Mheshimiwa Simbachawene akabidhi Gari la Wagonjwa Mtera

GEORGE MARATO TV
0



   Mtera: 

🗓️ 07/01/2025.


    📍Ikiwa takribani siku  42 zimepita ambazo ni sawa na mwezi mmoja na siku kumi na mbili lilipofanyika zoezi la ufungaji wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwezi Novemba leo hii wananchi hao wa Kata ya Mtera wamefanikiwa kukabidhiwa gari hilo la kubebea wagonjwa 

Akikabidhi gari hilo Mheshimiwa Waziri wa nchi Ofisi ya Rais menejment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Mb) wa Jimbo la Kibakwe Mheshimiwa George B.Simbachawene mbele ya viongozi wengne wa serikali Mheshimiwa Simbachawene amesisitiza kulitunza gari hilo ili liweze kuwa msaada kwa wananchi hao hasa akina mama wajawazito ambao wengi wamekuwa wakipoteza maisha kwa kutoweza kukimbizwa haraka katika kituo Cha afya kwaajili ya kupewa huduma ya kujifungua.

 

Naye diwani wa Kata hiyo Mheshimiwa Robert Maulya amemshukuru Mheshimiwa Simbachawene ambae kwa Umoja wake yeye na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano w Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan wameweza kuisikia kero hiyo ya wananchi na kuwatatulia ndani ya muda mfupi wa siku 42 hivyo amemuomba Mheshimiwa Simbachawene amfikishie salamu za wananchi wake wa Kata hiyo ya Mtera na kuahidi kuwa watavuka na Mheshimiwa Mbunge pamoja na Mheshimiwa Rais.

   Katika makabidhiano  hayo ya gari wameweza kufika viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Mpwapwa akiwemo Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi.Mwanahamisi Ally.

Imetolewa na:

Afisa habari wa Jimbo la Kibakwe


07/01/2025

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top