Hayo amebainisha baada ya kukagua daraja hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambapo ameagiza TARURA kufanya ukaguzi na kutoa tathimini kwenye eneo la daraja hilo ambapo Tathimini hiyo itabaini kama panafaa kujengwa daraja jipya au ipendekezwe eneo jingine litakalokuwa linaungana na barabara ili daraja hilo liweze kujengwa kwa haraka.
Chalamila amesema ujenzi wa daraja la kudumu ni muhimu ili kuondoa hofu na usumbufu unaowapata wananchi kila msimu wa mvua. Amesisitiza kuwa Serikali haiwezi kuruhusu miundombinu inayoweka maisha ya wananchi hatarini iendelee kutumika bila kuboreshwa.
Chalamila ametoa maagizo hayo leo Agosti 17, 2026 katika ziara ya kukagua ujenzi wa barabara ya Masaki iliyopo Toangoma pamoja na ya Ndunguru iliyopo Kibondemaji Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam ambapo ziara hiyo inalenga kuhakikisha miradi ya miundombinu inaendelea kwa kasi na kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Aidha amewataka wananchi wa Twangoma na maeneo jirani kuwa watulivu wakati zoezi la ukaguzi na tathimini likiendelea huku malengo ya Serikali ni kuhakikisha kuwa kila eneo linalopitwa na wananchi linakuwa na miundombinu imara na salama inayoweza kutumika muda wote bila vikwazo.
Mkuu wa mkoa Ameeleza kuwa Serikali ya Mkoa itashirikiana na TARURA na wadau wengine kuhakikisha changamoto ya daraja la Goloka B inapatiwa ufumbuzi wa kudumu. Aidha amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za maeneo mengine yenye changamoto kama hiyo ili hatua stahiki zichukuliwe mapema.










Comments
Post a Comment