CRJE yakabidhi majengo mawili ya hosteli za wanafunzi kwa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji

GEORGE MARATO TV
0


"Wakati wa mradi wa ujenzi zaidi ya wafanyakazi na mafundi 200 wa kitanzania waliajiriwa na kampuni ya CRJE (East Africa) Limited katika kuimarisha ushirikiano kati ya China na Tanzania," Meneja mradi wa majengo hayo kutoka CRJE (East Africa) Limited Dai Yanwei alisema wakati wa hafla ya kukabidhi majengo hayo.

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya ujenzi ya kutoka nchini China, ya CRJE (East Africa) Limited imekabidhi rasmi majengo mawili ya hosteli ya wanafunzi ambayo yamekamilika kwa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).

Kukamilika kwa majengo haya kunaashiria hatua kubwa katika maendeleo ya miundombinu inayoendelea katika taasisi hiyo. 

Hosteli hizo mbili ni sehemu ya mradi wa ujenzi ambao  umefadhiliwa na Benki ya Dunia chini ya Mradi wa Ujuzi wa Afrika Mashariki wa Mabadiliko na Ushirikiano wa Kikanda (EASTRIP). Mpango huu unalenga kuimarisha mazingira ya kujifunzia na kuboresha vifaa vya malazi kwa wanafunzi.

Kukamilika kwa majengo hayo kunaonyesha ushirikiano mkubwa kati ya NIT, CRJE, na mradi wa EASTRIP, na kuinyesha dhamira ya pamoja ya kuendeleza miundombinu ya elimu kwenye eneo la ukanda wa Afrika Mashariki.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mradi huo iliyofanyika katika Kampasi kuu ya NIT Mabibo, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, meneja mradi wa majengo hayo kutoka kampuni ya CRJE (East Africa) Limited Dai Yanwei alisema, "Tunamshukuru Mungu kwamba leo CRJE inakabidhi mradi wa ujenzi wa majengo haya mawili kwa mteja wetu (NIT) baada ya kufanya kazi mchana na usiku, ili kuhakikisha mradi huu unakamilika."

Dai Yanwei aliendelea kusema kuwa wakati wa mradi wa ujenzi wafanyakazi na mafundi wazawa zaidi ya 200 waliajiriwa na CRJE katika kuimarisha ushirikiano kati ya China na Tanzania.

Ujenzi wa majengo mawili ya hosteli za wanafunzi ulighalimu kiasi cha shilingi bilioni 10.8.

Majengo hayo mawili yatatumika kama hosteli za wanafunzi ili kukidhi uhaba wa huduma hiyo kwa Chuo cha NIT ambacho kwa sasa ina wanafunzi zaidi ya 16,000.

NIT ilitia saini mkataba wa mwaka mmoja wa ujenzi na Kampuni ya CRJE (East Africa) Ltd Novemba 2022 kwa ajili ya ujenzi wa majengo hayo mawili katika kampasi kuu ya Chuo hicho Mabibo, Dar es Salaam.

Hata hivyo, Yanwei alieleza kuwa mradi huo ulikabiliwa na ucheleweshwaji wa kukamilika kutokana na mvua kubwa iliyonyesha mwaka 2023 na 2024, ambayo ilileta changamoto kwenye kukamilika kwa muda muafaka.

Kwa upande wao, maofisa waandamizi kutoka Chuo cha NIT waliishukuru kampuni hiyo ya CRJE kwa kukamilisha mradi huo wa ujenzi.walithamini mradi wa ujenzi.

Kampuni ya CRJE imekuwa ikifanya kazi nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 50 tangu ilipoanzishwa mwaka 1969 na baadhi ya miradi ambayo imeshatekeleza ni pampja na mradi wa Reli ya Uhuru-TAZARA na vile vile  imeshatunukiwa mara tatu kuwa mkandarasi bora wa kigeni nchini Tanzania na imepata tuzo ya kifahari ya Luban kwa ubora wa ujenzi.

Kampuni hii ina wafanyakazi zaidi ya 5,000 kote Afrika Mashariki na inaendelea kupanua biashara yake huku wakiendea kuimarisha uhusiano kati ya China na Tanzania.

Katika kipindi cha miongo mitano iliyopita, CRJE imeshajenga jumla ya mita za mraba milioni tatu za miradi mbalimbali ya kihandisi nchini Tanzania.

Miradi mimubwa ambayo imeshajenga ni pamoja na Daraja la Nyerere, Chumba Kipya cha Mijadala ya Bunge, Ukumbi wa Mikutano Dodoma, Chuo Kikuu cha Dodoma, Rita Tower, Uhuru Heights, na Mwalimu Nyerere Foundation Square.

Kampuni hiyo imeshaweka rekodi ya kuwa kampuni inayoongoza kwenye kasi ya ujenzi katika nchi za Afrika Mashariki, ambapo inakamilisha ujenzi wa ghorofa moja kwa muda wa siku sita tu.

Kampuni hiyo iliweza kusanifu na kujenga Kituo cha Mikutano cha Dodoma kwa muda wa miezi saba tu.

Pamoja na kufanya kazi nchini, CRJE (East Africa) hufanya kazi  katika nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Sudan Kusini, Zimbabwe, Zambia, Msumbiji, Ethiopia na Malaysia.





Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top