Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MIKOPO YA TADB INAVYOCHOCHEA MAPINDUZI YA KILIMO NA UKUAJI WA UCHUMI


*Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO*

Sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania. Inatoa ajira kwa mamilioni ya Watanzania, inachangia usalama wa chakula na ni chanzo kikuu cha malighafi kwa viwanda. Hata hivyo, kwa miaka mingi sekta hii ilikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mitaji, hali iliyowafanya wakulima wengi kuendelea na kilimo cha kujikimu badala ya kilimo cha biashara.

Katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita , hali hiyo imeanza kubadilika kufuatia uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Kupitia ongezeko la mtaji na upanuzi wa utoaji wa mikopo, benki hiyo imekuwa nyenzo muhimu ya kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Serikali imeendelea kuiongezea mtaji TADB ili iweze kuwafikia wakulima wengi zaidi kwa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo kuu ni kuongeza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula, kupunguza umaskini na kukuza kilimo cha kisasa kinachozalisha kwa tija.

Mwaka 2021, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipoingia madarakani alifanya mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo kwa kuongeza bajeti za Wizara ya Kilimo pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Hatua hiyo ilienda sambamba na kuiongezea TADB mtaji kutoka shilingi bilioni 60 hadi bilioni 268 kupitia uwekezaji wa Serikali wa shilingi bilioni 208.

Jitihada hizo ziliendelea mwaka 2024 ambapo Serikali, kupitia ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), iliongeza mtaji wa shilingi bilioni 174.16 na kufanya mtaji wa benki kufikia shilingi bilioni 442.16. Mwaka 2025 Serikali iliongeza tena shilingi bilioni 10, hivyo mtaji kufikia shilingi bilioni 452.16.


Ongezeko hilo la mtaji limeongeza uwezo wa TADB kutoa mikopo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi nchini.

Kwa kipindi cha mwaka 2021 hadi 2025, TADB imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi trilioni 1.55. Kati ya kiasi hicho, zaidi ya asilimia 80, sawa na takribani shilingi trilioni 1.24, kimetolewa katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita.

Aidha, idadi ya wanufaika imeongezeka kwa kiwango kikubwa. Kabla ya mwaka 2021, benki ilikuwa imewafikia takribani wakulima milioni 1.6. Hadi sasa, zaidi ya wakulima milioni 2.6 wamepata mikopo ya moja kwa moja, huku zaidi ya wakulima 659,000 wakinufaika kupitia Dirisha la Dhamana la Mikopo ya Wakulima Wadogo.

Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege, anasema dirisha hilo limepanua upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wakulima ambao hapo awali walishindwa kupata mikopo kutokana na ukosefu wa dhamana.

Anasema kupitia utaratibu huo, TADB hutoa dhamana kwa benki na taasisi za fedha ili ziweze kuwakopesha wakulima wadogo kwa masharti nafuu.

 "TADB inaendelea kutoa mikopo katika sekta zote za kilimo. Pia tunaziwezesha benki nyingine kwa kuzipa fedha za muda mrefu na dhamana ili nazo ziweze kuwakopesha wakulima kwa riba nafuu," anasema Nyabundege na kuongeza kuwa kwa sasa, dirisha hilo lina thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 692 na linatekelezwa kupitia benki 19 nchini.

Upatikanaji wa mitaji umeongeza uzalishaji wa mazao na kuimarisha usalama wa chakula nchini. Mwaka 2021 Tanzania ilizalisha tani milioni 17.148 za mazao ya chakula, lakini kufikia mwaka 2025 uzalishaji umeongezeka hadi tani milioni 22.8.

Ongezeko hilo limeifanya Tanzania kufikia kiwango cha utoshelevu wa chakula kwa asilimia 130, hali inayowezesha nchi kujitosheleza kwa chakula na kuuza ziada katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Mbali na usalama wa chakula, mikopo ya TADB imeongeza matumizi ya pembejeo bora, teknolojia za kisasa na mbinu bora za kilimo, hatua ambazo zimeongeza tija na kipato cha wakulima.

Matokeo yake yanaonekana pia katika mazao ya biashara. Kwa mfano, uzalishaji wa korosho umeongezeka kutoka tani 210,000 mwaka 2021 hadi tani 750,000 mwaka 2025. Wakati huo huo, mapato yatokanayo na mauzo ya mazao nje ya nchi yameongezeka kutoka dola za Marekani bilioni 2.1 hadi dola bilioni 5.

Ukuaji huo unaonesha namna upatikanaji wa mitaji unavyochangia kuongeza uzalishaji, kukuza biashara ya mazao na kuongeza mapato ya fedha za kigeni.

Serikali pia ilianzisha kifurushi cha uchochezi cha shilingi trilioni moja kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ili benki za biashara ziweze kuwakopesha wakulima kwa riba nafuu.

Sambamba na hilo, Benki Kuu ilizikopesha benki za biashara kwa riba ya asilimia tatu ili ziweze kutoa mikopo kwa wakulima kwa riba isiyozidi asilimia 10. Kabla ya hatua hiyo, wakulima wengi walikabiliwa na riba kati ya asilimia 20 na 25, kiwango kilichowafanya wengi kushindwa kukopa.

Hatua hizo zimeongeza kwa kiasi kikubwa mikopo inayokwenda kwenye sekta ya kilimo. Mikopo ya sekta hiyo imeongezeka kutoka shilingi trilioni 1.3 kabla ya mwaka 2021 hadi kufikia shilingi trilioni 5.8.

Athari chanya zimeonekana pia katika sekta ya benki ambapo jumla ya mikopo iliyotolewa na benki nchini imeongezeka kutoka shilingi trilioni 18.1 mwaka 2021 hadi trilioni 44.7, huku mali za benki zikifikia shilingi trilioni 77.7.

Ukuaji huo unaonesha jinsi uwekezaji katika sekta ya uzalishaji unavyochochea ukuaji wa sekta nyingine za uchumi, hususan sekta ya fedha.

Katika mwaka wa fedha 2026/27, TADB imejipanga kuongeza upatikanaji wa mitaji kwa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, kuimarisha minyororo ya thamani ya mazao ya kimkakati, kuongeza mauzo ya bidhaa nje ya nchi na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje.

Aidha, benki hiyo inalenga kuendeleza matumizi ya teknolojia za kisasa katika kilimo, kuwawezesha vijana na wanawake kupata huduma za kifedha, kufadhili miradi inayokabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuimarisha ushirikiano na Serikali, sekta binafsi pamoja na washirika wa maendeleo.

Pia itaendelea kuchochea uongezaji thamani wa mazao ya kilimo ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la ndani na kimataifa, sambamba na kuunga mkono ajenda ya uchumi wa viwanda na diplomasia ya uchumi.

Kwa ujumla, uwekezaji wa Serikali katika TADB umeonyesha kuwa upatikanaji wa mitaji ni nguzo muhimu ya mageuzi ya sekta ya kilimo. Kupitia mikopo hiyo, wakulima wameongeza uzalishaji na kipato, usalama wa chakula umeimarika, sekta ya benki imekua na uchumi wa Taifa umeendelea kupata nguvu. Kadri TADB inavyoendelea kupanua huduma zake, kilimo kinazidi kuwa biashara yenye tija, chanzo cha ajira kwa vijana na nguzo imara ya maendeleo endelevu ya Tanzania.













Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...