ELIMU NA HAMASA NZURI YAWAFANYA WAZAZI NA WALEZI KATA YA MWISENGE KUHAKIKISHA WATOTO WAO WANAPATA CHANJO YA POLIO.
Na Mwandishi wetu Jovina Massano Musoma.
ELIMU na hamasa nzuri kwa jamii yasababisha wazazi,watoto na walezi Kata ya Mwisenge Manispaa ya Musoma mkoani Mara kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo ya Polio awamu ya tatu.
Hayo yamesemwa na wazazi na walezi Agosti 30, 2026 katika mitaa na maeneo ya Ibada mara baada ya kufikiwa na timu ya utoaji chanjo.
Wamesema kuwa wahamasishaji wakiwemo wenyeviti wa mitaa na taarifa zinazotolewa katika vyombo vya habari zimewafanya wamepata hamasa na uelewa mpana wa umuhimu wa chanjo hiyo.
Wakizungumza kwa Nyakati tofauti wamesema utoaji elimu mapema ni muhimu kwa kuwa inasaidia kupata taarifa na uelewa usahihi wa zoezi husika.
Frank David afisa usafirishaji wa Mtakuja Kituo Cha mianzini ni miongoni mwa wazazi ambae nae mtoto wake ameweza kupata chanjo hiyo.
Amesema hapo awali watu waliongea vibaya kuhusiana na chanjo ya Polio wengi walipata hofu lakini hivi sasa baada ya kupewa elimu kwa usahihi imewapa ujasiri wa kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo hiyo kikamilifu.
Hata hivyo zoezi la utoaji chanjo limefika mpaka kwenye nyumba za Ibada na baadhi ya watoto ambao hawakufikiwa wamewafuata watoa huduma na kupata chanjo hiyo.
Kwa Upande wao wenyeviti wa mitaa ya VETA Goodluck Kuboja Nyamwero na Mtakuja "A" Aloyce Masatu Lawi wamewashukuru wazazi, walezi na wananchi wote kwa kuonesha ushirikiano kwa kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo iliyoandaliwa na wataalam wa afya.
"Sisi kama wenyeviti wa Serikali ya mitaa kabla ya kuchanja ilibidi tuwatangazie kwenye mitaa yetu wananchi waliitikia na kila mwenye mtoto ameweza kufikiwa".
Pia wamewashukuru Viongozi wa nyumba za Ibada kutoa ushirikiano na kuweza kukamilisha zoezi hili la chanjo.
Akimalizia Mtoa huduma ya Chanjo mtaa wa VETA Chausiku Joram Makanya amewashukuru wazazi,walezi,walimu na wananchi wote kwa ujumla kwa ushirikiano wao na kuwa na mwitikio mkubwa na kuwezesha huduma ya utoaji chanjo bila kuwepo kwa changamoto yeyote.
Miongoni mwa watoa huduma ya utoaji chanjo walioweza kufikiwa na GMTV wakati wakiendelea na zoezi la chanjo ni pamoja na Dorcas Masanja mtoa huduma ,Nyakwesi James Mtakwimu Aloyce Masatu Lawi Mwenyekiti wa mtaa pia ni mhamasishaji Msimamizi wa zoezi la chanjo mtaa wa Mtakuja A.









Comments
Post a Comment