Rais Samia Atangaza Kifo Cha David Cleopa Msuya

GEORGE MARATO TV
0


 Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kifo cha aliyewahi kuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu,Cleopa David  Msuya kilichotokea majira ya saa tatu za asubuhi ya leo Jumatano,Mei saba Mwaka 2025 katika Hospitali ya Mzena Jijini Dar-es-salaam.

Akitangaza Msiba huo kwa Taifa,Rais Samia amesema Mzee Msuya ameugua tatizo la moyo kwa kipindi kirefu na kupata matibabu ndani ya nchi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete,Mzena  pamoja na nchini Uingereza.

“Natoa pole kwa familia,ndugu,jamaa na marafiki kwa msiba huu mkubwa kwa Taifa na natangaza siku saba za maombolezo kuanzia Julai saba hadi 13,2025 ambapo Bendera zitapepea nusu mlingoti”amesema Rais Samia

Kwa mujibu wa Rais Samia,Taarifa zaidi kuhusu msiba huo zitaendelea kutolewa na serikali.

Mzee Msuya amefikwa na Umauti akiwa na umri wa miaka 94.Alizaliwa Januari nne,1931 katika kijiji cha Chomvu Usangi,wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top