Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Sekta ya Madini Yakusanya Zaidi ya Bilioni 902 Kati ya Lengo la Trilioni Moja


*Mchango Wafikia Asilimia 10. 1 katika Pato la Taifa (GDP) kwa mmoja kabla ya lengo*


 📍 *Dodoma*

Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amebainisha kuwa Sekta ya Madini nchini imeendelea kupiga hatua kubwa, ambapo maduhuli ya zaidi ya shilingi bilioni 902 sawa na asilimia 90.2 ya lengo la kukusanya Shilingi trilioni moja kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 kufikia Mei 15, 2025, ikiwa ni kabla ya kumalizika kwa Mwaka wa Fedha, huku zikiwa zimesalia zaidi ya siku 45, jambo linalotoa matumaini makubwa kuwa lengo litafikiwa kwa asilimia 100.

Ameyasema hayo leo Mei 15, 2025, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Kipindi cha Miaka Minne ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Mavunde ameeleza kuwa, Sera ya Madini ya Mwaka 2009 na Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Taifa ulielekeza Sekta ya Madini ikichangia asilimia 10 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2025. Hata hivyo, tayari mwaka 2024 sekta hiyo imefikia mchango wa asilimia 10.1, ikiwa ni mafanikio yaliyotangulia muda uliopangwa.

“Tumefanikiwa kuvuka lengo la kitaifa. Mwaka 2021 Sekta ya Madini ilichangia asilimia 7.3 kwenye pato la Taifa, mwaka 2023 ilifika asilimia 9.1, na hivi sasa tupo kwenye asilimia 10.1 kufikia mwaka 2024. Hili ni jambo la kujivunia,” amesema Mhe. Mavunde.


*Makusanyo ya Serikali Yaongezeka kwa Kasi*


Katika kipindi hicho, maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini yameongezeka kwa zaidi ya asilimia 20, kutoka Shilingi bilioni 623.24 mwaka 2021/2022 hadi kufikia bilioni 753.18 mwaka 2023/2024. Hadi kufikia Mei 9, 2025, Wizara ya Madini ilikuwa imekusanya Shilingi bilioni 902, sawa na asilimia 90.2 ya lengo la mwaka.


*Upatikanaji wa Fedha za Kigeni na Ajira Nchini*


Sekta ya Madini imeendelea kuwa mhimili mkubwa wa upatikanaji wa fedha za kigeni. Mnamo mwaka 2023, mauzo ya madini nje ya nchi yalifikia Dola za Marekani bilioni 3.55, yakichangia asilimia 46.1 ya mauzo yote ya bidhaa nje ya nchi. Aidha, Kampuni za wazawa zimenufaika kwa kiasi kikubwa, ambapo bidhaa na huduma zenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 3.5 sawa na asilimia 92 ya thamani ya manunuzi yote migodini zilitolewa na Watanzania.


Kwa upande mwingine, Sekta ya Madini imezalisha ajira 19,356 katika kipindi cha mwaka 2021 hadi 2023, ambapo kati ya hizo ajira 18,853 sawa na asilimia 97.4 ni Watanzania.


*Masoko na Minada ya Madini Yachochea Biashara*

Waziri Mavunde ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini imeendelea kuimarisha mazingira ya biashara ya madini kwa kuongeza idadi ya masoko na vituo vya ununuzi hadi kufikia 152 nchi nzima. Aidha, minada ya madini ya vito imeanzishwa upya baada ya kusimama tangu mwaka 2017. Mnada wa kwanza ulifanyika Desemba 2024 na wa pili Aprili 2025, ambapo madini yenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 2.5 yaliuzwa na kuiwezesha Serikali kukusanya zaidi ya Shilingi milioni 163 kupitia mrabaha, ada za ukaguzi, usimamizi na ushiriki wa minada hiyo.


*Maono ya Vision 2030: Madini ni Maisha na Utajiri*


Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde ameeleza kuwa utekelezaji wa Vision 2030: Madini ni Maisha na Utajiri unaendelea kwa kasi. Maono hayo yanalenga kuimarisha usimamizi wa rasilimali za madini, kuongeza upatikanaji wa taarifa za jiosayansi hususan za kina za jiofizikia, na kuhakikisha sekta ya madini inaunganishwa kikamilifu na sekta nyingine kama viwanda, kilimo, fedha na ujenzi kwa ajili ya uchumi shirikishi na endelevu.


*Programu ya Mining for A Brighter Tomorrow – MBT*


Aidha, kupitia programu ya Mining for Brighter Tomorrow, Serikali inatekeleza mpangoi mahsusi kwa ajili ya kuwainua wachimbaji wadogo, hususan wanawake na vijana, kuwa kuwapatia maeneo ya kuchimba na kuwasaidia teknolojia za kurahishisha shughuli zao.

Katika kuwajengea mazingira bora wachimbaji wadogo, Serikali imefuta leseni na maombi 2,648 ambayo hayakuendelezwa na ina mkakati wa kuzigawa upya kwa wachimbaji wadogo. Aidha, STAMICO imeendelea kuwalea wachimbaji hao kupitia vituo vya mfano na mitambo ya CIP, huku Kamati maalum ya watu 6 ikiundwa kwa ajili ya kuishauri Serikali kuhusu njia bora za kuwawezesha wachimbaji hao. Pia, mfumo wa dhamana (Credit Guarantee Scheme) umeandaliwa, sambamba na ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kuchakata chumvi kwa ajili ya kusaidia wakulima wa chumvi nchini.


*Mkakati wa Uongezaji Thamani Mdini Ndani ya Nchi*


Kwa upande wa kuongeza thamani ya madini, Mhe. Mavunde amesema, Serikali inaendelea kuimarisha viwanda vya usafishaji ambapo hadi sasa kuna viwanda 9 vya kuchakata madini ya metali kama shaba na nikeli ikiwemo Kiwanda kikubwa cha kusafisha makinikia cha Kbanga Nickel kinachojengwa eneo la Buzwagi, ambapo vingine 6 kati ya hivyo vikitarajiwa kujengwa Dodoma. 

Vilevile, Ujenzi wa jengo la ghorofa nane la Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) unaendelea Jijini Arusha kwa ajili ya kuongezea thamani madini ya vito. 


*Mafanikio Mengine kwa Ufupi*


Katika kipindi cha miaka minne ya Rais Dkt. Samia, Jumla ya leseni za Uchimbaji Mkubwa, wa Kati na Mdogo 34,348 zimetolewa na Kampuni mbalimbali zimesaini mikataba kwa ajili ya kuanza uendelezaji wa migodi nchini. 

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) nalo limepiga hatua kubwa, kutoka kutengeneza faida ya shilingi bilioni 1 kwa mwaka hadi kufikia bilioni 84 kwa mwaka ndani ya miaka mitatu,

Mafanikio hayo ni taswira chanya ya sekta ya madini, ikiwa ni uthibitisho usimamizi na miongozo inayohakikisha Watanzania wananufaika na rasilimali madini, jambo linaloifanya Tanzania kusimama imara kama moja ya nchi zenye mifumo madhubuti ya usimamizi na ukuaji wa sekta ya madini barani Afrika na kuvutia matifa kadhaa kuja kujifunza hapa nchini.




Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...