Leo Jumatano ofisini kwake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete ametembelewa na ugeni wa Watendaji wa Benki ya NMB wakiongozwa na Bi. Vicky Bishubo, Meneja mahusiano Benki na Serikali waliofika kujitambulisha na kutambulisha Wizarani bidhaa mbalimbali zinazotolewa na Benki hiyo.
Katika kikao hicho wamejadiliana kiundani baadhi ya maeneo ambayo Benki hiyo inaweza shirikiana na Serikali katika kufanikisha uwezeshaji Vijana na Jamii.
#KaziInaendelea #UwezeshajiVijana




