Rais wa Rwanda Paul Kagame amemteua Dkt Justin Nsengiyumva, kuwa Waziri Mkuu mpya.
Nsengiyumva anatwaa nafasi ya Édouard Ngirente, ambaye amehudumu katika wadhifa wa Waziri Mkuu tangu mwaka 2017.
Nsengiyumva ni mtaalam wa masuala ya uchumi kutoka chuo kikuu cha Leicester, na awali alihudumu kama Naibu Gavana wa benki kuu nchini Rwanda tangu Februari mwaka huu.
Kando ya Nsengiyumva, Rais Kagame pia ameteua mawaziri mapya wanne akiwemo wa michezo,Vijana na Sanaa, Afya pamoja na Kilimo na Mifugo