Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MKUU WA MKOA AZINDUA 'INNOIP TANZANIA': WABUNIFU 5,000 NA WANAWAKE KUNUFAIKA

Na MASHAKA MHANDO, Tanga

SERIKALI imezindua rasmi programu mpya ya kitaifa ijulikanayo kama InnoIP Tanzania, inayolenga kuwasaidia wabunifu zaidi ya 5,000 nchini kulinda haki zao za miliki bunifu kisheria na kuzigeuza kuwa biashara zinazoingiza fedha na kutengeneza ajira, ili kuepuka wizi wa mawazo unaowaathiri wabunifu wengi wazawa.

Uzinduzi huo wa kihistoria umefanywa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian Leo Augosti 22 wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi, na Ubunifu yanayoendelea katika viwanja vya Usagara jijini Tanga, hafla iliyobebwa na kaulimbiu isemayo; "Kutoka Wazo hadi Fursa za Miliki Bunifu: Kulinda Ubunifu, Kujenga Thamani na Kuharakisha Ubiasharishaji".

Akihutubia mamia ya wadau wa sekta ya sayansi na ubunifu, Mkuu wa Mkoa alisema Tanzania lazima ihakikishe ubunifu wa ndani unalindwa na kuunganishwa na masoko makubwa, ili kuepuka hasara inayosababishwa na wabunifu kuweka wazi mawazo yao mapema mno kwa umma kabla ya kuyalinda kisheria.

Dkt. Batilda alibainisha kuwa hali ya wabunifu kuweka wazi mawazo yao bila makubaliano yanayoeleweka kuhusu umiliki, inamkosesha mbunifu fursa ya kupata ulinzi wa kazi yake, na inawafanya wawekezaji wasite kumwaga mitaji yao iwapo kampuni changa haithibitishi umiliki wake kisheria.

Sambamba na uzinduzi wa InnoIP, Mkuu wa Mkoa alitangaza pia kuanza kwa programu ya 'Fursa Women', inayolenga kuwainua wanawake wajasiriamali kwa kuwapa ujuzi wa kutumia teknolojia na mifumo ya kidijitali ili kukuza biashara zao, akisisitiza kuwa teknolojia hupunguza gharama za uendeshaji na kuongeza wateja haraka.

Katika kuhakikisha mafanikio ya mipango hiyo, Mkuu wa Mkoa alitoa maagizo mazito kwa Vyuo Vikuu na taasisi za utafiti nchini kuhakikisha wanatengeneza bidhaa halisi zinazonufaisha jamii badala ya kuziacha tafiti zikioza kwenye makabati, huku akiwaasa wawekezaji na taasisi za fedha kushirikiana na wabunifu wa Kitanzania kwa kununua bidhaa zao na kuwapa mitaji.

Kwa upande wake, akizungumzia ushiriki wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika programu hiyo, Mkurugenzi wa Miliki akimwakilisha Afisa Mtendaji Mkuu, Loy Mhando  alieleza kuwa programu hiyo haimaanishi kuwa kila ubunifu lazima upatiwe Hataza (Patent), bali inamsaidia mbunifu kutambua mbinu sahihi za ulinzi ikiwemo alama za biashara, hakimiliki, na siri za biashara.

Alifafanua kuwa InnoIP inasimamiwa na BRELA ikiratibiwa na COSTECH kupitia atamizi za Dar Teknohama Business Incubator (DTBi) na Buni Innovation Hub, ambapo itawasaidia kampuni changa, watafiti, wanafunzi wa vyuo vikuu, biashara ndogo na za kati, na wajasiriamali kutambua, kulinda, na kubiasharisha haki zao za miliki bunifu.

Alieleza kuwa katika mwaka wa kwanza wa utekelezaji, programu hiyo inalenga kufanya uchambuzi wa mahitaji ya kina kwa wabunifu 120 wa mwanzo, ambao watasaidiwa kisheria na kifedha kulinda kazi zao, kisha kuunganishwa na wawekezaji, ambapo wabunifu hao watapatikana kwa kuzingatia vigezo vya umuhimu wa ubunifu husika kwa jamii na uwezo wa kuingiza faida.

Alisema kuwa  programu hiyo itawasindikiza wabunifu kupitia hatua saba ikiwemo utambuzi na uhamasishaji, mafunzo na warsha za vitendo, uchambuzi wa mahitaji, maandalizi ya ramani ya ulinzi, kuwasilisha maombi ya usajili, ubiasharishaji kwa kuwatafutia wawekezaji, na hatimaye ufuatiliaji endelevu.

Mhando aliwataka wabunifu na kampuni changa nchini kutumia programu hiyo mapema na kutosubiri hadi mgogoro wa umiliki utokee, wazo linakiliwe na wajanja, au mwekezaji aanze kudai uthibitisho wa kisheria wa biashara zao.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, akitoa hotuba ya ukaribisho, alisema miliki bunifu si suala la kisheria pekee, bali ni rasilimali ya kiuchumi ambayo inaweza kuwa msingi mkuu wa kuvutia uwekezaji, kutoa leseni kwa viwanda vingine, kuhamisha teknolojia, na kujenga biashara kubwa zinazoweza kukua kimataifa.

"Changamoto yetu kuu kwa sasa nchini si ukosefu wa mawazo; ni kuhakikisha kuwa mawazo mazuri ya vijana, watafiti na wabunifu wetu yanalindwa kisheria, yanaendelezwa na hatimaye yanafikishwa sokoni," alisema Dkt. Nungu alipokuwa akisisitiza dhima kuu ya programu hiyo.

Mkurugenzi huyo wa COSTECH alisisitiza kuwa lengo kuu la programu hiyo si kuhesabu idadi ya watu waliohudhuria mafunzo na semina, bali matokeo ya InnoIP yatapimwa kwa kuona idadi ya ubunifu mwingi zaidi ukilindwa, teknolojia mpya zikiingia sokoni, biashara zikikua, uwekezaji mkubwa ukivutwa, na ajira nyingi mpya zikizalishwa nchini.

Akizungumzia Programu ya 'Fursa Women', Dkt. Nungu aliishukuru Kampuni ya simu ya Airtel Tanzania kwa ushirikiano wake na COSTECH katika kufadhili programu hiyo, akieleza kuwa ushirikiano huo unaonesha umuhimu wa sekta ya umma na binafsi kufanya kazi pamoja katika kujenga jamii yenye ujuzi wa kidijitali.

Alifafanua kuwa kupitia Fursa Women, wanawake watajengewa uelewa kuhusu matumizi sahihi na salama ya mifumo ya kidijitali katika kutangaza bidhaa, kuwafikia wateja wengi, kufanya na kupokea malipo mtandaoni, na kuhifadhi kumbukumbu za biashara zao.

Dkt. Nungu alihitimisha kwa kutoa wito kwa wawekezaji na sekta binafsi kutambua kuwa ubunifu wa Kitanzania ni fursa ya uwekezaji iliyolala, hivyo akawaalika kushirikiana na Serikali katika kujaribu, kununua, na kupanua matumizi ya teknolojia na suluhisho mbalimbali zinazozalishwa na Watanzania wazawa.

Maonesho ya wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanatarajiwa kufungwa Jumatatu na Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba.







Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...