Je Unafahamu Kuwa Unaweza Kutumia Pump za Umwagiliaji Zinazotumia Solar Zinazohamishika Kumwagilia Shamba Zaidi ya Moja Kwa Gharama Nafuu?

GEORGE MARATO TV
0

 


Na Emmanuel Chibasa

Katika maeneo ya vijijini mkoani Mara, wakulima wanakumbana na changamoto katika kilimo Cha umwagiliaji kutokana na kukosa elimu ya matumizi ya teknolojia ya kisasa katika kutengeneza mifumo ya nishati ya jua (Solar) unaohamishika Ili kupunguza gharama za uendeshaji wanazotumia Katika pump za mafuta.

Uchunguzi uliofanywa George Marato Tv katika baadhi ya maeneo Musoma umebaini kuwa  wakulima wanatumia pamp za mafuta ambazo wanaweza kumwagilia Kwa kuhamisha lakini hawana uelewa kuwa Kuna teknolojia ya mfumo wa pump za umwagiliaji Zinazotumia solar zinazohamishika na hivyo kuwa ni Suluhu mbadala ya kupunguza gharama wanazotumia Katika pump za mafuta lakini pia kuhifadhi mazao baada ya mavuno Ili yasiharibike.

Wakulima pia hawana uelewa wa kutosha juu ya matumizi ya Teknolojia ya umeme jua inauwezo WA Kuongeza uzalishaji na kupunguza upotevu WA mazao baada ya mavuno na Kuboresha Maisha ya wakulima na Uchumi wa nchi Kwa ujumla na teknolojia hii inaweza Kuleta mabadiriko chanya Katika Taifa 

Tayari baadhi ya taasisi hapa nchini zimeanzisha suluhisho la kipekee kubadilisha kilimo katika maeneo ya vijijini  kwa kutumia pampu za umwagiliaji za nishati ya jua zinazohamishika.

Mhandisi Adrian Edwin Mapunda ni mtaalam wa nishati ya umeme jua kutoka shirika hilo, anasema asilimia 83 ya maeneo yanayolimwa hapa nchini yanalimwa na wakulima wadogo na wamekua wakiwasaidia wakulima katika miradi ya kilimo cha umwagiliaji na wanatekeleza mpango wa kusambaza mifumo ya umwagiliaji ya jua inayohamishika na grid ndogo za umeme zinazohusiana na kilimo katika maeneo ya vijijini.

Mfumo wetu wa kisasa wa pampu za maji za umeme wa jua wenye uwezo wa 0.5 – 2 hp, unaoendeshwa na moduli za PV za 600W – 1,200W zilizowekwa kwenye trolly ya jua, una uwezo wa kupump maji hadi lita 20,000 kwa siku kwa umbali wa hadi 0.8km. Kwa kubadilisha pampu za mafuta ya petroli ambazo ni ghali na zinahitaji matengenezo mengi, mifumo ya umwagiliaji ya jua ya ELICO inatoa mbadala wa kimsingi na wenye ufanisi unaolingana na mahitaji ya wakulima wadogo.

Akielezea juu jinsi teknolojia hiyo inavyoweza kubadilisha kilimo katika maeneo ya vijijini amesema  pampu za umwagiliaji zinazotumia nishati ya jua inayohamishika inatoa suluhisho bora kwa wakulima wa vijijini Kwa kutumia moduli za PV zilizowekwa kwenye troli, wakulima wanaweza kubeba pampu hizi kutoka eneo moja hadi lingine, hivyo kuongeza ufanisi wa umwagiliaji. Tunatumia mifano ya umiliki, upangaji, na matengenezo ili kuhakikisha kwamba teknolojia hii inakuwa rahisi kupatikana na nafuu kwa wakulima.

“Kwa kubadilisha pampu za mafuta ya petroli ambazo ni ghali na zinahitaji matengenezo mengi, mifumo ya umwagiliaji ya jua ya ELICO inatoa mbadala wa kimsingi na wenye ufanisi unaolingana na mahitaji ya wakulima wadogo.

Pia kuwawezesha wakulima wadogo kupata zana wanazohitaji kustawi. Mkakati wa usambazaji unajumuisha mfumo wa PAY-AS-YOU-GO kwa umiliki, umwagiliaji kama huduma, pamoja na mitindo ya upangaji inayowezesha wamiliki kupata mapato huku ikihimiza matumizi ya kijamii.” Amesema Mhandisi Adrian


Teknolojia ya matumizi ya nishati ya umeme jua inayohamishika inonekana  bado haijafahamika kwa wakulima wengi kutokna na kukosa elimu ya namna wnavyoweza kuitumia katika shughuli zao za kilimo na hivyo kuondokana na matumizi ya pampu za mafuta ambazo huzitumia kwa kuhamisha kutoka eneo moja kwenda jingine.

