Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

SHULE ZIIGE MFANO WA BUNAZI GREEN ACRES KUFUNDISHA TEHAMA


 Na Mwandishi Wetu

Serikali imezitaka shule nchini kuweka kipaumbele kwenye mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA kwa wanafunzi wao ili kwenda sanjari na dunia ya sasa ya utandawazi na teknolojia inayokua kwa kasi.

Imesema kwa dunia ya sasa teknolojia inakwenda kwa kasi kubwa hivyo shule zinapaswa kuwa na miundombinu bora ya wanafunzi wake kujifunza TEHAMA huku ikiipongeza shule ya Bunazi Green Acres iliyoko mji mdogo wa Bunazi Kata ya Kassambya wilayani Misenyi kwa kuwa mfano kwenye eneo la mafunzo ya TEHAMA.

Ushauri huo ulitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera, Phocus Rwegasira, wakati wa mahafali ya 10 ya shule hiyo ya Bunazi Green Acres iliyoko mji mdogo wa Bunazi Kata ya Kassambya wilayani Misenyi yaliyofanyika shuleni hapo ambapo yeye alikuwa mgeni rasmi.

Alisisitiza kuwa mafunzo ya teknolojia ni muhimu kwani dunia inakwenda kwa kasi kwenye eneo hilo huku akisisitiza pia umuhimu wa ushirikiano kati ya wazazi, walimu na jamii katika kuhakikisha watoto wanapata elimu bora na malezi yanayowaandaa kuwa viongozi na wataalamu wa baadaye.

Alisema pamoja na shule hiyo kuweka miundimboinu bora na ya kisasa lakini mafanikio ya mwanafunzi hayawezi kutenganishwa na juhudi za walimu, wazazi na uongozi wa shule, hivyo kila upande unapaswa kutekeleza wajibu wake kwa umakini.

Rwegasira pia aliwahimiza wahitimu kuwa na nidhamu, bidii na kujituma katika masomo yao ya ngazi zinazofuata, akiwataka kutumia fursa za elimu kujenga maisha yao na kuchangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Aidha, aliwataka wazazi kuendelea kuwa karibu na watoto wao, kufuatilia maendeleo yao ya kitaaluma na kuwajengea misingi mizuri ya maadili.

Katika hafla hiyo, Rwegasira alikabidhi vyeti kwa baadhi ya wahitimu, huku akipongeza uongozi wa Bunazi Green Acres kwa kutimiza miaka 10 ya mahafali na kuendelea kutoa mchango katika sekta ya elimu nchini.

Mkurugenzi wa Shule ya Bunazi Green Acres, Jackline Rushaigo, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya shule, wazazi na jamii katika kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora na malezi yenye misingi ya maadili.

Alisema mafanikio yaliyofikiwa na shule hiyo ni matokeo ya juhudi za pamoja za walimu, wazazi, wanafunzi na wadau wa elimu.

Aliwapongeza wanafunzi waliohitimu kwa hatua waliyofikia na kuwataka kuendelea kuwa na nidhamu, bidii na kujituma katika masomo yao ya ngazi zinazofuata.

Aidha, aliwashukuru wazazi na walezi kwa kuendelea kuiamini shule hiyo na kushirikiana na uongozi katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunza na kukua kitaaluma na kimaadili.

Mkuu wa shule hiyo, Geoffrey Moses alisema shule hiyo tangu kuanzishwa kwake miaka 10 iliyopita imepata mafanikio makubwa kwani wanafunzi wake wote wamekuwa wakipata daraja A katika matokeo ya mitihani ya kitaifa inayotangazwa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA).

Alisema shule imejitahidi kuboresha miundombinu yake kwa kujenga majengo sita ya madarasa yenye vyumba 25 vya kujifunzia na imejanga maabara ya kisasa ya TEHAMA yenye huduma za mtandao kwaajili ya mafunzo kwa vitendo.

Alisema shule imejitahidi kujenga maktaba yenye vitabu vingi vya kiada na vya ziada na mabweni sita yenye vitanda kwa kila mwanafunzi na kwamba mazingira hayo ndiyo yameiwezesha shule kutoa huduma bora na matokeo mazuri kila mwaka.

“Tunajivunia kwamba miaka yote 10 tangu shule ianze tumefanya vizuri kitaaluma tumeshatoa wanafunzi 500 kwa miaka yote 10 na muda wote huo shule imekuwa ikipata wastani wa alama 251 ambayo ni darasa A bora,” alisema

Aidha, alisema mafanikio ya shule hiyo yametokana na juhudi kubwa za walimu wake nidhamu ya wanafunzi na ushirikiano mkubwa wa wazazi na serikali kuanzia ngazi ya kata hadi nagzi ya Wizara.

“Mwaka huu tuna wahitimu 64 wa darasa la saba ambao tunaamini wataendeleza historia yetu nzuri ya kitaaluma kwasababu wameandaliwa vizuri sana,” alisema

Aidha, Mkuu huyo wa shule alisema katika kutambua ulimwengu unavyokwenda kwa kasi kwenye teknolojia, shule imeanzisha maabara ya TEHAMA yenye mtandao ili kuwapa wanafunzi ujuzi wa kompyuta kwa vitendo.

“Wanafunzi wetu wanajivunia kutumia teknolojia kwa kujiamini na kwa ubinifu hivyo tunaamini ujuzi huu utawaandaa kushindana na kufanikiwa katika dunia ya sasa,” alisema mwalimu Mosses






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...