Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MSIGWA: SERIKALI YA SAMIA YAVUNJA REKODI YA MIRADI YA MAENDELEO, UCHUMI WAENDELEA KUPAA

SERIKALI imesema utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umeendelea kuzaa matunda makubwa, huku uchumi wa taifa ukiimarika, mapato ya ndani yakiongezeka na huduma za kijamii zikiboreshwa kwa kiwango kikubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema Serikali imeendelea kutekeleza kwa vitendo ahadi zake kwa kuwekeza trilioni za fedha katika sekta za kimkakati zikiwemo umeme, maji, afya, elimu, kilimo, reli, barabara, bandari na usafiri wa anga.



Msigwa ameema mafanikio hayo yanaonesha wazi kuwa Tanzania inaendelea kujenga uchumi imara unaojitegemea, huku utegemezi wa misaada ya nje ukizidi kupungua kutokana na ongezeko kubwa la ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Ameeleza kuwa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/27 yenye thamani ya Shilingi trilioni 62.33 ni bajeti ya kihistoria itakayokuwa msingi wa kuanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku asilimia 74.2 ya fedha zake zikitokana na mapato ya ndani.

"Kipindi cha miaka michache iliyopita tulikuwa tunategemea misaada kwa kiwango kikubwa, lakini leo Tanzania imefikia hatua ya kujitegemea kwa zaidi ya asilimia 74 ya bajeti yake. Haya ni mafanikio makubwa ya uongozi wa Awamu ya Sita," amesema Msigwa.

Amebainisha kuwa uchumi wa Tanzania umeendelea kukua kwa wastani wa asilimia 5.9 mwaka 2025 na unatarajiwa kufikia asilimia 6.3 mwaka 2026, huku mfumuko wa bei ukiendelea kubaki ndani ya kiwango kinachokubalika cha asilimia 3.4.

Msigwa amesema Serikali imewekeza nguvu kubwa katika sekta ya nishati ambapo uzalishaji wa umeme umeongezeka kwa kasi baada ya kukamilika kwa Mradi wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere (JNHPP), pamoja na miradi mingine ya umeme wa maji, gesi na jua, hatua iliyomaliza tatizo la mgao wa umeme na kuongeza uwezo wa kuhudumia viwanda na wawekezaji.

Katika sekta ya kilimo, amesema Serikali imeongeza bajeti kutoka Shilingi bilioni 294 mwaka 2021/22 hadi Shilingi trilioni 1.19 mwaka 2025/26, huku zaidi ya wakulima milioni 2.8 wakinufaika na ruzuku ya mbolea iliyoongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara pamoja na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Aidha, amesema Serikali imewekeza zaidi ya Shilingi trilioni 3.4 katika miradi ya maji, hatua iliyoongeza upatikanaji wa maji safi vijijini hadi asilimia 85.2 na mijini kufikia asilimia 92.5, huku miradi mikubwa ya maji ikiendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Kwa upande wa miundombinu, Msigwa amesema Serikali imeendelea kuwekeza katika ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), barabara, madaraja, viwanja vya ndege na maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam, hatua zilizoongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo na abiria pamoja na kukuza biashara ya kikanda na kimataifa.

Amesema Bandari ya Dar es Salaam sasa inahudumia shehena nyingi zaidi kuliko ilivyokuwa awali, huku muda wa kuhudumia meli ukipungua kwa kiasi kikubwa kutokana na maboresho yaliyofanyika.

Katika sekta ya anga, Msigwa amesema Serikali imenunua ndege mpya 15 na kuifanya ATCL kuwa na jumla ya ndege 16 zinazotoa huduma ndani na nje ya nchi, huku idadi ya vituo vya safari ikiongezeka kutoka 23 hadi 33.

Akizungumzia mahusiano ya kimataifa, Msigwa amesema ziara ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi imefungua fursa mpya za uwekezaji katika nishati, kilimo, utalii, elimu, usafiri wa anga na biashara, huku safari za moja kwa moja kati ya Dar es Salaam na Moscow zikitarajiwa kuanza Julai 2, 2026.

Amesema Serikali pia imeimarisha ushirikiano wa kiuchumi na Singapore pamoja na Namibia na inajiandaa kumpokea Rais wa Msumbiji Daniel Francisco Chapo ambaye atafanya ziara ya kikazi nchini Julai 2 hadi 3, 2026.

Msigwa amewahimiza Watanzania kuendelea kulipa kodi kwa hiari, akieleza kuwa mafanikio yote ya maendeleo yanatokana na mapato ya ndani pamoja na matumizi sahihi ya mikopo ya maendeleo.

Akizungumzia deni la taifa, amesema Serikali inakopa kwa ajili ya kuwekeza katika miradi yenye tija na si kwa matumizi ya kawaida, huku tathmini zikionesha kuwa deni la Tanzania bado liko ndani ya viwango vinavyokubalika kimataifa.

Ametaka wananchi kupuuza taarifa za upotoshaji kuhusu hali ya uchumi na deni la taifa, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo inayoboresha maisha ya Watanzania na kuifanya Tanzania kuwa taifa lenye uchumi imara na shindani ifikapo mwaka 2050.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...