Leo, tarehe 07 Juni 2026, Kamati Maalum ya CHADEMA Zanzibar imeketi katika kikao chake kilichofanyika Kisiwani Pemba. Kikao hicho kimeongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Mhe. Said Mzee Said, na kuhudhuriwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Mhe. John Heche, pamoja na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Mhe. John Mnyika.
Kikao hicho kinajikita katika kujadili hali ya siasa ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla, kwa lengo la kufanya tathmini ya mwenendo wa kisiasa na kuweka mwelekeo wa hatua za chama katika kipindi kijacho.
Aidha, kikao hicho kinajadili na kupitisha Mpango Mkakati wa CHADEMA Zanzibar wa miaka mitano, utakaokuwa mwongozo wa utekelezaji wa shughuli, sera na vipaumbele vya chama kwa kipindi husika.





Comments
Post a Comment