Rais wa zamani wa Ufaransa afikishwa mahakamani akituhumiwa kupokea pesa kutoka kwa Gaddafi

GEORGE MARATO TV
0


Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy amefikishwa mahakamani siku ya Jumatatu, kwa tuhuma za kupokea mamilioni ya euro za ufadhili usio halali katika kampeni za kugombea urais 2007, kutoka kwa hayati Rais wa Libya Muammar Gadaffi.

Sarkozy amekuwa akikana mashtaka hayo na kesi hiyo itaendelea kwa muda wa miezi mitatu.

Kiongozi huyo wa zamani wa chama cha kihafidhina anakabiliwa na mashtaka ya "kuficha ubadhirifu wa fedha za umma, ufisadi, ufadhili haramu wa kampeni na njama ya kufanya uhalifu," imesema ofisi ya mwendesha mashtaka wa fedha.

Waendesha mashitaka wanasema mwaka 2005, Sarkozy, aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa wakati huo, aliafikiana na Gaddafi, ili kupata ufadhili wa kampeni ili kuiunga mkono serikali yake katika uwanja wa kimataifa ambapo ilikuwa imetengwa.

Gaddafi aliyeondolewa madarakani kisha kuuawa mwaka 2011.

Wachunguzi wanadai alifanya mapatano ya kifisadi na serikali ya Libya, yaliyohusisha majasusi wa Libya, gaidi aliyepatikana na hatia, wauzaji silaha na madai kwamba Gaddafi alitoa pesa kufadhili kampeni ya Sarkozy na pesa hizo kusafirishwa hadi Paris katika masanduku.

Wakili wa Sarkozy amesema kesi dhidi ya rais huyo wa zamani ni uzushi na hakuna ufadhili wa pesa kutoka Libya katika kampeni yake.

Iwapo atapatikana na hatia, Sarkozy anaweza kufungwa jela hadi miaka 10 na faini ya euro 375,000 ($386,000).

Sarkozy katika miaka ya hivi karibuni amekabiliwa na safu ya kesi za kisheria. Mwezi Desemba, mahakama ya juu zaidi ya Ufaransa ilikubali hukumu dhidi yake juu ya rushwa na kutafuta upendeleo kutoka kwa jaji.

Sarkozy ameagizwa kuvaa bangili ya kielektroniki kwa mwaka mmoja badala ya kwenda jela, ikiwa ni mara ya kwanza kwa rais wa zamani wa Ufaransa kuamriwa hivyo.

Katika kesi nyingine, Sarkozy alipatikana na hatia ya kuficha matumizi haramu ya kampeni, na kesi hiyo inasubiria.





Chanzo Al Jazeera

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top