Na Shomari Binda-Musoma
JIMBO la Musoma vijijini mkoani Mara linaratajia kufungua shule mbili mpya za sekondari za kidato cha tano na sita julai 1, 2025 baada ya ujenzi wake kukamilika.
Shule hizo zilizojengwa na serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ni pamoha na Suguti itakayoanza na wanafunzi 158 pamoja na Mugango itakayoanza na wanafunzi 62 ambazo usajili wake umekamilika.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijni Profesa Sospeter Muhongo imeeleza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya shule hizo kutarahisisha utoaji wa elimu, ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.
Mbunge huyo amesema baada ya muhula wa masomo kuanza atatembelea shule hizo na kugawa vitabu vya masomo ya sayansi kwa lengo la kupanua utoaji wa elimu.
Baadhi ya wadau wa elimu waliopokea taarifa hiyo wakiwemo wananchi wa jimbo la Musoma Vijijini wamemshukuru mbunge huyo kwa jitihada zake za kuinua elimu.
Wakizungumza na GMTV wamesema mbunge huyo ni mfano wa kuigwa katika kufatilia na kuhimiza masuala ya elimu.
Juma Mhina mkazi wa Kata ya Mugango amesema juhudi za mbunge huyo kwenye elimu zinaonekana kuanzia elimu ya awali,msingi hadi sekondari.
Amesema wananchi wanapaswa kumuunga mkono kutokana na juhudi hizo kubwa anazozifanya kwenye sekta hiyo.
" Tumeona taarifa kutoka ofisi ya mbunge juu ya kuanza masomo ya kidato cha 5 na 6 kwa kweli tunashukuru jitihada za mbunge wetu.
" Kwa hili hatupepesi macho tunamuomba agombee tena kwenye uchaguzi wa 2025 na tunaahidi kumchagua ili aendelee kutuletea maendeleo yakiwemo ya elimu kwa watoto wetu",amesema.
Sekondari nyingine zinazokaribia kukidhi vigezo vya uwepo wa High Schools za sayansi ni Mtiro Secondari iliyopo Kata ya Bukumi,Makojo Sekondari, Kata ya Makojo iliyopo Kata ya Bugwema Sekondari, Kata ya Bugwema,Kiriba Sekondari, Kata ya Kiriba,Nyakatende Sekondari, Kata ya Nyakatende na Etaro Sekondari iliyopo Kata ya Etaro
Vigezo muhimu kwa shule hizo ni pamoja na kuwa na maabara 3 za Jimbo la Musoma Vijijini Kufunguliwa Shule 2 Za "High Schools"za Masomo ya Sayansi ya sayansi,Bweni,Bwalo la chakula,Maji ya bomba pamoja na Umeme
Sekondari mpya zote zilizopata uwekezaji mkubwa kutoka serikalini kwenye jimbo la Musoma Vijijini zina maabara tatu za masomo ya sayansi ambazo ni Kabegi (Kata ya Ifulifu), Kurwaki (Kata ya Mugango), Wanyere (Kata ya Suguti), Kasoma (Kata ya Nyamrandirira), na Butata (Kata ya Bukima)
Mbunge wa jimbo hilo Profesa Sospeter Muhongo ameendelea kuwaimba wananchi kuongeza High Schools za Masomo ya Sayansi jimboni humo.