Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MKUU WA JESHI LA MAGEREZA AFUNGUA MAFUNZO YA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA UREKEBISHAJI KWA MAAFISA USTAWI WA JAMII


 Na. Ssgt Mawazo Mtondo - Dodoma.

Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, leo Juni 10, 2026, amefungua rasmi Mafunzo kwa Maafisa Ustawi wa Jamii kuhusu Mwongozo wa Utekelezaji wa Programu za Urekebishaji katika Ukumbi wa Rugimbana, Msalato, jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, CGP Katungu aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, kwa namna inavyoendelea kuliwezesha Jeshi la Magereza kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Alisema Serikali imekuwa ikitoa rasilimali fedha kwa ajili ya  ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya magereza, makazi ya watumishi, vyombo vya usafiri pamoja na kugharamia mafunzo mbalimbali kwa watumishi wa Jeshi la Magereza.






CGP Katungu alibainisha kuwa moja ya majukumu ya msingi ya Jeshi la Magereza ni urekebishaji wa wafungwa kwa kuwapatia elimu, ujuzi na maarifa ili wanapomaliza vifungo vyao warejee katika jamii wakiwa raia wema na wenye tija. Alieleza kuwa jukumu hilo limeainishwa katika Sheria ya Magereza, Sura ya 58, Kanuni Na. 62 pamoja na Kanuni za Kudumu za Magereza (Prisons Standing Orders, 2003, 4th Edition), Kanuni Na. 404. Aidha, sheria za kimataifa pamoja na mikataba na matamko mbalimbali ya kikanda vimeendelea kusisitiza umuhimu wa urekebishaji wa wafungwa kwa lengo la kuwajengea ujuzi na maarifa yatakayowasaidia baada ya kumaliza vifungo vyao.

Aliongeza kuwa Mheshimiwa Rais amekuwa akielekeza Jeshi la Magereza kuimarisha utekelezaji wa majukumu yake, hususan katika eneo la urekebishaji wa wafungwa ili waweze kurejea katika jamii wakiwa na mchango chanya wa maendeleo. Vilevile, Tume ya Kuboresha Mfumo wa Haki Jinai ilitoa mapendekezo mbalimbali yanayolihusu Jeshi la Magereza, ikiwemo kuboresha programu za urekebishaji wa wafungwa. Sambamba na hilo, Ukaguzi wa Ufanisi (Performance Audit) uliofanywa mwaka 2024 na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (CAG) ulipendekeza kuandaliwa na kutekelezwa kwa Mwongozo wa Utekelezaji wa Programu za Urekebishaji.

Kutokana na maelekezo na mapendekezo hayo, Jeshi la Magereza limeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha utekelezaji wa jukumu la urekebishaji. Miongoni mwa hatua hizo ni kuandaa mitaala mipya ya mafunzo kwa watumishi pamoja na kuimarisha ushirikiano na taasisi mbalimbali za Serikali, ikiwemo Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) katika utoaji wa mafunzo kwa wafungwa na watumishi.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Magereza limeandaa Mwongozo wa Utekelezaji wa Programu za Urekebishaji wa Wafungwa unaobainisha hatua kuu nne za mzunguko wa urekebishaji (Rehabilitation Circle). Hatua hizo ni mapokezi na maelekezo ya awali gerezani (Admission and Orientation), kipindi cha kutumikia kifungo na kupatiwa huduma za urekebishaji (Incarceration Period), maandalizi ya kuachiliwa (Pre-Release) na hatua ya kurejea na kuunganishwa tena katika jamii (Reintegration).

Alisema mwongozo huo utamwezesha kila mfungwa kufanyiwa tathmini ya kina ili kubaini mahitaji yake na kuingizwa katika programu stahiki za urekebishaji. Hadi sasa, makundi yaliyokwisha kupatiwa mafunzo hayo ni Maafisa Mapokezi, Wakuu wa Magereza yote nchini, na sasa wataalamu wa Ustawi wa Jamii, Saikolojia na Sosholojia.

Aidha, CGP Katungu alisema Jeshi la Magereza limeanza kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais kwa vitendo, ambapo utafiti kuhusu urudiaji wa makosa kwa wafungwa waliomaliza vifungo vyao umeanza kufanyika kwa ushirikiano na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo cha Takwimu cha Afrika Mashariki kilichopo Dar es Salaam. Kwa sasa, wataalamu hao wanaendelea na ukusanyaji wa takwimu kwa ajili ya utafiti huo.

Pia, Jeshi la Magereza limeunda timu maalumu ya kuandaa andiko la kuanzisha Mfuko Maalumu wa Kuwasaidia Wafungwa Wanaomaliza Vifungo vyao ili kuwawezesha kujitegemea wanaporejea katika jamii. Vilevile, Jeshi linaendelea kuunda Mfumo wa Kuhifadhi Taarifa za Wafungwa (PIPMIS) kwa kushirikiana na Wakala wa Serikali Mtandao (e-GA), ambapo utekelezaji wake umefikia hatua nzuri.

Akiwasilisha taarifa ya mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Sehemu ya Huduma za Usimamizi wa Wafungwa ya  Jeshi la Magereza, SACP Emmanuel Malisa, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Edith Mbogo, alisema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha Maafisa Ustawi wa Jamii kuelewa na kutekeleza ipasavyo Mwongozo wa Urekebishaji wa Mwaka 2025. Alibainisha kuwa mafunzo hayo ni mwendelezo wa awamu zilizopita na yanakusudia kuimarisha usimamizi wa programu za urekebishaji, kuwajengea washiriki uwezo wa kitaaluma na kuchangia urejeshwaji bora wa wafungwa katika jamii. 




















Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...