Moja ya mkulima Chacha Mang’era  kutoka Musoma, akizungumza na George Marato Tv katika mahojiano maalum ameonesha  kushangaa aliposikia  kuhusu teknolojia hii katika mfumo matumizi ya umeme wa solar zinavyoweza kuhamishika katika kilimo cha umwagiliaji maji kutoka sehemu moja hadi nyingine .

“Nilikuwa sijasikia kuhusu hili kabla na nilidhani umwagiliaji wakutumia  Solar unahitaji vifaa vya kudumu vilinavyungwa sehemu moja hususasni juu ya bati, na sikujua kuwa kuna njia rahisi ya kubeba vifaa hivyo kutoka shamba moja hadi lingine.” Amesema Chacha

Naye Mwasi  Zebedayo  ambaye pia ni mkazi wa Musoma amesema  ameona pampu za umwagiliaji zinazotumia solar zinazohamishika zina faida nyingi kwa  kufanya kazi katika maeneo tofauti, siyo lazima ziwe sehemu moja  hivyo mkulima  haituhitaji mafuta na wataalamu wanasema  matengenezo machache na hii inamanisha wakulima wanaweza kutumia maji kwa ufanisi zaidi na kupunguza gharama.”

Kwa upande wake Francis Mtayomba  kutoka rusoli musoma vijijini amesema wakulima hasa walio kwenye vikundi wanapaswa kufikishiwa elimu hii kwa wingi ili kuwasaidia kutatua changamoto katika kilimo cha umwagiliaji.

 “Sikujua kwamba tungeweza kutumia pampu hizi kwa kuhamisha na kutumia kwa pamoja, Tukijipanga na kupata uelewa zaidi vikundi vyetu vinaweza kushirikiana kununua na kutumia pampu hizi, hivyo kusaidia kumwagilia mashamba ya wanakikundi wote kwa pamoja na kuongeza uzalishaji” Amesema Francis

Wakulima kutoka musoma na maeneo mengine ya mkoa wa Mara wakitumia nishati ya umeme wa Solar kwa kutengeza mfumo unao hamishika na wakulima wakijengewa  uelewa wakutosha juu ya matumizi teknolojia hii wataweza kufaidika kwa njia bora zaidi na kuboresha uzalishaji wa mazao yao na hivyo kukabiliana na athari za mabadiriko ya tabia nchi pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji wanazotumia katika matumizi ya pump za mafuta pamoja na mazao kuharibika baada ya mavuno

Licha ya serikali ya Tanzania kusisitiza matumizi ya nishati safi Ili Kulinda afya za Watanzania lakini Sekta ya kilimo bado  inaonekana kuachwa nyuma licha ya kuwepo rasilimali jua ambapo  sababu  Kuu ikitajwa kuwa ni uelewa mdogo wa matumizi ya nishati ya umeme jua huku vyombo vya habari na Waandishi wa habari wakidaiwa kuwa na mchango mdogo Katika Kutoa habari na kuelimisha Jamii juu ya faida ya nishati hiyo.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na kituo Cha ubora wa Vyombo Vya habari Africa(ACME) uliofanywa Mwaka 2023 kuhusu uandishi wa habari za nishati ya umeme jua Katika kilimo Katika nchi za Africa mashariki unaonesha kuwa Katika sampuli ya habari 63 waliochukua kwenye Vyombo Vya habari maarufu Katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda unaonesha Kati ya Vyombo hivyo, Vyombo vya habari kutoka Uganda viliandika habari 30, Kenya 23 huku Tanzania Ikiwa na habari 10 na Kati ya habari hizo zilizotolewa kwenye luninga ni 33 huku habari zilizotolewa kwenye magazeti zikiwa 29.

Katika bajeti ya wizara ya kilimo ya Mwaka 2023/2024 serikali imeweka Mkakati wa Kujenga mabwawa 100 nchi nzima Yenye Uwezo wa kuhifadhi Lita Bilioni 900 nchi nzima na Kwa Mkoa wa Mara serikali inatarajia Kujenga Miundombinu ya umwagiliaji Katika bonde la Bugwema na Suguti Katika Halmashauri ya Musoma Vijijini baada ya hatua ya hatua ya upembuzi yakinifu kukamilika.

Wakulima Mkoani Mara wakitumia fursa hii ya Mradi wa kilimo Cha umwagiliaji Kwa Kutumia teknolojia ya umeme jua Katika kilimo Cha umwagiliaji, Uhifadhi wa mazao ya chakula Ili yasiharibike baada ya mavuno pamoja wataweza kukuza Uchumi, kuwa na Usalama wa chakula pamoja na Utunzaji wa Mazingira.

Picha zote na Maelezo ya Mtaalam ni kwa hisani ya Elico Foundation.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top