Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TRA IMEANZA VIZURI MAKUSANYO JULAI, 2026, WANANCHI TUENDELEZE UAMINIFU ULIPAJI KODI

 


NA: DK. REUBENI LUMBAGALA 


Katika maisha ya kawaida ya mwanadamu, kuna kuweka malengo ili kufikia mafanikio. Inapotokea malengo yametimia, moyo hujaa furaha kwani mlango wa kufanikiwa unakuwa umefunguka.

Haya ndiyo yaliyotokea kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kwa TRA, mwaka wa fedha 2026/2027 umeanza vizuri. Hii ni kufuatia Mamlaka hiyo kukusanya shilingi trilioni 3.245 kwa mwezi Julai, 2026, ambapo makusanyo hayo ni sawa na asilimia 109 ya lengo la kukusanya trilioni 2.971 kwa mwezi huo.

Ni kwamba; mwaka mpya wa fedha huanza Julai 1 ya kila mwaka. Hivyo mwezi wa kwanza wa mwaka mpya wa fedha ni kuanzia Julai 1 hadi 31. Kwa malengo ambayo TRA ilijiwekea, ni kukusanya shilingi trilioni 2.971, lakini lengo hilo limetimia na kuzidi, ambapo zimekusanywa shilingi trilioni 3.245. 

Kimsingi, bajeti iliyopitishwa na bunge kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ni shilingi trilioni 62.33, ambapo asilimia 74 ya fedha hizo zinategemewa kukusanywa kupitia mapato ya ndani (own sources).

Katika fedha hizo, TRA inawajibika kukusanya shilingi trilioni 41.08, sawa na asilimia 67 ya bajeti nzima katika kipindi cha Julai 1, 2026 hadi Juni 30, 2027.

Akiwa katika hafla ya Uwekezaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya TRA, Kizimkazi, Zanzibar, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Omar, ameipongeza TRA kwa kufanikiwa kukusanya shilingi trilioni 3.245 kwa mwezi Julai, 2026.


Naye, Kamishna Mkuu wa TRA, CPA Yusuph Mwenda, amesema wanaendelea kuwahudumia vyema walipakodi na kutatua changamoto zao ili Mamlaka ifanikishe malengo.

"Kutokana na usimamizi wako mzuri Mheshimiwa Waziri wa Fedha na ushirikiano na walipakodi, tunakuhakikishia tutavuka lengo hilo na kupitia, ishara inaonyesha kwamba tumeanza mwaka wa fedha kwa nguvu kubwa na tuna imani tutafikia na kuvuka malengo tuliyowekewa," amesema CPA Mwenda.

MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA SAFARI YA UKUSANYAJI MAPATO WENYE TIJA

Mosi, kufanya malipo kwa njia za kieletroniki. Moja ya mabadiliko ya sheria za kodi ni pamoja na kuhimiza malipo ya kieletroniki ili kuendana na uchumi wa kidijitali unaoachana na matumizi ya fedha taslimu (cashless economy). Ni muhimu kufanya malipo kwa njia za kieletroniki kama simu na benki.

Pili, kudai na kutoa risiti halali ya kieletroniki. Ni muhimu kwa mnunuaji kudai risiti pale anapofanya malipo na muuzaji nae atoe risiti halali ya kieletroniki (EFD), ili serikali ipate kodi yake halali. Mmoja kati ya hawa wawili au wote wawili wasipotimiza wajibu wao, serikali itakosa mapato, na hivyo kushindwa kutimiza kikamilifu malengo ya kuwahudumia wananchi.

Tatu, kuwa waaminifu katika kurekodi taarifa za mauzo. Muuzaji anapaswa kuandika taarifa sahihi za mauzo ili Mamlaka iwe na taarifa sahihi za mwelekeo wa biashara au shughuli za uzalishaji zinazofanyika. Kwa mabadiliko ya sheria za kodi yaliyofanyika, udanganyifu katika uandishi wa taarifa za mauzo, adhabu yake ni mhusika kulipa mara mbili ya kiwango kilichofanyiwa udanganyifu.

Nne, kuboresha uhusiano baina ya walipakodi na TRA. Pamoja na mafanikio katika eneo la uhusiano, bado suala hili linapaswa kuhimizwa kwani walipakodi ndiyo waliobeba hatma ya maendeleo ya nchi yetu. Namna yeyote ya kuwapuuza, ni kuikosesha serikali mapato na kuua shughuli zao za uzalishaji ambazo zinachangia kutoa ajira na kuongeza mapato ya nchi.

Tano, kutoa makadirio ya kodi yanayoendana na kiwango cha biashara. Wakati mwingine, mfanyabiashara anaweza kufunga baishara pale anapokadiriwa kiwango kikubwa zaidi ya uwezo wa biashara yake. Hivyo basi, ukadiriaji kodi unapaswa kumwezesha mfanyabiashara kukua na si kumrudisha nyuma.

Sita, ajenda ya kujitegemea iwe ni ajenda ya kitaifa na si ya viongozi. Mwelekeo wa serikali ni kujitegemea kibajeti. Ajenda hii imefungamanishwa na ulipaji kodi wa hiari na wa kizalendo. Katika safari ya maendeleo ya nchi yetu wananchi na walipakodi kwa ujumla, tuone fahari kulipa kodi kwani kodi hizo ndizo zitakazotujengea heshima ya kujitegemea na kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na ya kimkakati nchini.

Saba, kutoa elimu endelevu ya kodi kwa walipakodi na wananchi. Elimu ya kodi izidi kutolewa ikizingatiwa serikali imefanya mabadiliko makubwa ya sheria za kodi. Elimu ya kodi itolewe kwa wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo. Klabu za kodi ziimarishwe katika taasisi za elimu nchini. Pia, elimu hiyo itolewe sehemu za wazi kama sokoni, vituo vya mabasi ili kujenga uelewa mkubwa kwa wananchi. Pia, TRA iwafuate wafanyabiashara kule walipo kuwapa elimu ya kodi.

Ni faraja kuona mwaka mpya wa fedha umeanza kwa kishindo cha makusanyo yaliyozidi malengo yaliyowekwa. Nchi yetu itaendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo endapo wananchi tutalipa kodi kwa uaminifu. Hakuna mwingine wa kutuletea maendeleo katika nchi yetu - ni sisi wenyewe tunawajibika, hivyo kodi zetu zitaamua maendeleo yetu


Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...