Na Angela Sebastian, Kagera KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2026, Wazo Michael Mwang’onda, amepongeza ushiriki wa makundi maalumu katika mbio hizo wilayani Muleba, mkoani Kagera, akisema hatua hiyo ni ishara kuwa Mwenge wa Uhuru ni mali ya wananchi wote bila kujali hali zao katika jamii. Mwang’onda alitoa kauli hiyo jana wakati wa ziara ya Mwenge huo wilayani Muleba, ambapo alieleza kufurahishwa na namna makundi hayo yalivyoshiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za mbio hizo. Alisema ushiriki huo unaakisi umoja, mshikamano na jitihada za Serikali za kuwahusisha wananchi katika shughuli za maendeleo. Katika hatua hiyo, Mwang’onda akiwa na Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, aliwakabidhi Mwenge huo makundi maalumu na kushiriki nao katika shughuli mbalimbali, jambo lililowapa furaha na kuifanya mbio hiyo kuwa jukwaa la wananchi wote. Alisema kwa sasa Mwenge umekabidhiwa kwa wananchi, hivyo ni muhimu kila kundi kushiriki katika kuunga mkono juhudi za kuleta mae...
Marato tv - Sauti ya Jamii