Waziri wa Mambo ya Nje wa Italia Antonio Tajani amesema leo Ijumaa kuwa nchi hiyo haiwezi ikakubali “umwagaji damu na njaa” katika Ukanda wa Gaza.
Ameishutumu Israel lakini akaelezea kuwa Italia haiko tayari kulitambua taifa la Palestina kama inavyopanga kufanya Ufaransa.
“Kamwe hatuwezi tukakubali umwagaji damu na njaa,” alisema Tajani, kwa mujibu wa shirika la habari la Italia la ANSA.
Aliongeza kuwa Italia inaweza tu kuitambua Palestina “wakati sawa kama utambuzi wao wa taifa la Israeli