Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Wizaya ya Maji na DAWASA wakabidhi JKCI hundi ya milioni 20


 

Na Mwandishi Wetu

WIZARA ya Maji imeikabidhi Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), hundi la  shilingi milioni 20 kwaajili ya matibabu kwa watoto wenye changamoto mbalimbali  za magonjwa ya moyo.

Hundi ya fedha hizo ilikabidhiwa mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu Wizara hiyo,  Mhandisi Mwajuma Waziri  kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dk Angela Muhozya.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi hundi hiyo, Katibu Mkuu Mwajuma, alisema ziara hiyo ni sehemu ya shamrashamra za wiki ya maji inayofanyika kila mwezi wa tatu kila mwaka

 “Sisi tunatambua ukubwa wa tatizo la moyo kwasababu hata sisi hivi karibuni tulimpoteza mfanyakazi mwenzetu ambaye alifariki ghafla mkoani Dodoma kwa hiyo tukisikia mtu anachangamoto ya moyo tunapata hisia kuhusu tatizo hilo,” alisema

Alisema Wizara ya Maji imeandaa utaratibu ambapo wafanyakazi wake watakuwa wakifika kwenye taasisi hiyo kwaajili ya kufanya vipimo vya moyo ili watakaobainika kuwa na tatizo watibiwe mapema.

Alisema waliamua kuweka utaratibu huo wa kupima afya mara kwa mara baada ya kubaini kuwa kuna watumishi wengi wanaosumbuliwa na moyo ambao wakipima mapema watatibiwa na kuokoa maisha.

Alisema Wizara ya Maji kupitia taasisi zake itaendelea kukusanya fedha kwaajili ya kusaidia watoto na watu wazima wanaosumbuliwa na magonjwa ya moyo maeneo mbalimbali nchini.

“Nimeambiwa kwamba mnapanga kuongeza idadi ya wataalamu wa moyo hilo ni jambo jema sana kwasababu ongezeko hilo litakuwa msaada mkubwa kwasababu watu wenye matatizo watatibiwa kwa wakati na kwa ufanisi mkubwa,” alisema

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dk. Angela Muhozya alishukuru Wizara hiyo kwa msaada huo na kuomba wadau wengine waige mfano huo kwani wahitaji wa matibabu ya moyo wako wengi.

Alisema huduma za moyo bado hazijafika kwenye maeneo mbalimbali nchini na kuongeza kuwa watoto wanaohitaji matibabu ya moyo wamekuwa wakigundulika wakiwa wamechelewa.

 “Ndiyo maana tumeanzisha huduma yakwenda mikoa mbalimbali kila mwezi kutoa huduma za upimaji na kuwajengea uwezo wahudumu wa afya mikoani ili waweze kugundua tatizo mapema ili wawahishwe JKCI watibiwe haraka,” alisema

Aidha, alisema wagonjwa wengi wanaowachukua kutoka mikoani wanakuwa wanahitaji huduma ya kibingwa ya upasuaji wa tundu dogo na tundu kubwa tiba ambayo gharama yake iko juu kutokana na vifaa vinavyotumika kwenye matibabu hayo na dawa.

“Matibabu ni gharama kubwa kwa hiyo tukipata wadau wakutusaidia kama nyinyi tunafurahi sana kwasababu wagonjwa wengi wanatoka familia za kipato cha chini sana kwa hiyo wakipata matibabu mapema wanakwenda kuendelea na kazi zao kama kawaida za kuzalisha uchumi,” alisema

Naye Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa JKCI, Stella Mongella alisema idadi kubwa ya watoto wanazaliwa wakiwa na shida kwenye moyo yakiwemo ya kuzaliwa nayo kama matundu, mishipa kubana na mishipa kuvurugika.

Alisema maradhi hayo yanaweza kumpata mtoto aliyetumboni kama mama mjamzito atapata shinikizo la damu na sukari kuwa nyingi pamoja na maambukizi mengine ya virusi mbalimbali.

“Zaidi ya matatizo ya kuzaliwa nayo mtoto anaweza kupata maradhi haya ukubwani kama moyo kuwa mkubwa na dalili ya mtoto mwenye shida ya moyo ni kama kukua kwa shida, kupumua kwa shida na kutoka jasho jingi na katika kliniki yetu hapa tunapata watoto 10 kila siku wenye shida ya moyo,” alisema

Alisema watoto wanaohitaji matibabu ya moyo ya upasuaji wa kufungua kifua au kupitia mishipa ni 500 kila mwaka na kwamba idadi imekuwa ikiongezeka kila mwaka na gharama zake ni kubwa kutokana na vifaa na dawa zinazotumika.

Meneja Mkuu wa Global Medicare, Daniel Lazaro, alimshukuru Katibu Mkuu wa Wizara kwani walipoambiwa wachangie matibabu ya watoto wenye changamoto ya moyo  walitoa ushirikiano mkubwa kuhakikisha wanatoa mchango wao.

“Kwa taarifa iliyotolewa na daktari bingwa haoa inaonyesha tatizo bado ni kubwa na safari bado ni ndefu sana kwa hiyo tunaomba tutakapokuja tena mtuunge mkono kwasababu huduma hizi za upasuaji ni endelevu na tunatamani kumaliza wote wenye changamoto ya moyo,” alisema

Mwakilishi wa Ofisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA,  Evarlasting Lyaro, alisema huo ni mwanzo tu wa ushirikiano na JKCI na kwamba wataandaa MoU kwaajili ya kushirikiana kupima afya za wafanyakazi.




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...