Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Hakuna Taifa Lisilokopa Duniani, Uchumi wa Dunia Umejengeka Kwa Mikopo. Kukopesheka ni Ishara ya Uchumi Imara


 _Deni la Tanzania ni himilivu na lina afya kiuchumi ukilinganisha na Mataifa mengi ya Afrika na ulimwenguni._ 


Na Bwanku M Bwanku.

Kwa siku za hivi karibuni kwenye Taifa letu kumezuka mjadala kuhusu nchi kukopa ama kutokukopa. Je kuna haja ya kukopa au kutokukopa au lipi ni lipi? Kama mwananchi nami ningependa kutoa mchango wangu kwa faida ya wote kuhusu huu mjadala.

Je ni muhimu kukopa? Hatuwezi kuleta maendeleo yetu wenyewe bila kukopa? Na maeneo mengine kama hayo yanayozunguka kwenye mjadala huu. 

Kwa Mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyosomwa Wiki iliyopita Alhamisi Machi 27, 2025 Deni la Taifa hadi kufikia muda huu ni Trilioni 97. Deni hili linahusisha mikopo kutoka kwenye Taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi n.k ambazo fedha zote hizo zikikopwa zinaelekezwa kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo ndani ya Taifa. 

Kwanza, ni muhumu ikafahamika kwamba hakuna nchi yoyote duniani inayofanya shughuli za kiuchumi kutekeleza miradi ya maendeleo bila kukopa.  Hata nchi tajiri ulimwenguni zinakopa kwa ajili ya kutekeleza shughuli zao za kiuchumi na miradi mbalimbali ya maendeleo tena zenyewe zikiwa na madeni makubwa sana kwenye Taasisi za Kimataifa za Fedha, Mabenki, Sekta binafsi n.k. 

Mpaka sasa Deni lote la Dunia ni zaidi ya Dola za Marekani Trilioni 315 yani mara 3 ya uchumi wa Dunia nzima ambao ni takribani Dola za Marekani Trilioni 105. 

Kwa Mujibu wa Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF), Mataifa makubwa pamoja na yale yanayokua kwa kasi kiuchumi kama Marekani, China, Vietnam, Japan, India na mengine mengi ndiyo yanaongoza kuwa na mikopo mikubwa. Zaidi ya asilimia 60 ya madeni yote ya Dunia yanadaiwa na Mataifa haya makubwa na yale yanayoendelea kwa kasi. 

Kwenye uchumi huu wa Dunia ya kisasa na shindani, hakuna nchi inaweza kufanya maendeleo yake bila kukopa au kushirikiana na Sekta binafsi kupitia Public-Private Partnership (PPP). Haipo Serikali inaweza kufanya mambo yote yenyewe bila kushirikiana na kutumia hizo PPP kwa kukopa kwenye Mabenki, Taasisi za Kifedha na hizo Sekta binafsi. 

Na sio kukopa tu bali kuruhusu pia sekta binafsi kuingia kwenye mzunguko wa uchumi na utoaji huduma kwa watu na serikali kukusanya kodi yake tu, kitu ambacho sasa kinafanyika duniani kote.

Na hata katika hesabu ya kawaida tu, uwezo wa kukopeshwa unaendana na uimara wa uchumi. Hayupo mtu anaweza kukukopesha kama hauko imara. Kwa Taifa, uchumi imara unaozalisha, unaosafirisha bidhaa nje, uchumi madhubuti ni kigezo cha kukopesheka kama ambavyo Taifa letu lilivyo imara ndiyo maana linakopesheka. Huwezi kukopesha kitu kisichoeleweka


Hiyo ndiyo kanuni ya uchumi, serikali haiwezi kufanya kila kitu yenyewe.

IMF wametoa afya ya deni na uchumi wa Taifa ambapo Tanzania bado iko wastani wa chini wa asilimia 47 kutoka wastani usiotakiwa kuvuka asilimia 65. Mataifa majirani na mengi ya Afrika yamevuka wastani wa afya wa Deni la Taifa kwa uchumi wa Nchi. Mfano Kenya wako asilimia 70, Rwanda 71, Uganda 51, Msumbiji 96, Malawi 84, Namibia 67, Congo 70. 

