Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MUSWADA WA SHERIA YA MIKOPO KWA DHAMANA ZA MALI ZINAZOHAMISHIKA WAWASILISHWA BUNGENI


 Na Joseph Mahumi na Peter Haule, Dodoma

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amewasilisha Bungeni Muswada wa Sheria ya Mikopo kwa Dhamana za Mali Zinazohamishika wa Mwaka 2026, unaolenga kuweka mfumo bora wa usimamizi wa mikopo inayotolewa kwa kutumia mali zinazohamishika kama dhamana.

Akiwasilisha Muswada huo Bungeni jijini Dodoma, Mhe. Balozi Omar amesema Sheria hiyo inayopendekezwa inalenga kuongeza matumizi ya huduma za benki nchini kutoka asilimia 22 mwaka 2023 hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.



Mhe. Balozi Omar amesema pia Muswada huo unalenga kuongeza uwiano wa mikopo inayotolewa kwa sekta binafsi dhidi ya Pato la Taifa kutoka asilimia 22.5 mwaka 2024 hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030, sambamba na kuongeza ajira na kuchochea ukuaji wa sekta ya fedha kufikia asilimia 20 ifikapo mwaka 2030, kutoka asilimia 17.1 mwaka 2024.

Alisema kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kupanua wigo wa wananchi na wafanyabiashara kupata mikopo kwa kutumia mali zinazohamishika kama dhamana, badala ya kutegemea zaidi mali zisizohamishika kama vile ardhi na majengo.

Aidha Mhe. Balozi Omar alisema miongoni mwa changamoto zinazolengwa kutatuliwa na Muswada huo ni kutokuwepo kwa mfumo wa pamoja wa usajili wa mali zinazohamishika zinazoweza kutumika kama dhamana, ambapo hali hiyo imekuwa ikisababisha mali moja kutumika kama dhamana kwa mikopo mbalimbali bila wakopeshaji wengine kuwa na taarifa, jambo ambalo linaweza kuchangia kuongezeka kwa mikopo chechefu katika sekta ya fedha.

Changamoto nyingine ni kukosekana kwa usimamizi na utaratibu wa pamoja wa mali zinazohamishika zinazoweza kutumika kama dhamana, pamoja na kutokuwepo kwa utaratibu madhubuti wa utekelezaji wa haki za mkopaji na mkopeshaji wakati wa kuuza mali hizo.

Mhe. Balozi Omar, aliongeza kuwa umuhimu wa kuweka utaratibu huo unatokana pia na ukweli kwamba baadhi ya mali zinazohamishika zinaweza kupoteza thamani ndani ya muda mfupi au kuharibika.

Alibainisha kuwa Muswada huo umegawanyika katika sehemu kumi zinazoweka mfumo mpana wa kisheria wa matumizi, usajili, usimamizi na utekelezaji wa dhamana zinazotokana na mali zinazohamishika.

Mhe. Balozi Omar alisema Sehemu ya Kwanza, inahusu masharti ya utangulizi, ikiwemo jina la Sheria, kuanza kutumika kwake, matumizi ya Sheria na tafsiri ya misamiati huku Sehemu ya Pili inaanzisha masharti ndani ya Benki Kuu ya Tanzania yanayohusu dhamana na kuainisha mamlaka ya Benki pamoja na ukasimishaji wa majukumu.

Aliongeza Sehemu ya Tatu inaainisha maslahi katika dhamana kwa mkopo mmoja au zaidi, pamoja na aina za mali zinazoweza kutumika kama dhamana, zikiwemo mali zinazoshikika na zisizoshikika, zinazoweza kuhamishika au zisizoweza kuhamishika, na Sehemu hiyo pia inaweka sharti la Benki Kuu kushauriana na Waziri kabla ya kutangaza mali zinazoweza kutumika kama dhamana.

Sehemu ya Nne inahusu usajili wa maslahi katika dhamana, muda wa uhalali wa usajili, marekebisho au ufutaji wa usajili pamoja na upekuzi wa taarifa, huku Sehemu ya Tano inahusu maslahi katika dhamana dhidi ya mtu wa tatu, maslahi katika mapato yanayotokana na dhamana pamoja na utekelezaji wa maslahi katika mali zinazohamishika zilizochanganywa.

Aidha, alisema Sehemu ya Sita inaainisha vipaumbele katika maslahi ya wakopaji tofauti, mapato na malipo yanayochanganywa kwa mkusanyiko, pamoja na athari za kufilisika kwa mkopaji, ikiweka masharti kuhusu haki za wahusika mbalimbali katika matumizi ya dhamana na haki ya kipaumbele katika maslahi ya dhamana.

Kwa mujibu wa Mhe. Balozi Omar, alisema Sehemu ya Saba inaainisha haki ya kukagua dhamana, wajibu wa kutoa taarifa, jukumu la kutunza dhamana, pamoja na haki na wajibu wa mdaiwa, ambapo pia inahusu madai ya malipo yaliyofanywa na mdaiwa, haki katika makusanyo yanayotarajiwa, mali au hati za malipo zinazowezesha malipo au utekelezaji wa dhamana, pamoja na ulinzi wa haki za mkopaji.

Aliongeza kuwa Sehemu ya Nane inaweka masharti yanayohusu utekelezaji wa dhamana, ikiwemo usajili wa taarifa za utekelezaji, uondoshaji wa dhamana, matumizi ya dhamana katika kutekeleza wajibu unaotokana na mkopo na utaratibu wa uondoshaji wa dhamana. 

Sehemu hiyo pia inaainisha ukomo wa maslahi katika dhamana baada ya uondoshaji, mgawanyo wa mapato, pendekezo la kumiliki dhamana katika malipo ya deni na utaratibu wa kuweka pingamizi dhidi ya pendekezo hilo. Aidha, inaweka masharti kuhusu uhifadhi wa dhamana, gharama za uhifadhi na haki ya mkopaji kuchagua sehemu mbadala ya kuhifadhi dhamana.

Mhe. Balozi Omar, alisema Sehemu ya Tisa inahusu masharti ya jumla, ikiwemo utekelezaji wa haki na wajibu, haki ya kudai fidia dhidi ya ukiukwaji wa wajibu, kinga, kosa la kutoa taarifa za uongo, malalamiko na mapitio ya maamuzi ya Benki pamoja na rufaa, ambapo Sehemu hiyo pia inampa Waziri mamlaka ya kutengeneza kanuni kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji bora wa Sheria hiyo.

Sehemu ya Kumi inaainisha marekebisho ya sheria mbalimbali pamoja na Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania, Sheria ya Kampuni, Sheria ya Ufilisi na sheria nyingine zinazohusiana na usimamizi wa mali na masuala ya kifedha, yanayopendekezwa kufanyika ili kuwezesha utekelezaji wa Muswada huo.

Mhe. Balozi Omar, alisema kuwa kutungwa kwa Sheria hiyo kutasaidia kuweka mazingira bora ya upatikanaji wa mikopo, kuimarisha usimamizi wa dhamana, kulinda haki za wakopaji na wakopeshaji, na kuchochea maendeleo ya sekta ya fedha nchini.



Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...