Skip to main content

Posts

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

RAIS SAMIA AIPA TADB NGUVU,MTAJI WAPAA HADI BILLIONI 452.16

Jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha sekta ya kilimo zimeendelea kuzaa matunda baada ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuongeza mtaji wake kutoka Shilingi bilioni 60 hadi kufikia Shilingi bilioni 452.16, hatua inayoongeza uwezo wa benki hiyo kufadhili kilimo, mifugo na uvuvi kwa kiwango kikubwa zaidi. Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 30, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari  MAELEZO jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya kilimo Tanzania TADB, Frank Nyabundege, amesema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa wa Serikali pamoja na ushirikiano na taasisi mbalimbali za maendeleo. Amesema kabla ya Serikali ya Awamu ya Sita, mtaji wa TADB ulikuwa Shilingi bilioni 60 pekee, lakini sasa umefikia Shilingi bilioni 452.16, jambo linaloifanya benki hiyo kuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kuwafikia wakulima, wafugaji na wavuvi nchini. "Kabla ya Serikali ya Awamu ya Sita, mtaji wa ...

JAB YAANZA NA BONGO FM MAFUNZO RASMI YA WAANDISHI WA HABARI

 Mwandishi Wetu, Dar es Salaam, Julai 29, 2026 Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza rasmi kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini, yakilenga kuimarisha weledi, maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari wa Bongo FM jijini Dar es Salaam, redio dada ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya JAB, Tido Mhando, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wa kuelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, kwa kuzingatia weledi, maadili na uwajibikaji. “Mafunzo haya ni utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari. Leo tumeanza rasmi na waandishi wa habari wa Bongo FM, tutaendelea kwa vyombo vingine pia kwa sababu, kutakuwa na mafunzo ya muda mfupi na ya muda mrefu. Hivyo, mafunzo haya yawe fursa ya kujenga uwezo na kuweka msingi imara wa kukuza na kulind...

RAIS SAMIA AONGOZA KAMATI KUU YA CCM ZANZIBAR

  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao Cha Kamati Kuu ya Halamshauri Kuu ya CCM Taifa tarehe 29 Julai 2026 Zanzibar

MARY SURATI ACHAGULIWA KUNDI LA KWANZA LA WANAWAKE VIONGOZI AFRIKA

 MBUNGE wa Jimbo la Serengeti, Mhe. Mary Daniel Surati (MB), amepata heshima kubwa baada ya kuchaguliwa kuwa miongoni mwa washiriki 40 wa kundi la kwanza la waanzilishi (Founding Fellows) wa programu ya African Academy for Women in Political Leadership, inayotekelezwa kupitia African School of Governance (ASG). Uteuzi huo umefanyika baada ya mchakato wa ushindani uliowashirikisha waombaji 1,334 kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, jambo linaloonyesha kiwango cha juu cha ushindani na ubora wa washiriki waliochaguliwa kujiunga na programu hiyo ya kimataifa inayolenga kuwaandaa wanawake viongozi wa kizazi kipya barani Afrika. Akizungumzia mafanikio hayo, Mhe. Surati amesema anajivunia kuwa sehemu ya kundi la kwanza la waanzilishi wa programu hiyo, akieleza kuwa ni fursa muhimu ya kujifunza, kukuza uwezo wake wa uongozi na kujenga mtandao wa ushirikiano na wanawake viongozi kutoka nchi mbalimbali za Afrika. Amesema mafunzo hayo yatamwezesha kupata maarifa mapya kuhusu uongozi wa kisias...

DR. JUDITH MHINA RAISES THE TANZANIAN FLAG HIGH IN CHINA

 By Staff Writer A leading Tanzanian businesswoman in the port and maritime transport sector, Dr. Judith Mhina Spendi, continues to represent Tanzania on the international stage following her participation in a major conference on Indian Ocean shipping held in Zhoushan, China. The high-level forum brought together shipping executives, port authorities, investors, and policymakers from across Asia, Africa, and the Middle East to discuss the future of maritime trade in the Indian Ocean region. Dr. Judith’s invitation to the conference underscores the recognition Tanzania is receiving as a key player in East Africa’s blue economy. Dr. Judith is among the few Tanzanian women who have successfully established a strong presence in the maritime shipping sector through PMM Group. The company has built a solid reputation in cargo shipping across the Indian Ocean, inland container depot management, and operations linked to the mining and environmental sectors. Over the years, PMM Group has p...

SEKTA BINAFSI YATAJWA NGUZO MUHIMU KUFANIKISHA DIRA YA TAIFA 2050

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amesema sekta binafsi ina nafasi ya kipekee katika kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku akiwataka viongozi na watumishi wa umma kubadili mtazamo na kuiona kama mshirika muhimu wa maendeleo badala ya mpinzani. Akifunga kikao cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Mkoa wa Dodoma kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Senyamule alisema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejikita katika kujenga uchumi unaomilikiwa na Watanzania kupitia uwekezaji wa ndani na ushirikiano imara kati ya sekta ya umma na sekta binafsi. "Katika kutekeleza Dira ya Taifa 2050, tutaendelea kupokea wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi. Wawekezaji kutoka nje watakuja na mtaji na teknolojia, huku Watanzania wakinufaika kupitia ajira, mapato ya kodi na ukuaji wa uchumi. Hivyo, ni muhimu tubadili mtazamo wetu na kuitambua sekta binafsi kama mshirika wetu wa maendeleo," amesema...