Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

DC Rorya aeleza hatua za kutatua changamoto za Kwibuse

RORYA. 

Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mkoani Mara, Dk. Khalfan Haule, amesema serikali itachukua hatua za haraka za muda mfupi na muda mrefu kukabiliana na changamoto za Barabara, maji, afya na nishati ya umeme zinazoikabili kijiji cha Kwibuse iliyoko Kata ya Kisumwa wilayani humo

Dk. Haule ameyasema hayo baada ya kukagua uharibifu wa barabara ya Kuruya–Kwibuse–Marasibora, ambapo amesema kuwa sehemu ya barabara hiyo imekatika katika maeneo yenye makalavati matano mapya yaliyojengwa, hali iliyosababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi na wasafiri.

Amesema hatua za muda mfupi zitahusisha kujaza mawe na vifusi katika maeneo yote yaliyoathirika ili magari na wananchi waweze kuendelea kutumia barabara hiyo, huku serikali ikiandaa mpango wa matengenezo makubwa zaidi ya kudumu.

“Mpango wa muda mrefu ni kunyanyua tuta la barabara hasa kwenye bonde la karibu na eneo la Kukona ili kuondoa kabisa tatizo hili,” alisema Dk. Haule alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kwibuse katika mkutano wa hadhara.

Katika sekta ya maji, Mkuu huyo wa Wilaya alisema mradi wa maji kutoka Komuge pamoja na visima viwili vilivyochimbwa umekuwa ukikabiliwa na changamoto ya uharibifu wa mabomba unaofanywa na baadhi ya wananchi, hali inayosababisha maji kupotea kabla hayajawafikia wananchi.

Amesema serikali kwa kushirikiana na viongozi wa kijiji imekubaliana kuimarisha ulinzi wa bomba hilo huku Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ukitarajiwa kufanya ukarabati wa maeneo yote yaliyoharibiwa ili huduma ya maji irejee katika hali ya kawaida.

Aidha, amebainisha kuwa serikali itanunua pump mpya ya kusukuma maji mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu ili kuwezesha kisima kilichochimbwa kufanya kazi kikamilifu hasa wakati wa kiangazi.

Kuhusu kisima cha Kukona, Dk. Haule ameliagiza Jeshi la Polisi kuwatafuta viongozi wa kitongoji wanaodaiwa kuhusika na wizi wa pump ya maji ili irejeshwe na huduma kuendelea.

Akizungumzia sekta ya afya, Dk. Haule ameeleza kuwa zahanati ya kijiji ina wahudumu watatu wa afya, lakini kwa sasa mmoja yupo masomoni, hivyo huduma zinaendelea kutolewa na wahudumu wawili waliobaki.

Amesema changamoto nyingine ni wahudumu hao kuishi katika kijiji jirani cha Nyanchabakenye, hali inayochelewesha wakati mwingine utoaji wa huduma kwa wananchi.

 Kutokana na hali hiyo, serikali imemwagiza mwenyekiti wa kijiji cha Kwibuse kuwatafutia wahudumu hao nyumba ya kupanga karibu na zahanati ili wawe karibu zaidi na eneo lao la kazi.

Pia amekitaka kijiji hicho kuendelea na ujenzi wa nyumba ya mganga ili ikikamilika iwe suluhisho la kudumu kwa makazi ya wahudumu wa afya. Aidha, ameahidi kuwa serikali itaipa kipaumbele zahanati ya Kwibuse mara itakapopata watumishi wapya wa afya ili kupunguza uhaba wa watumishi uliopo sasa.

Kwa mujibu wa Dk. Haule, licha ya changamoto zilizopo, zahanati hiyo inaendelea kutoa huduma huku ukarabati ukiendelea baada ya sehemu ya paa kuharibiwa na upepo ambapo Serikali tayari imetoa Sh milioni 3.7 kwa ajili ya kugharamia matengenezo hayo.

Kuhusu sekta ya elimu, Dk. Haule amesema wakati wa mkutano na wananchi hakuelezwa kuhusu uchakavu wa madarasa na uhaba wa madawati katika Shule ya Msingi Kwibuse, lakini ameahidi kufika binafsi kukagua hali hiyo wakati atakapokwenda tena eneo hilo kukagua maendeleo ya matengenezo ya barabara.

“Sijafika na wananchi hawakusema. Nikirudi kukagua matengenezo ya barabara nitapitia kuyaona,” alisema.

Aidha, alisema wananchi walimweleza kuhusu kubomoka kwa madarasa yaliyokuwa yakijengwa kwa nguvu na michango yao wenyewe, jambo lililomsukuma kuagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo cha tatizo hilo na kuchukua hatua stahiki.

Kwa upande wa nishati ya umeme, alisema kati ya vitongoji sita vya kijiji hicho, vitatu tayari vina huduma ya umeme huku vitongoji viwili, ikiwemo Bosi, vikitarajiwa kupata huduma hiyo mwaka huu. Kitongoji kimoja kilichobaki kitapata huduma hiyo katika awamu inayofuata.

Dk. Haule alisisitiza kuwa serikali itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha changamoto zote zinazogusa maisha yao zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...