Tanzania bado iko mbali na mstari wa hatari wa Deni kuwa kubwa na bado inaendelea kuwa na uhimilivu wa deni kwa wastani wa chini kwa asilimia 47 ukilinganisha na Mataifa ya wenzetu ambayo yamevuka hadi mstari wa hatari wa Deni.

Kwa Takwimu za IMF na zile za Global debt, Marekani, Ulaya, China na Japan ndizo nchi zinazoongoza kwa kukopa ulimwengu. Marekani pekee yake inashare asilimia 31.8 ya Deni lote la Dunia kwenye Mashirika ya Fedha Duniani na Taasisi zake za Sekta Binafsi. Japan anashare asilimia 18.8 ya Deni lote la Dunia, wakati China yuko zaidi ya asilimia 10 na Ulaya ikiongozwa na Uingereza iko pia zaidi ya 10%.

Afrika nzima kwenye Deni zima la Dunia iko chini ya asilimia 2 wakati Mataifa Makubwa kuanzia Marekani, Japan, China na Ulaya yako zaidi ya asilimia 60 ya Deni zima la Dunia kwenye hizi Taasisi za Fedha (IMF na WB) na nyinginezo.

Kwahiyo haipo nchi isiyokopa Duniani, mjadala ni unakopa kupeleka huo mkopo wapi? Kama unakopa unakwenda kulipa mishahara na kufanyia shughuli zingine za anasa, hapo ndipo unaweza kuhoji ubovu wa kukopa lakini kama unakopa kujenga Reli za kisasa, huduma za wananchi na vitu vya namna hiyo, hakuna ubaya hata kidogo kukopa kwenye calculation za uchumi kwasababu unakopa, unawekeza halafu uwekezaji wako unapoanza kulipa unakuwa unalipa mkopo wako kidogokidogo huku ukiwa umeshaimarisha huduma, kutoa ajira kwa watu wako, kuzungusha uchumi n.k.

Muhimu mikopo hiyo ni kudhibitiwa ipasavyo na kuhakikisha inatumika ipasavyo kwenye shughuli tarajiwa za maendeleo na uchumi. 

Kinachoangaliwa kwenye kukopa ni unakopa kwa ajili ya nini? riba ikoje. Kwa mfano Mikopo yote tunayokopa Tanzania ina riba ndogo sana na yote inakwenda kwenye shughuli za kiuchumi na uzalishaji. Yako Mataifa ya wenzetu majirani nisingependa kuyataja tunasikia yanakopa kwa ajili ya kulipa mishahara, riba yake kubwa na mikopo ya muda mfupi. Kwenye calculation za uchumi aina hii ya ukopaji ndiyo inakatazwa na ni mbaya sana. 

Lakini Taifa letu mikopo yote inayochukua hakuna inayokwenda kwenye matumizi ya kawaida na anasa, yote inakwenda kwenye shughuli za maendeleo hasa kugharamia miradi ya maendeleo ambayo itakuja kuchangamsha shughuli za maendeleo za wananchi na Taifa na hivyo kuinua uchumi na kupata maendeleo huku ukiwa unalipa kidogokidogo na wakati huo ushafanya tayali maendeleo yako.

Mfano, tumekopa kugharamia ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), ujenzi wa miundombinu, kufanyia maboresho makubwa kwenye sekta ya afya na kadhalika.

Hii yote itainua uchumi wa mtu mmoja mmoja huku tukilipa kidogokidogo. Hata mkopo ule mkubwa kutoka Korea Kusini wa Trilioni 6.7 ni nafuu sana na riba yake ni ndogo mno ya asilimia 0.01 huku ukianza kulipwa baada ya miaka 25 ijayo.

Hayupo Tajiri au nchi Tajiri inatekeleza miradi yake mikubwa na ya kimkakati kwa kutumia tu fedha zake za walipa kodi, haipo nchi ya namna hiyo Duniani. Lazima ushirikiane moja kwa moja au nusu na Sekta binafsi kujenga uchumi wako. 

