Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAZIRI MAVUNDE AZINDUA PROGRAMU YA KESHO ILIYO NJEMA KATIKA SEKTA YA MADINI (MBT)


▪️Azindua na Zoezi la Urushaji wa Helikopta ya Utafiti wa Madini ya Barrick 

▪️Maeneo ya Leseni za Vijana,Wanawake na Wenye Ulemavu Kufanyiwa Utafiti kwa Helikopta

▪️Rais Dkt. Samia Apongezwa kwa Maelekezo na Maono Yake Sekta ya Madini

▪️Baraza la Dhahabu Duniani Lavutiwa na Programu ya MBT

▪️Waziri Mavunde Aagiza Mitambo ya Uchorongaji ya STAMICO Kufika Mara Baada ya Utafiti Kukamilika

📍Nyamongo, Mara. 

Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amezindua rasmi Programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT), maarufu kama “Kesho Iliyo Njema,” na kueleza kuwa programu hiyo ni hatua ya kimkakati ya Serikali katika kufungua milango mipya ya fursa na uwezeshaji kwa vijana, wanawake na watu wenye mahitaji maalum kushiriki kikamilifu katika Sekta ya Madini na kwamba programu inalenga kuwasaidia walengwa kuondokana na uchimbaji wa kubahatisha na kuelekea kwenye uchimbaji wenye tija, unaotumia maarifa, teknolojia na taarifa sahihi za kijiolojia, huku Serikali ikiendelea kuweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa maeneo ya uchimbaji, leseni na fursa za kiuchumi zinazotokana na rasilimali madini.

Waziri Mavunde amebainisha hayo, leo Agosti 31, 2026, katika eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime, Mkoani Mara, wakati akizungumza katika hafla hiyo iliyokwenda sambamba na uzinduzi wa utafiti wa kina wa madini unaofanywa na Barrick Gold Corporation, 


Mhe. Mavunde ametumia nafasi hiyo kumpogeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maelekezo na maono yake ya kuweka mazingira wezeshi kwa makundi hayo na kuongeza kuwa Rais Dkt. Samia ameagiza asilimia 10 ya mapato yatokanayo na makusanyo ya Sekta ya Madini kutengwa kwa ajili ya utafiti wa kina wa madini, hatua ambayo inalenga kuongeza taarifa za rasilimali madini nchini na kufungua fursa zaidi kwa wananchi.

Waziri Mavunde pia ameishukuru Barrick kwa kukubali kufanya utafiti katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wachimbaji wadogo Nyamongo, akieleza kuwa ndani ya wiki mbili utafiti huo unaweza kufanyika katika eneo lenye ukubwa wa takribani kilomita za mraba 6,000 na kusisitiza kuwa dhamira ya Serikali kuhakikisha matokeo ya utafiti yanageuka kuwa fursa halisi kwa wananchi, sambamba na kumuelekeza Kamishna wa Madini, kwa kushirikiana na GST na STAMICO, kukaa na Barrick na kuhakikisha mara utafiti utakapokamilika, mitambo ya uchorongaji inafika Nyamongo kwa ajili ya hatua inayofuata ya utafiti.

Aidha, Waziri Mavunde amesema uzinduzi huo unaashiria mwanzo wa safari ya kujenga “Kesho Iliyo Njema” katika Sekta ya Madini, huku akieleza kuwa Rais wa Baraza la Dhahabu Duniani (World Gold Council) amevutiwa na programu ya MBT na kwamba vijana wa Nyamongo ndio watakaokuwa miongoni mwa vijana wa kwanza kunufaika na mpango huo. 

“Tunaenda kupanda mbegu, tunaanza safari; leo mnaianza safari ya kwenda kubadilisha maisha yenu na mimi nitasimamia programu hii ili tufikie lengo,” amesema Mavunde.

Kwa upande mwingine, Waziri Mavunde amesema kuwa amedhamiria kuipima Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa ya Kimadini kwa kuhakikisha maeneo maalum yanatengwa kwa ajili ya makundi ya vijana na wanawake, huku leseni zikitolewa kwa kasi ili kuwawezesha kushiriki katika shughuli za uchimbaji, amesema lengo ni kuona programu ya MBT ikienda sambamba na ukusanyaji wa maduhuli na kwamba angependa kuona kila siku fursa mpya za leseni zikitolewa kwa vijana kupitia programu hiyo. Aidha, ametoa wito kwa viongozi wa vijana wachimbaji kuweka pembeni tofauti zao, kushirikiana na kuepuka kuwagawa vijana, akisisitiza kuwa Serikali haitakubali migogoro ya makundi iwe kikwazo cha utekelezaji wa programu hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Brigedia Jenerali Evans Mtambi amesema kuwa, Kupitia programu hiyo na tafiti zinazofanyika, tunaamini vijana wataweza kuchimba kisayansi zaidi, kwa kutumia taarifa na teknolojia badala ya kuchimba kwa kubahatisha na kwamba hatua hiyo itasaidia kupunguza gharama na hasara zisizo za lazima, kuongeza tija na hatimaye kuwawezesha wachimbaji wetu kupata matokeo makubwa zaidi kutokana na juhudi wanazoweka katika shughuli zao na kwamba ukosefu wa taarifa sahihi zinazoweza kuwaongoza wachimbaji kujua madini yapo wapi kwa kiwango gani na namna bora ya kuyafikia ndiyo ilikuwa changamoto kubwa.

Awali, Meneja Mkazi (Country Manager) wa Kampuni ya Barrick Gold nchini Tanzania, Dkt. Melkiory Ngido ameeleza kuwa kama Barrick wanajivunia kuwa miongoni mwa wadau walioshiriki katika programu tangu mwanzo. 

“Tulichukua hatua ya kimkakati ya kurudisha leseni ya eneo ambalo tayari tulikuwa tumelifanyia utafiti na kubaini kuwa lina uwezo wa kutoa fursa kwa makundi ya wachimbaji wadogo. Tuliona ni muhimu eneo hilo lisibaki chini ya umiliki wetu wakati linaweza kuwa chanzo cha ajira, kipato na fursa za kiuchumi kwa Watanzania wanaojihusisha na uchimbaji mdogo. Hatua hii inaakisi dhamira yetu ya kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha rasilimali za madini zinawanufaisha wananchi na zinachangia maendeleo ya jamii zinazozunguka maeneo ya migodi.” Amesema Ngido

Makamu Rais wa FEMATA, Victor Tesha ameeleza kuwa wao kama wachimbaji wadogo wa madini nchini Tanzania wanayo furaha kubwa kwa hatua hii iliyofikiwa na wanaiona programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT) kama hatua muhimu sana katika kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikituathiri kwa muda mrefu, ameongeza kuwa wana imani kubwa na Serikali na wanaamini kupitia programu hiyo, maisha ya wachimbaji wadogo na familia zinazotegemea shughuli za madinj yanaenda kubadilika kwa kiwango kikubwa. 








Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...