Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

"Tuendelee Kuiunga Mkono Serikali Yetu Kwa sababu ni Serikali Sikivu na inatatua Kero za Wananchi", Mtendaji Mkuu Temesa

 

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) Lazaro Kilahala amewaomba wananchi wa Kanda ya Ziwa na maeneo mengine ya Nchi kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Sita inayooongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwakuwa Serikali hiyo ni Serikali sikivu inayowajali wananchi wake kwa kutatua kero zinazowakabili hasa za usafiri wa maji ambao ndio umekuwa tegemeo kubwa kwa wakazi wanaoishi visiwani na pembezoni mwa Ziwa Victoria.

Kilahala ameyasema hayo leo Tarehe 15 Desemba, 2024 wakati alipofanya ziara ya kikazi katika eneo la Buyagu Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza, kukagua maendeleo ya ujenzi wa maegesho mapya ya kivuko cha Buyagu- Mbalika yanayoendelea kujengwa katika eneo hilo. 

Kilahala amesema, katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inafanya kazi ya ujenzi wa vivuko vipya vitano huku vitatu kati ya hivyo vikiwa vinatarajiwa kupelekwa katika maeneo ambayo hayakuwahi kabisa kuwa na vivuko hapo awali na viwili vinapelekwa maeneo ambayo vivuko vilikuwepo lakini mahitaji yameongezeka na hivyo kuhitaji vivuko vikubwa zaidi ili kuhakikisha wananchi hao wanapata huduma nzuri na ya kuridhisha.



‘’Hapa tuko eneo linaitwa Buyagu, kuna kivuko kipya kitakuja hapa kitakuwa kinafanya kazi kati ya hapa Buyagu na upande wa pili unaitwa Mbalika, lakini katika vile vivuko vitatu vipya nilivyovisema kingine kitapelekwa Ijinga- Kahangala ambako pia ni eneo ambalo lilikuwa halina huduma ya kivuko kabisa na kivuko kingine cha tatu kitapelekwa Bwiro- Bukondo, haya ni maeneo yalikuwa hayana vivuko.’’ Amesema Kilahala.

Mtendaji Mkuu ameongeza kuwa, baada ya kukamilisha ujenzi wa maegesho katika vituo, Serikali itaendelea na ujenzi wa majengo ya kupumzikia abiria (Waiting Lounges) wakati wakisubiri vivuko na amesema uwekezaji huo wa ujenzi wa maegesho ya vivuko pamoja na ujenzi wa majengo ya kupumzikia abiria (Waiting Lounges) utaendelea pia kufanyika katika maeneo yote mapya ikiwemo Ijinga-Kahangala na Bwiro-Bukondo. Aidha amesema kuwa maeneo ya Kisorya na Rugezi pia, uendelezaji wa miundombinu unafanyika ambapo majengo ya kupumzikia abiria na maegesho mapya yenye viwango vya kisasa, yanaendelea kujengwa na Serikali ili kuboresha utoaji huduma.

‘’Kipekee kabisa tunaipongeza na kuishukuru Serikali yetu kwasababu ni Serikali sikivu inaangalia mahitaji na shida za wananchi na kuzipatia majibu, mfano hapa Buyagu-Mbalika, wananchi wamekuwa na shida ya usafiri kwa zaidi ya miaka ishirini hawakuweza kupata kivuko, lakini Mheshimiwa Rais ndani ya miaka yake mitatu hii tunaona nini kinaendelea nyuma yetu, ni Serikali sikivu, Serikali inayotatua changamoto na madhila yanayowakabili wananchi ili kuhakikisha maisha ya wananchi yanaendelea kuwa bora.’’ Alisema Kilahala na kuongeza kuwa hayo ndiyo maono ya Mheshimiwa Rais ya kutaka kuona wananchi wake wanaishi na kupata huduma katika ubora ambao ni stahiki.

Naye Mkandarasi anayesimamia ujenzi wa maegesho hayo kutoka Vikosi vya ujenzi, QS Basesa Nyendeza Simion, amesema ujenzi wa maegesho ya kivuko upande wa Buyagu tayari umefikia asilimi sitini na mara watakapomaliza kazi hiyo upande wa Buyagu watahamia upande wa Mbalika. Basesa ameongeza kuwa maegesho mengine wanayoyasimamia ni yale yaliyoko Mkoa wa Mara eneo la Mwigobero ambayo ujenzi wake unaendelea na umefikia asilimia saba pamoja na maegesho ya Bukimwi upande wa Wilaya ya Ukerewe ambako ujenzi wake umefikia asilimia sabini. Basesa ameongeza kuwa maegesho yote hayo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi wa sita mwaka 2025.

Katika ziara hiyo, Kilahala ameambatana na Mkurugenzi wa Uendeshaji na Ujenzi wa Vivuko Mha. Sylvester Simfukwe ambapo ziara yao ilianzia katika eneo la Ilunda- Luchelele ambako walikagua maendeleo ya ujenzi wa maegesho unaoendelea katika kituo hicho kabla ya kwenda Wilaya ya Magu ambako nako pia walipata fursa ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa maegesho mapya ambapo kwa upande wa Kahangala maegesho hayo yamefikia hatua za mwisho za ujenzi wake, walifika pia upande wa Ijinga ambako kazi ya usombaji wa mawe ya kujengea maegesho hayo inatarajiwa kuanza hivi karibuni, wamekagua pia maegesho ya Mwigobero-Kinesi Wilayani Musoma pamoja na Kisorya Wilayani bunda kabla ya kumaliza ziara yao leo katika eneo la Buyagu Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.









Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...