Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mbunge Mathayo Ashusha Shehena Ya Mbao Utengenezaji Madawati,Viti Na Meza Mashuleni

Na Shomari Binda-Musoma  MBUNGE wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo ameshusha mbao   zaidi ya 35000 kwaajili ya utengenezaji wa madawati,viti na meza kwa shule za msingi na sekondari. Mbao hizo zimeteremshwa leo februari 20/2025 kwenye eneo la utengenezaji shule ya msingi Mukendo na kupokelewa na diwani wa Kata ya Nyakato Joseph Tikina Kisunda.  Akizungumza mara baada ya kupokea mbao hizo diwani huyo amesema mbunge Mathayo amedhamiria kuondoa kero ya madawati,viti na meza kwa shule za msingi na sekondari manispaa ya Musoma. Amesema mbunge ameaxgiza mbao nyingi ambazo zikitengenezwa vifaa hivyo itawafanya wanafunzi kukaa kwa nafasi na kupata elimu bora. Kitina amesema mbunge Mathayo anastahili kupongezwa kwa kuthamini elimu ya mtoto wa jimbo la Musoma mjini. Diwani huyo amesema anaamini baada ya mafundi kupokea watatengeneza na kukamilika kwa wakati. " Tunamshukuru sana mbunge Vedastus Mathayo kwa kuagiza na kuleta mbao kwaajili ya utengenezaji wa madawati,viti ...

Mama Maria Nyerere: CCM idumishe uwezo wa Taifa kujitegemea

Mjane wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Mama Maria Nyerere, ameitaka CCM kuendelea kutimiza wajibu wake wa kuzisimamia serikali zake zote mbili ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na uwezo wa kujitegemea, hasa katika kujilisha. Mama Maria alisema hayo alipokutana na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, aliyefika nyumbani kwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Msasani, jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kumsabahi na kumjulia hali, leo Alhamisi, tarehe 20 Februari 2025. “Naomba tu muendelee kusimamia sera ya msingi ya CCM kuhusu kujitegemea… Uhuru wa taifa unakamilika zaidi pale taifa linapojitegemea, hasa katika kujilisha na kuwa na chakula. CCM isiache wajibu wake wa kuzisimamia serikali zake zote mbili ili nchi yetu iendelee kujitegemea,” alisema Mama Maria.

Jaji Warioba: Napongeza Ccm Kwa Hatua Zake Dhidi Ya Rushwa

Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba, amepongeza hatua zilizoanza kuchukuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mapambano dhidi ya rushwa kwenye uchaguzi. Jaji Warioba ametoa pongezi hizo akirejea mabadiliko ya Katiba ya CCM yaliyofanywa na Mkutano Mkuu Maalum wa CCM, yakiwemo marekebisho ya namna ya kupata wagombea wa udiwani, uwakilishi na ubunge, kwa kuongeza idadi ya wapiga kura wa vikao vya kura za maoni. Amesema kwa kuwa vita dhidi ya rushwa si ya siku moja, CCM haina budi kuhakikisha mapambano ya kumshinda adui huyo yanakuwa endelevu kwa kusimamia misingi ya kuanzishwa kwa chama hicho. Mhe. Warioba, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mstaafu, amesema hayo katika mazungumzo yake na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, leo Alhamisi, tarehe 20 Februari 2025, baada ya Balozi Nchimbi kumtembelea nyumbani kwake, jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kumjulia hali. Aidha, Jaji Warioba, mbali na kukumbusha kuhusu m...

Mbunge Wa Rorya Matatani Kukiuka Taratibu Ccm Kwenye Mafunzo Ya Watendaji Wake

-Ni mafunzo ya watendaji wa ccm ngazi za kata na matawi,mbali na mbunge mwenyekiti pia atuhumiwa Na Shomari Binda;Mara. MAFUNZO ya watendaji wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) Wilaya ya Rorya yamedaiwa kuingiliwa na kuvurugwa na viongozi wa chama hicho akiwemo na mbunge. Viongozi wanaodaiwa kuvuga mafunzo hayo ni mbunge wa jimbo la Rorya Jafari Wambura Chege na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya Ongujo Wakibara wakidaiwa kuiingilia semina ya makatibu wa matawi na kata leo  20/02/2025 na kugawa posho shilingi 50,000 kwa kila katibu. Kwa mujibu wa taarifa zilizosambaa mitandaoni ukiwa ni pamoja na group la Whassap la CCM mkoa wa Mara zimedai utaratibu huo unakiuka maelekezo  kutoka makao makuu ya chama Taarifa hiyo inadai  kuwa mafunzo hayo ya watendaji yasiingiliwe na viongozi au wanasiasa kwa sababu ni mafunzo ya kiutendaji na chama kilisema kitagharamia kila kitu ikiwemo chakula na posho. "Lengo la chama kufanya hivyo ilikuwa ni kuondoa urasimu wa wagombea kutumia nafasi hiyo ...

Mkuu Wa Mkoa Wa Kagera Amwaga Pongezi Jwtz

Mkuu wa Tawi la Utumishi Jeshini Meja Jenerali Marco Elisha Gaguti amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mheshimiwa Fatma Mwasa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera leo tarehe 20 Februari 2025. Amemuhakikishia kuwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania litaendelea kuhakikisha eneo lote la Mkoa wa Kagera linakuwa salama ili kuruhusu wananchi kufanya shughuli za maendeleo kwa uhuru. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mheshimiwa Fatma Mwasa amelishukuru  JWTZ kwa namna linavyohakikisha mpaka wa Tanzania kwa upande wa Mkoa wa Kagera liko salama wakati wote. Amemuhakikishia Meja Jenerali Gaguti kuwa uongozi wa Mkoa utaendelea kutoa ushirikiano kwa JWTZ katika mambo yote ambayo utahusishwa. Meja Jenerali Marco Elisha Gaguti na ujumbe wake yupo Mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi.

Benjamin Mkapa Hospital Kuanza Kutoa Matibabu Ya Ubingwa Wa Juu Kwa Wagonjwa Nchini Burundi

Na Mwandishi wetu , Bujumbura Burundi  Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), Tanzania itaanza kutoa huduma za matibabu ya Ubingwa wa juu kwa wagonjwa nchini Burundi baada ya kukamilisha maandalizi ya kambi ya matibabu inayotegemewa kufanyika hivi karibuni . Hatua hiyo imefikiwa katika ziara ya Wataalamu toka BMH wakiongozwa na Prof Abel Makubi walipokutana na Uongozi wa Hospitali kuu za Prince Regent Charles na Gitega nchini Burundi chini ya uratibu wa Mhe. Gelasius Byakanwa, Balozi wa Tanzania nchini Burundi na Wizara ya Afya ya Burundi. Mashirikiano haya yataruhusu BMH kufanya kambi za matibabu mbalimbali katika Hospitali ya Taifa mjini Bujumbura na pia ile ya Rufaa katika Mkoa wa Gitega na kwa wale wagonjwa ambao hawataweza kutibiwa nchini humo, watapata huduma katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma. Chini ya mpango, BMH pia itasaidia kutoa mafunzo ya ubingwa wa juu kwa watalaamu kutoka Burundi .