Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAZIRI MAVUNDE AELEKEZA USIMAMIZI THABITI WA SHERIA ILI ASILIMIA 90 YA BIDHAA NA HUDUMA MIGODINI KUFANYWA NA WATANZANIA


 ▪️Ampongeza Rais Samia kwa kuwa kinara wa ushirikishwaji wa Watanzania migodini

▪️Awataka Watanzania kuunganisha nguvu na kutoa huduma bora

▪️Atoa angalizo kwa wawekezaji kutii sheria za nchi

▪️Ununuzi wa bidhaa na huduma sasa wafikia Shilingi Trilioni 5.1 kwa mwaka

MWANZA

Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony P. Mavunde, ameelekeza usimamizi madhubuti wa Sheria ya Madini na kanuni zake ili kuhakikisha asilimia 90 ya bidhaa na huduma zinazotumika katika migodi nchini zinatolewa na Watanzania, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wa wananchi na kukuza uchumi wa nchi.

Waziri Mavunde ametoa maelekezo hayo mapema leo Julai 22, 2026, wakati akizindua Jukwaa la Tano la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini, lililofanyika Mwanza na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta hiyo, wakiwemo kampuni za uchimbaji wa madini, watoa huduma migodini, wafanyabiashara wa madini, wawekezaji, taasisi za umma na binafsi pamoja na vyama vya wachimbaji wa madini nchini.




Amesema utekelezaji madhubuti wa Sheria ya Madini na kanuni zake utasaidia kuongeza ushiriki wa Watanzania katika uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma migodini, sambamba na kuhakikisha fursa zinazotokana na ukuaji wa Sekta ya Madini zinawanufaisha wananchi na biashara za ndani.

“Serikali inatarajia kuona asilimia 90 ya bidhaa na huduma zinazotumika katika migodi zikizalishwa na kutolewa na Watanzania. Hili linahitaji usimamizi madhubuti wa sheria, pamoja na Watanzania kujiandaa kutumia fursa zinazopatikana katika Sekta ya Madini,” amesema.

Waziri Mavunde amewataka watoa huduma katika migodi nchini kuunganisha nguvu na kufanya kazi kwa pamoja ili kuchangamkia fursa zinazoongezeka katika sekta hiyo, hususan katika uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma bora zinazokidhi viwango vinavyohitajika.

Amesema ongezeko la uwekezaji katika Sekta ya Madini na matarajio ya kuanzishwa kwa migodi mipya linatarajiwa kufungua fursa zaidi kwa Watanzania, hivyo watoa huduma wanapaswa kujiandaa kwa kuwekeza katika uzalishaji wa ndani, kuongeza ubora wa bidhaa na huduma na kujenga uwezo wa kushindana katika soko.

“Watoa huduma wanapaswa kuungana na kufanya kazi kwa pamoja ili kutoa huduma zenye ubora wa hali ya juu na kuchangamkia fursa zinazopatikana katika Sekta ya Madini. Hii itawasaidia kukua kibiashara na pia kuchangia katika kukuza uchumi wa nchi,” amesema Waziri Mavunde.

Wakati huo huo, Waziri Mavunde ametoa angalizo kwa wawekezaji katika Sekta ya Madini kuhakikisha wanazingatia na kutii sheria na kanuni za nchi zinazosimamia sekta hiyo.

“Serikali imeboresha mazingira ya uwekezaji kwa kuweka sheria na kanuni ambazo mnapaswa kuzifuata ili uwekezaji wenu uwe na tija nchini,” amesisitiza.

Akielezea mafanikio yaliyopatikana tangu kufanyika kwa maboresho ya Sheria ya Madini na kanuni zake, Waziri Mavunde amesema Serikali imeendelea kushuhudia ongezeko la ushiriki wa Watanzania katika utoaji wa huduma na usambazaji wa bidhaa kwenye migodi.

Amesema ununuzi wa bidhaa na huduma katika Sekta ya Madini umefikia Shilingi trilioni 5.1 kwa mwaka, hali inayoonesha ukubwa wa fursa zilizopo kwa wazalishaji na watoa huduma wa ndani.

Aidha, amesema Sekta ya Madini imezalisha ajira rasmi 20,421, ambapo ajira 16,695 zinashikiliwa na Watanzania.

“Mpaka sasa tumeshuhudia watendaji wakuu na mameneja wa migodi wakiwa Watanzania. Haya ni mafanikio makubwa tofauti na zamani, ambapo nafasi nyingi za uongozi katika migodi ya madini zilishikiliwa na raia wa kigeni,” amesisitiza.

Waziri Mavunde amesema mafanikio mengine ni kuanzishwa kwa masoko ya madini 44 na vituo vya ununuzi wa madini 117, hatua ambayo imechangia kuongeza ukusanyaji wa maduhuli yatokanayo na Sekta ya Madini kutoka Shilingi bilioni 161 katika mwaka wa fedha 2015/2016 hadi Shilingi trilioni 1.393 katika mwaka wa fedha 2025/2026.

Aidha, amesema utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuanzisha hifadhi ya dhahabu katika Benki Kuu ya Tanzania, ulioanza rasmi Oktoba 1, 2024, umeiwezesha Tanzania kuwa na hifadhi ya dhahabu yenye uzito wa tani 28 na kuiweka nchi miongoni mwa mataifa matano barani Afrika yenye hifadhi kubwa ya dhahabu.

Amesema mchango wa Sekta ya Madini katika Pato la Taifa umeendelea kuongezeka na kufikia asilimia 10.1, hatua inayoonesha umuhimu wa sekta hiyo katika kukuza uchumi wa nchi.

Waziri Mavunde amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuipa kipaumbele Sekta ya Madini na kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na ushiriki wa Watanzania katika sekta hiyo.

Pia amewapongeza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa usimamizi madhubuti wa Sekta ya Madini, pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Madini na Tume ya Madini kwa uchapakazi na ubunifu unaochangia kuiwezesha sekta hiyo kuendelea kufanya vizuri.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, amesema Serikali imeendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji katika Sekta ya Madini ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Amewataka watoa huduma katika migodi kutoa huduma bora kwa kuzingatia weledi, uadilifu na viwango vinavyokubalika, akisisitiza kuwa Wizara itaendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali na kufanya kazi kwa karibu zaidi na wadau wa Sekta ya Madini.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Amir Mkalipa, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, ameipongeza Wizara ya Madini kwa juhudi zake za kuendelea kuvutia uwekezaji katika Mkoa wa Mwanza.

Amesema uwekezaji huo umechangia kuanzishwa kwa Mgodi wa Dhahabu wa Sotta Mining, ambao unatarajiwa kutoa ajira 1,500 utakapoanza uzalishaji.

Naye Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet R. Lekashingo, amesema Jukwaa la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini limekuwa na manufaa makubwa katika kuchochea ushiriki wa Watanzania katika sekta hiyo.

Amesema mafanikio hayo yanaonekana kupitia ongezeko la uwasilishaji wa mipango ya ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini, kutoka mipango 51 mwaka 2018 hadi kufikia mipango 1,312 mwaka 2025.






Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...