Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

RAIS SAMIA: VIJANA JIFUNZENI UJUZI UNAOENDANA NA MAHITAJI YA DUNIA YA KISASA


 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka wanafunzi wa elimu ya juu kujiandaa kwa dunia inayohitaji ujuzi zaidi ya vyeti, akisisitiza umuhimu wa maarifa, nidhamu, uzalendo, utu, udadisi na uwezo wa kushirikiana nje ya mipaka ya tamaduni, taaluma na mataifa.

Rais Dkt. Samia ameyasema hayo leo jijini Moscow baada ya kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima ya Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN University), kwa kutambua mchango wake katika maendeleo ya elimu, ushirikiano wa kimataifa na urafiki kati ya mataifa.





Halikadhalika, Rais Dkt. Samia ameitambua heshima hiyo kama utambuzi wa nafasi ya elimu katika maendeleo ya jamii na uchumi, pamoja na uhusiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi uliosaidia kujenga kizazi cha wataalamu waliochangia maendeleo ya mataifa hayo mawili.

"Katika dunia inayobadilika kwa kasi, jukumu letu ni kuwaandaa vijana wenye maarifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza katika uchumi wa maarifa," amesema Rais Samia.

Aidha, ameeleza kuwa Tanzania imeweka elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu katika kiini cha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku programu ya ufadhili wa masomo ya Samia Scholarship ikiendelea kupanua fursa za elimu kwa Watanzania vijana wenye uwezo na vipaji katika fani za kimkakati.

Mpango huo, ulioanzishwa mwaka 2023, tayari umenufaisha zaidi ya wanafunzi 5,000 na sasa unaelekezwa katika maeneo ya sayansi ya data, akili unde, tiba, uhandisi, mafuta na gesi, pamoja na teknolojia za mazingira.

Kwa upande wake, Rais wa Chuo, Prof. Vladimir Mikhaylovich Filippov, amesema Shahada ya Heshima aliyotunukiwa Rais Dkt. Samia hutolewa kwa nadra kwa viongozi wanaotoa mchango mkubwa katika kuimarisha amani, urafiki na ushirikiano kati ya mataifa.

"Uamuzi wa Baraza la Chuo ni utambuzi wa mchango mkubwa wa Mheshimiwa Rais katika kuimarisha mahusiano ya Tanzania na Urusi na kuendeleza urafiki kati ya wananchi wa mataifa yetu," amesema Prof. Filippov.

Ameongeza kuwa, Tanzania ni mmoja wa washirika wakuu wa RUDN barani Afrika, na kwamba uamuzi wa kumtunuku Rais Samia Suluhu Hassan Shahada ya Heshima ulipitishwa kwa azimio moja na Baraza la Chuo kupitia kura ya siri iliyofanyika tarehe 16 Machi, 2026.

Naye, Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Oleg Yastrebov, alisema Tanzania ina nafasi ya pekee katika historia na ushirikiano wa chuo hicho barani Afrika.

"Ushirikiano kati ya RUDN na vyuo vikuu vya Tanzania unaingia katika hatua mpya yenye fursa kubwa zaidi za elimu, utafiti na ubunifu," amesema Prof. Yastrebov.



Aidha, amesema Watanzania wamekuwa wakisoma RUDN tangu kuanzishwa kwa chuo hicho mwaka 1960 na kwamba ushirikiano wa sasa baina ya Tanzania na chuo hicho unaendelea kupanuka kupitia ushirikiano katika tafiti za pamoja na programu za maendeleo ya rasilimali watu.

Kando ya hafla hiyo, Tanzania na Urusi zilisaini mikataba mitatu ya ushirikiano katika elimu ya juu, na programu mbili za pamoja za shahada kati ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na Chuo Kikuu cha RUDN katika Sayansi ya Takwimu, Mifumo ya Anga, Akili Unde na "Machine Learning."

Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN University) kilianzishwa mwaka 1960. Chuo kina zaidi ya wanafunzi 46,000 kutoka nchi zaidi ya 160, na programu zaidi ya 800.

Tanzania na RUDN zina ushirikiano wa zaidi ya miaka 65. Hadi sasa, Watanzania 1,132 wamehitimu RUDN, idadi inayoiweka Tanzania katika nafasi ya pili barani Afrika kwa wingi wa wahitimu wa chuo hicho, ikitanguliwa na nchi ya Nigeria. Kwa sasa Watanzania 72 kati ya 200 wanaoendelea na masomo nchini Urusi, wanasoma Chuo Kikuu cha RUDN.

Viongozi wengine wa Afrika waliowahi kutunukiwa Shahada za Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Peoples' Friendship University of Russia (RUDN) ni pamoja na Hayati Sam Nujoma, Rais wa Jamhuri ya Namibia, aliyetunukiwa mwaka 1998.

Mheshimiwa José Eduardo dos Santos, Rais wa Jamhuri ya Angola, aliyetunukiwa mwaka 1998; Mheshimiwa Thabo Mvuyelwa Mbeki, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, aliyetunukiwa mwaka 1998.

Mheshimiwa Olusegun Obasanjo, Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Nigeria, aliyetunukiwa mwaka 2001; Mheshimiwa Alpha Condé, Rais wa Jamhuri ya Guinea, aliyetunukiwa mwaka 2016; na Mheshimiwa Hery Rajaonarimampianina, Rais wa Jamhuri ya Madagascar, aliyetunukiwa mwaka 2018.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...