalifu huo.

"Tunatarajia kuona maboresho makubwa kuanzia hatua za uchunguzi, upelelezi, ukusanyaji wa ushahidi hadi kesi zinapofikishwa mahakamani. Tukifanya kazi kwa weledi, wahalifu watawajibishwa kwa mujibu wa sheria na wahanga watapata haki yao," alisema Mugambila.

Alibainisha kuwa kwa Tanzania Bara, Mkoa wa Kagera unashika nafasi ya pili baada ya Morogoro miongoni mwa mikoa 10 inayoongoza kwa matukio ya usafirishaji haramu wa binadamu.

Mikoa mingine iliyotajwa ni Iringa, Dar es Salaam, Mwanza, Tabora, Geita, Shinyanga, Mara na Kilimanjaro.

Alieleza kuwa Kagera ni mkoa wa kimkakati kutokana na mipaka yake na nchi kadhaa za Afrika Mashariki, hali inayoufanya kuwa njia mojawapo inayotumiwa na mitandao ya usafirishaji haramu wa binadamu.

Mugambila amesema watoto wa kike na wanawake ndio waathirika wakubwa wa biashara hiyo haramu, huku maeneo ya vijijini na mipakani yakiongoza kwa matukio mengi.

Ameeleza kuwa mara nyingi wahanga hutoka katika familia zenye kipato cha chini na hurubuniwa kwa ahadi za ajira zenye mishahara mikubwa, elimu au maisha bora.

Baada ya kukubali safari hizo, baadhi yao huishia kulazimishwa kufanya kazi za ndani bila malipo stahiki, biashara ya ngono, kuombaomba au kazi nyingine za kinyonyaji huku wakinyang'anywa nyaraka zao za kusafiria, simu na kuzuiwa kuwasiliana na familia zao.

Katika matukio mengine, alisema wahanga hukumbana na vitisho, unyanyasaji na hata biashara haramu ya viungo vya binadamu.

Mugambila aliwataka wananchi kuwa makini wanapoona watu wanaowafuata watoto au vijana kwa ahadi za kazi bila kufuata taratibu za Serikali.

Aliwashauri kutoa taarifa mapema kwa vyombo vya dola au kupiga simu ya bure 195 ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ili kupata ushauri na msaada.

"Ushirikiano wa wananchi ni silaha muhimu katika kukomesha biashara hii haramu. Taarifa zinazotolewa mapema zinaweza kuokoa maisha ya watu wengi na kuwafikisha wahalifu mbele ya sheria," amesema.

Wakili wa Serikali na Mwendesha Mashtaka Kiongozi Mkoa wa Kagera, Amani Kyando, amesema mafunzo hayo yataongeza uwezo wa waendesha mashtaka katika kushughulikia kesi za usafirishaji haramu wa binadamu na kuwasaidia wahanga kutoa ushahidi unaokubalika mahakamani.

Naye Mkuu wa Dawati la Jinsia, Wanawake na Watoto wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera, Mkaguzi wa Polisi Suzan Kamwaga, amesema polisi ndio hupokea taarifa nyingi za awali kutoka kwa wahanga, hivyo mafunzo hayo yatawawezesha kuandaa majalada ya uchunguzi kwa weledi na kuondoa mianya inayoweza kuhatarisha kesi mahakamani.

Amesema wahanga wengi wanaokutana nao ni watoto wa kike, wafanyakazi wa ndani na watu wanaoingia au kuishi nchini bila vibali halali.




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...