Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MAKONDA: UWEKEZAJI WA AFYA WAIFANYA DIRA YA TAIFA 2050 KUWA HALISI


Na Mwandishi Wetu, Arusha

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Arusha, Paul Christian Makonda, ameridhishwa na maboresho yanayoendelea katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center inayotoa huduma kwa ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, ALMC–JKCI Arusha.

Maboresho hayo yanafanyika kwa uwezeshaji wa Global Medicare, kwa lengo la kuongeza ubora wa huduma za afya, kuboresha mazingira ya matibabu, kuimarisha utalii tiba na kuiandaa hospitali kutoa huduma zinazokidhi viwango vya kimataifa kuelekea mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2027.

“Lengo kubwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kabisa na katika mazingira mazuri. Vilevile tunataka kuimarisha utalii tiba na kutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya AFCON 2027,” alisema Mhe. Makonda.


 Makonda alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya afya na kuruhusu taasisi za kibingwa kama JKCI kupanua huduma zake hadi mikoani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa JKCI ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dkt. Peter Kisenge, alisema maboresho yanayoendelea yanalenga kuibadilisha ALMC–JKCI kuwa kituo cha kisasa cha huduma za kibingwa chenye mazingira rafiki kwa wagonjwa.

Dkt. Kisenge alisema lengo ni kuhakikisha mgonjwa anapofika hospitalini anakutana na mazingira yenye usafi, utulivu, faraja na huduma zinazofanana na zinazopatikana katika hospitali kubwa za kimataifa.

“Tunataka mgonjwa anapokuja hapa asiingie katika mazingira yanayomwongezea hofu. Tunataka akute hospitali yenye mazingira mazuri, tulivu na yenye huduma zinazompa faraja,” alisema Dkt. Kisenge.

Kwa mujibu wake, skrini moja itaonyesha taarifa za wagonjwa waliopo wodini, ikiwemo mapigo ya moyo, kiwango cha oksijeni kwenye damu, shinikizo la damu na viashiria vingine muhimu vya afya.

Skrini nyingine itaunganishwa na mfumo wa Dozee, teknolojia inayowezesha mgonjwa kuendelea kufuatiliwa hata baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.

Alisema mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji, upasuaji wa kujifungua au matibabu mengine yanayohitaji uangalizi wa siku kadhaa ataweza kufuatiliwa akiwa nyumbani, huku wauguzi na madaktari wakipokea taarifa za afya yake kwa wakati.

Dkt. Kisenge alisema mfumo huo utasaidia kugundua mapema mabadiliko ya hali ya mgonjwa na kuwawezesha wataalamu wa afya kuchukua hatua kabla hali haijawa mbaya.

Alisema vyumba vya wagonjwa vitawekewa vifaa vya kisasa vya ufuatiliaji, televisheni na mifumo ya kidijitali ya kuhifadhi historia ya mgonjwa, uchunguzi, dawa na matibabu yote anayopatiwa.

Dkt. Kisenge alisema hospitali pia inaandaa wodi maalumu ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu baada ya kutoka katika chumba cha wagonjwa mahututi, inayojulikana kama High Dependency Unit.

Dkt. Kisenge alisema mashine ya Cath Lab yenye thamani ya takribani shilingi bilioni tatu inatarajiwa kuwekwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya matatizo ya mishipa ya moyo.

Mkurugenzi wa Huduma za Kliniki wa ALMC–JKCI Arusha, ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dkt. Sakeh Hamisi Mwishete, alisema uongozi wa hospitali umeweka mkakati wa kuhakikisha wagonjwa wenye mahitaji tofauti wanapata huduma zinazowafaa.

Dkt. Mwishete alieleza kuwa vyumba vya VIP vimewekewa vifaa vinavyowezesha kubadilishwa haraka kuwa vyumba vya uangalizi maalumu au ICU endapo hali ya mgonjwa itabadilika.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mji

“Hiki ni chumba cha VIP, lakini kimewekewa vifaa maalumu. Endapo hali ya mgonjwa itabadilika, kinaweza kupandishwa hadhi na kutoa huduma za dharura au huduma zinazohitajika katika ICU bila kuchelewa,” alisema Dkt. Mwishete.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura katika ALMC–JKCI Arusha, Dkt. Farida Abdallah, alisema kitengo cha dharura kinaendelea kupokea wagonjwa kutoka Arusha, Manyara, Singida na maeneo mengine ya Kanda ya Kaskazini.

“Lengo letu kubwa ni kuhakikisha mgonjwa wa dharura anapata huduma kwa wakati ili kuzuia madhara ya kudumu au kupoteza maisha. Mimi pamoja na timu yangu tunafanya kazi saa 24 kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma za haraka,” alisema Dkt. Farida.


Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...