Serikali imetoa ufafanuzi kupinga uongo wao

GEORGE MARATO TV
0

 

Serikali inapenda kutoa ufafanuzi kwa umma kufuatia taarifa potofu iliyotolewa na

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kuhusu uteuzi wa Mbunge uliofanywa

na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 02 Aprili 2026 chini ya Ibara ya

66(1)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Ni sahihi kuwa kabla ya uteuzi huo, Mheshimwa Angela Kizigha alikuwa Mbunge wa

Bunge la Afrika Mashariki (EALA).


Hata hivyo, kwa mujibu wa Ibara ya 51(3)(c) ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya

ya Afrika Mashariki, Mbunge wa EALA hukoma kuwa Mbunge endapo atateuliwa

kuwa Mbunge wa Bunge la Nchi Mwanachama.

Kutokana na masharti hayo, ubunge wa EALA kwa Mheshimiwa Angela Kizigha na

Waheshimiwa Dkt. Ngwaru Maghembe na James Milya ulikoma baada ya

kuteuliwa/kuchaguliwa kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania.


Aidha, Ibara ya 50 ikisomwa pamoja na Ibara ya 52 ya Mkataba inatoa mamlaka kwa

Bunge la Nchi Mwanachama kujaza nafasi zilizo wazi katika Bunge la Jumuiya ya

Afrika Mashariki kulingana ratiba zake kama zitakavyopangwa kwa mujibu wa

taratibu husika.


Hivyo, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litajaza nafasi tatu (3)

zilizoachwa wazi, kama itakavyolezwa katika ratiba ya shughuli za Bunge. Aidha,


inapaswa kufahamika kuwa mchakato wa kujaza nafasi hizo unapaswa kuanzia

katika vyama vya siasa ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 50(1) ya Mkataba wa

Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kwa msingi huo, Serikali inasisitiza kuwa hakuna mgongano wowote kati ya uteuzi

uliofanywa chini ya Katiba na masharti ya Mkataba wa Kuanzishwa Jumuiya ya Afrika

Mashariki.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top