Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Samia Aandikiwa Barua Hii na Kada wa Ccm


 *BARUA YA WAZI KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA*

*MH. SAMIA SULUHU HASSAN*


YAH. *MAONI YA KUBADILISHA UTARATIBU WA KURUDISHA MAJINA MATATU*


Mheshimiwa Mwenyekiti,

Husika na kichwa cha barua hapo juu

Kutokana na Idadi ya wananchi kuongezeka, Chama chetu pia kimeongeza Idadi ya wanachama wengi wenye sifa na uwezo wa kushika nafasi mbalimbali za Uongozi, 

Lakini pia idadi ya wasomi nayo imeongezeka hivyo sasa hivi tuna rasilimali watu kubwa,

Idadi hii kubwa inapelekea pia kuwa na wanachama wengi wanaowania nafasi za Uongozi, 

Hapo awali wanachama waliokuwa wakiwania nafasi za Uongozi walikuwa wachache na hata wengine walikuwa wakishawishiwa kuombwa kugombea hivyo ilikuwa ni rahisi kuchuja na kupata majina matatu ya wanachama watakaokwenda kupigiwa kura,Lakini sasa hivi hali imebadilika

Imefikia hatua mamia na huenda hata maelfu ya wanachama wakajitokeza kuomba ridhaa ya kuwania nafasi za Uongozi hivyo si rahisi kwa majina matatu tu kutosha kumpata mtu sahihi anayestahili kuongoza na zipo sababu,

1) Jina la kwanza ni muhimu kupitishwa Kiongozi aliyepo madarakani ili atetee nafasi yake

2) Jina la pili ni muhimu kupitisha jina la mgombea kwa kuzingatia usawa wa Kijinsia (Gender)


Hivyo inabaki nafasi moja tu ya mgombea kwa hawa wanachama wote wanaogombea,

Kimsingi nafasi moja hii ni finyu mno kwa wanachama hususani wanachama wale wasio na Viongozi wanaoweza kuwasemea kwenye Vikao,


Si hivyo tu,

Kipindi cha Uchaguzi ni kipindi kizuri sana kwa Chama kuona vipaji vipya vya Uongozi,

Kupitia Chaguzi tunaona vipaji vya mikakati, vipaji vya maono, vipaji vya kusema kwa wanachama wanaogombea n.k

Hivyo ikiwa tutatumia utaratibu huu wa kurudisha majina matatu vipaji vyote hivi hatutaweza kuviona na huenda wengine wakakata tamaa na kuachana kabisa na Siasa na wengine wakahamia vyama vya Upinzani kutafuta fursa ya kugombea na kuwatumikia wananchi,

Utaratibu huu wa majina matatu utakifanya Chama kionekane ni cha watu wachache, familia chache watakaosemeana wenyewe kwenye vikao na wengine wajione sio sehemu ya CCM kwasababu ya kukatwa majina yao na kupitishwa wachache wanaojulikana na wanaotokea familia zinazojulikana hivyo itapelekea Chama kupunguza Idadi kubwa ya wafuasi na wanachama ambao watatafuta fursa katika vyama vingine,

Utaratibu huu wa majina matatu unaondoa haki ya mwanachama ya Kuchagua na kuchaguliwa, Kwasababu wajumbe wanaweza kuletewa majina matatu ya wanachama ambao si chaguo lao, 

Hivyo haki yao ya kuchagua itakuwa imepokwa,

Vilevile pia wanachama watakaokatwa majina yao watakuwa wameondolewa haki yao ya Kikatiba ya kuchaguliwa, Utaratibu huu wa majina matatu unakwenda kuminya Demokrasia ndani ya Chama kwasababu utazuia wanachama wengine kuonekana, kupata fursa ya kugombea na kupata fursa ya kumchagua Kiongozi wanayemtaka,

Utaratibu huu wa kurudisha majina matatu unapunguza nguvu ya maamuzi ya wanachama na kuvipa vikao nguvu ya kuwaamulia na kuwachagulia wanachama Viongozi wao,

Utaratibu huu wa majina matatu unaua Vijana na vizazi vijavyo vya kisiasa kwasababu kwa kiasi kikubwa hivi havijulikani na vikao vya maamuzi bali vinapambana kutafuta kuonesha vipawa vyao,Kipindi cha Uchaguzi ndicho kinakuwa kipindi kizuri sana kwa kizazi hiki kipya kuonekana hivyo utaratibu wa majina matatu unakwenda kukizika rasmi kizazi hiki kisionekane,


Siasa ni mchezo wa fitna

Viongozi waliopo madarakani pia nao wanaweza wakafanya fitna ili wanachama wenye nguvu wasipitishwe kugombea nao,  

Hili tumelishuhudia maeneo mengi ambapo inafikia hatua wanachama wanaamua kumchagua mtu dhaifu ilimradi tu wamuondoe Kiongozi aliyepo madarakani, 

Siasa ni uwekezaji wa muda mrefu wa hali na mali hivyo ikiwa hawa wanachama waliowekeza kwa wananchi wao kisha wakaja kukatwa majina yao lazima itakwenda kuhatarisha mno Uhai wa chama na kupelekea mipasuko mikubwa kwenye Chama, 

Tuutumie Uchaguzi wa mwaka 2015 kama rejea lilipokatwa jina la Mh. Edward Lowassa ilipelekea kuwepo na mpasuko mkubwa ndani ya Chama,


Tumeona huko nyuma,

Wanachama wanapoletewa majina ambayo sio machaguo yao waliamua kushirikiana na vyama pinzani kukihujumu chama,

Tumeona kuna wanachama ambao walikuwa Viongozi wazuri lakini walipokatwa walikwenda Upinzani na hatimaye tukapoteza Chaguzi mbalimbali, 

Ili yasitokee haya ni vema chama kikatafakari upya kuhusu mfumo huu wa majina matatu,

Naomba ikikipendeza Chama kiongeze majina walau yawe kumi (10) kutokana na wingi wa wanachama wanaoomba kuwania nafasi za Uongozi,

Ama chama kikiona inafaa kipitishe wanachama wote kugombea kisha vikao viamue kuhusu majina matatu miongoni mwa wanachama watakaoongoza kwa kura,

Uchaguzi wa mwaka 2020 binafsi niliwania Ubunge kura hazikutosha nilikuwa mtu wa tatu kwa kura,

Lakini kama ungekuwa utaratibu wa chama kuleta majina matatu naamini kwa asilimia zaidi ya mia moja jina langu lisingepitishwa na wala lisingedhaniwa kama ni jina ambalo linaweza kuleta ushindani na kuwa watatu kwa kura,

Utaratibu huu wa majina matatu umetukatisha tamaa na kuturudisha nyuma wanachama wengi tulio na nia ya kuwania nafasi mbalimbali za Uongozi,

Kwa kuwa chama chetu ni sikivu na kinajali mno wanachama wake na kinafanya Siasa kulingana na wakati,

Ni matumaini yangu makubwa kuwa maoni haya yatazingatiwa na marekebisho yenye tija yatafanywa kwa ajili ya kuboresha na kukiimarisha chama chetu!

Wako katika ujenzi wa Chama cha Mapinduzi na Taifa la Tanzania 

*IBRAHIM JEREMIAH*

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...