Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu Atatua Mgogoro wa Ardhi Uliodumu Kwa Miaka 51 Wilayani Rombo


Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ametatua mgogoro wa ardhi kati ya Parokia ya Mtimhoo ya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi na Mzee Peter Morisi wa Kijiji cha Msaranga, Wilaya ya Rombo Mkoa wa Kilimanjaro, uliodumu kwa kipindi cha miaka 51.

Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokea malalamiko ya Mzee Peter Morisi alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Rombo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Kilimanjaro tarehe 17 Februari 2026 ambapo aliahidi kuwa Serikali ingetuma wataalamu wilayani humo kwa ajili ya kuchunguza na kutatua mgogoro huo.

Kufuatia maelekezo hayo, Waziri Mkuu alituma timu ya wataalamu kutoka Ofisi yake ambao walifika mkoani Kilimanjaro na kushirikiana na viongozi wa Mkoa pamoja na viongozi wa Kijiji cha Msaranga kutembelea eneo la mgogoro. Aidha, timu hiyo ilifanya vikao na familia iliyokuwa katika mgogoro, viongozi wa kijiji, viongozi wa Parokia ya Mtimhoo pamoja na viongozi wa Jimbo Katoliki la Moshi ambapo pande zote zilikubaliana kuwa maridhiano ndiyo njia sahihi ya kumaliza mgogoro huo.

Katika madai yake, Mzee Peter Morisi alieleza kuwa eneo lake lilichukuliwa kwa nguvu na Kanisa Katoliki na kwamba fidia aliyolipwa ilikuwa ndogo ikilinganishwa na ukubwa wa eneo lililotwaliwa. Kutokana na kutopata suluhisho kwa muda mrefu, aliamua kuwasilisha malalamiko yake kwa Waziri Mkuu wakati wa mkutano wa hadhara.

Timu ya wataalamu ilipitia nyaraka zote zilizowasilishwa na pande husika na kubaini kuwa Mzee Peter Morisi alipokea fidia ya shilingi 3,935.50 tarehe 16 Aprili 1980. Aidha, alipewa eneo jingine katika Kitongoji cha Kirachi, Kijiji cha Msaranga ili kupisha ujenzi wa shule na kanisa katika eneo lake la awali.


Katika hatua nyingine, timu hiyo ilikutana na Askofu wa Jimbo Katoliki la Moshi, Askofu Ludovick Minde ambaye alisisitiza kuwa Kanisa Katoliki lina utamaduni wa kutatua migogoro kwa njia ya maridhiano na kuwataka wahusika kuendelea na mazungumzo ya amani.

Askofu Minde alitoa shilingi milioni tano kama kifuta machozi kwa madhara ambayo Mzee Peter Morisi na familia yake wameyapitia katika kipindi chote cha kutafuta suluhisho la mgogoro huo. Aidha, alisema Kanisa halina kinyongo na mlalamikaji na litaendelea kushirikiana naye wakati wote.

Vilevile, Askofu Minde alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutuma timu ya wataalamu kutoka Ofisini kwake na kumtakia heri katika utekelezaji wa majukumu yake ya uongozi.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Waziri Mkuu naye alitoa shilingi milioni tano na kufanya jumla ya fedha zilizotolewa kwa Mzee Peter Morisi kuwa shilingi milioni kumi kwa lengo la kujenga maridhiano na kuimarisha mshikamano katika jamii.

Baada ya kufikiwa kwa maridhiano hayo, pande zote zilitia saini nyaraka za makubaliano zikikiri kuwa mgogoro huo umemalizika kwa njia ya maridhiano na kuahidi kusameheana pamoja na kuendelea kuishi kwa amani. Kila upande pia ulikabidhiwa Hati za Hatimiliki za Kimila kwa maeneo husika.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa hati hizo na kusaini nyaraka za maridhiano, Mzee Peter Morisi aliishukuru Serikali kwa kumaliza mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu na kuahidi kushirikiana na Kanisa pamoja na wanakijiji wenzake bila kinyongo.

Naye Diwani wa Kata ya Kisale Msaranga, Mhandisi Mathias Assenga alisema mgogoro huo uliathiri mshikamano wa wananchi pamoja na uhuru wa kuabudu kwa kuwa ulihusisha eneo la kanisa linalotumiwa na waumini kwa ibada na shughuli nyingine za kidini.

Kwa upande wake, Padri Amadeus Mtui ambaye ni Wakili wa Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Moshi alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutuma timu ya wataalamu ambayo imekuwa chachu ya kumalizika kwa mgogoro huo.

Baadhi ya viongozi walioshiriki katika mchakato wa maridhiano hayo ni pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Charles Daudi Mganga, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Kilimanjaro, Rehema Mdee pamoja na Diwani wa Kata ya Kisale Msaranga, Mhandisi Mathias Assenga.

Mzee wa Kijiji cha Msaranga, Andrea Peter Mkenda alisema kumalizika kwa mgogoro huo kutaleta amani, utulivu na kuimarisha mshikamano miongoni mwa wananchi hali itakayowapa nafasi nzuri ya kuendelea na shughuli zao za maendeleo.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...