Matajiri wote na Mataifa yote Matajiri yanaingia Ubia na Makampuni makubwa na Taasisi za Kifedha wanapata mkopo halafu wanatekeleza uwekezaji wake halafu baada ya kumaliza na mradi ukianza kutoa matokeo na kuanza kazi, unakuwa unarejesha kidogokidogo kwa masharti na makubaliano mliyojiwekea. Hiyo ndiyo kanuni ya uchumi inayocontrol na kuendesha uchumi kote ulimwenguni. 

Kwahiyo kwenye mikopo hii unachoweza kujadili labda ni mikopo hii iwe ya kulipwa kwa muda mrefu, isiwe na riba kubwa, isiwe ya kibiashara na fedha zote za mikopo ziende kwenye shughuli za maendeleo na mzunguko wa kiuchumi, jambo ambalo mikopo yote ambayo tunaikopa hapa Tanzania kwenye Taasisi hizi za Kifedha inaingia kwenye maeneo niliyoyataja. 

Ndio maana unasikia Marekani inauza Treasury Bonds zake na nchi kama China inazinunua za thamani hadi dola za kimarekani Trilioni 1, huko ndio kukopa kwenyewe ili watekeleze miradi ya maendeleo.

Na huu mjadala wa kukopa ndiyo hiyo sababu inatufanya hadi leo Afrika tunakabiliwa na changamoto za kutokuwa na barabara za kutosha, hatuna reli za kutosha, hatuna maji ya kutosha, hatuna vituo vya afya vya kutosha, hatuna madarasa ya kutosha n.k

Wakati nchi za Afrika hazikopi vya kutosha ili kuweka hiyo miundombinu ya msingi, nchi tajiri zilizoendelea wanakopa ku-upgrade miundombinu ambayo tayari wanayo ili wapate maendeleo zaidi. Mfano hivi sasa China wanayo reli ambayo treni inasafiri kwa spidi ya km 300 kwa saa, sasa wamekopa kujenga reli yenye spidi ya kilomita 600 kwa saa. Sasa kuna kosa gani sisi kukopa kujenga barabara? Kama Nchi tajiri zinakopa kuvumbua teknolojia itakayofanya uzalishaji viwandani ufanywe na robot badala ya binadamu, kuna kosa gani sisi kukopa kwa ajili kujenga madarasa yatakayosaidia watoto wetu wasome kwa staha? 

Kama wenzetu wanakopa kwa ajili ya kwenda mwezini, kuna ubaya gani sisi kukopa kujenga reli ya Kaliua-Mpanda-Kalema? Kuna ubaya gani kukopa kupeleka Reli Dodoma, Tabora, Mwanza na kuendelea ambayo itafanya nchi yetu kuwa kitovu cha uchumi wa Afrika Mashariki kwa kusafirisha mizigo na nchi yetu kupata mapato makubwa sana yatakayotuwezesha kulipa kidogokidogo hiyo mikopo huku tukirahisisha sana shughuli zetu za kiuchumi na kijamii kwa miundombinu mizuri ya haraka. 

Hivyo ni muhimu sana kuielewa dhana ya nchi kukopa sio jambo geni na wala sio jambo baya na kila nchi duniani inakopa. Serikali  inavyokopa kutekeleza miradi muhimu ya maendeleo inapaswa kuungwa mkono na sio kubezwa.  Jambo la msingi ni lile alilosema Mhe Rais Samia kwamba tunapokopa miradi itekelezwe kwa ufanisi na kuzingatia thamani ya fedha inayotumika kutelekeza mradi "value for money".

Lakini pia tunakopa kupeleka kwenye shughuli za ujenzi wa miundombinu ya kiuchumi kama ujenzi huo wa reli na mengine ya maendeleo ambayo yanatuhakikishia kuimarisha zaidi uchumi wetu, mapato na kurahisisha shughuli za watu na maendeleo huku tukilipa polepole. Hiyo ndiyo kanuni ya uchumi inayoendesha Dunia na inayotumiwa na nchi matajiri wote Duniani. 

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na Bwanku M Bwanku ambaye ni Afisa Tarafa wa Tarafa ya Katerero iliyoko mkoani Kagera.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...