Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

RAIS SAMIA ATOA WITO KWA BARA LA AFRIKA KUJITEGEMEA ΚΑΤΙΚΑ MASUALA YA AFYA


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa mataifa ya Afrika kuwekeza katika huduma za afya za kibingwa ili kupunguza gharama na utegemezi wa matibabu nje ya Bara hilo.

Rais Dkt. Samia amesema hayo leo tarehe 01 Agosti, 2026, jijini Luanda baada ya kufungua Hospitali ya Rais Julius Nyerere ya Matibabu ya Majeraha ya Moto, akiambatana na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Angola, Mheshimiwa João Manuel Gonçalves Lourenço.





Amesema hospitali hiyo ni ushahidi kuwa ndoto ya Angola ya kubadilisha sekta ya afya kwa kuboresha upatikanaji wa huduma za kisasa za afya ndani ya nchi, inaendelea imetimia.

Aidha, ameipongeza Angola kwa kuimarisha huduma za matibabu ya kibingwa, ikiwemo matibabu ya majeraha makubwa, majeraha ya moto, macho na maeneo mengine yanayohitaji teknolojia na utaalamu wa kiwango cha juu.

Rais Dkt. Samia amesema uwekezaji huo utaongeza uwezo wa Angola kutibu wananchi wake ndani ya nchi na kupunguza gharama za kuwapeleka wagonjwa kupata matibabu nje ya mipaka yake.

Tanzania, amesema Rais Dkt. Samia, imepiga hatua katika matibabu ya huduma za figo, saratani na magonjwa ya moyo, na kwamba Tanzania na Angola zina nafasi kubwa ya kuimarisha ushirikiano katika huduma za kitabibu.

Ameongeza kuwa, ataelekeza wataalamu wa afya kutoka Tanzania kutembelea hospitali hiyo, mahsusi kwa kutibu majeraha yatokanayo na kuungua, kwa ajili ya kujifunza na kubadilishana uzoefu na wenzao wa Angola.

Vilevile, ametaja ushirikiano wa wataalamu, teknolojia na maarifa kuwa ni muhimu katika kujenga uwezo wa Afrika kutoa huduma bora za afya kwa wananchi wake, akieleza kuwa uwekezaji katika huduma za kibingwa ni sehemu ya kujenga uhuru wa kiafya wa Afrika na kupunguza utegemezi wa matibabu nje ya Bara.

"Waasisi wa Mataifa yetu walipigania uhuru wa nchi zetu ili kuzikomboa kutoka kwenye makucha ya wakoloni. Sisi tuliopo tuna jukumu la kuimarisha uhuru wa kiuchumi, maendeleo na haki za watu wa Afrika," amesema Rais Dkt. Samia.

Kwa upande wake, Rais João Manuel Gonçalves Lourenço amesema uwepo wa hospitali hiyo nchini Angola, unaziba pengo la matibabu ya kibingwa, hususan kwa waathirika wa majeraha ya moto ambao uhitaji huduma ya haraka.

Rais Lourenço amesema uamuzi wa kuipa hospitali hiyo jina la Mwalimu Nyerere unatambua mchango wa Kiongozi huyo katika kulijenga Taifa lake, na kusaidia ukombozi wa mataifa mengine Barani Afrika.

"Angola ya leo inaendelea kuthamini nafasi ya Mwalimu Nyerere, ambaye nchi yake iliwapokea wapigania uhuru, wanajeshi na raia wakati wa mapambano ya kusaka uhuru wa nchi yetu," amesema Rais Lourenço.

Halikadhalika, amemshukuru Rais Dkt. Samia, Mama Maria Nyerere na familia ya Mwalimu Nyerere kwa kushiriki ufunguzi huo, akisema uwepo wao umeipa hafla hiyo uzito wa kihistoria.

Amesema kuwa, ingawa Angola imechelewa kutoa heshima hiyo kwa Mwalimu Nyerere, uwepo wa Rais Dkt. Samia na familia ya Baba wa Taifa umeufanya ufunguzi wa hospitali hiyo kuwa wa maana zaidi.

Awali, akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Afya wa Angola, Dkt. Sílvia Lutucuta amesema Hospitali ya Rais Julius Nyerere imejengwa kuongeza uwezo wa Angola kutoa huduma za kibingwa na matibabu kwa wagonjwa wenye hali ngumu zinazohitaji utaalamu, teknolojia na uangalizi maalumu.

Dkt. Lutucuta amesema hospitali hiyo itakuwa kituo cha utafiti, ubunifu, mafunzo na umahiri wa kitaaluma kwa wataalamu wa afya. Ameongeza kuwa, hospitali imeanza kutoa huduma ikiwa na vitengo maalumu vya tiba ya watoto wachanga, watoto wadogo.

Akizungumza kwa niaba ya familia ya Mwalimu Nyerere, Bw. Madaraka Nyerere ameishukuru Serikali ya Angola kwa kuendeleza urithi wa Mwalimu kupitia taasisi itakayotoa huduma na kuokoa maisha ya wananchi.

Amesema ni matumaini ya familia kuona Hospitali ya Rais Julius Nyerere inakuwa kituo cha ubora katika matibabu, mafunzo na utafiti, huku ikiimarisha uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Angola.




Katika siku ya kwanza ya ziara yake, Rais Dkt. Samia alishiriki hafla ya uzinduzi wa kampeni ya "Building Resilience for Women and Girls: Climate, Conflict and Sustainable Futures," kwa lengo la kuwawezesha wanawake na wasichana kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, migogoro na kujenga mustakabali endelevu.

Rais Dkt. Samia alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa Wenza wa Viongozi wa Afrika kuunga mkono juhudi za kuboresha afya na ustawi wa wananchi wa Bara hilo, hususan katika utekelezaji wa majukumu yake ya U-kinara wa Umoja wa Afrika wa Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto.

Kampeni hiyo iliyoandaliwa pembezoni mwa Mkutano wa Umoja wa Wenza wa Viongozi wa Afrika (OASAD) iliwaleta pamoja wenza wa Marais wa nchi za Cabo Verde, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Gabon, Msumbiji, Sierra Leone, Namibia, Nigeria na visiwa vya São Tomé e Príncipe.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...

Majaliwa Achangisha Shilingi Milioni 900 za Ujenzi wa Kanisa Kuu Lindi

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee na kuchangisha sh. milioni 928.67  za ujenzi wa kanisa kuu tarajiwa la Mt. Andrea Kagwa la Jimbo Katoliki la Lindi. Kati ya fedha hizo, sh. milioni 464.3 ni fedha taslimu na nyingine kati ya hizo zimeshawekwa benki na sh. milioni 464.37 bado ni ahadi. Awamu ya kwanza ya ujenzi huo, inatarajiwa kugharimu sh. milioni 700. Akizungumza na waumini na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee iliyofanyika Ruangwa mjini, leo mchana (Jumamosi, Julai 27, 2024), Waziri Mkuu amewataka waliotoa ahadi wazikamilishe mapema ili kazi ya ujenzi isikwame. "Ninawashukuru sana wote mliofika na wote waliochangia ujenzi wa kanisa tarajiwa. Ninawaomba walioahidi, wakamilishe ahadi zao mapema ili kazi ianze kwani ramani ipo, mafundi wapo tayari,  wasimamizi wa ujenzi wapo," amesisitiza.  Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Askofu Wolfgang Pisa kuanza ujenzi wa kanisa kuu la jimbo hilo, ni utekelezaji ...