Rais Dkt Samia amfuta machozi Galacha Hassan Bitchuka

GEORGE MARATO TV
0


📍Amtumia shilingi milioni 10

Na Mashaka Mhando

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemjulia hali na kumpatia mkono wa pole nguli wa muziki wa dansi nchini, Mzee Hassan Rehani Bichuka, ambaye kwa sasa anauguza maradhi nyumbani kwake Sinza Mori, jijini Dar es Salaam.

Salamu hizo za faraja zimefikishwa jana, Machi 9, 2026, na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), aliyefika nyumbani kwa mwanamuziki huyo kwa niaba ya Rais.

Akikabidhi kiasi cha Shilingi Milioni 10 taslimu kutoka kwa Mheshimiwa Rais, Mhe. Mwinjuma alisema kuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anathamini mchango usiopimika ambao Mzee Bichuka ametoa katika kuijenga sanaa ya Tanzania kupitia sauti yake na tungo zilizolimika taifa kwa miongo mingi.

"Mheshimiwa Rais Samia amenituma nifike hapa kukupelekea salamu zake za pole na upendo. Anakuombea upate nafuu ya haraka na ameelekeza nikukabidhi kiasi hiki cha Shilingi Milioni 10 kwa ajili ya kusaidia taratibu zako za matibabu na kukutia moyo katika kipindi hiki," alisema Mhe. Mwinjuma.

Mzee Hassan Rehani Bichuka, ambaye ni mmoja wa waimbaji mahiri kuwahi kutokea nchini kupitia bendi maarufu kama DDC Mlimani Park Orchestra 'Sikinde Ngoma ya Ukae', Msondo Ngoma na OSS, alipokea msaada huo kwa hisia kali, akimshukuru Rais Samia kwa moyo wake wa kipekee wa kuwakumbuka wasanii wakongwe.

Tukio hili limekuja huku serikali ikionyesha nia ya dhati ya kuimarisha mifumo ya ustawi wa wasanii, hususan wale waliolitumikia taifa kwa uaminifu tangu enzi za kuanzishwa kwa muziki wa dansi nchini Tanzania.

Wadau wa sanaa wamepongeza hatua hiyo ya Rais, wakibainisha kuwa kuwajali magwiji kama Bichuka na Zorro kinaendana na kauli mbiu ya Kazi na Utu lakini pia kinarejesha heshima ya taaluma ya sanaa nchini.








Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top