Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Raila Odinga Avuna Matunda ya Handshake na Rais Ruto


 MKATABA wa ushirikiano ambao Kiongozi wa ODM Raila Odinga alitia saini na serikali ya Kenya Kwanza unaendelea kuzaa matunda huku washirika wake wakinufaika na nyadhifa za makatibu wa wizara.

Katika mabadiliko ambayo Rais William Ruto alifanyia makatibu wakuu wa wizara Alhamisi, Machi 20, 2025, washirika wa Bwana Odinga waliteuliwa kuhudumu katika Idara za wizara muhimu.

Katika mabadiliko hayo, Rais Ruto aliteua makatibu 14 wapya, zaidi ya 10 wakiwa washirika wa Bw Odinga na kuwahamisha sita kupisha wale wa waziri mkuu huyo wa zamani.

Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Ikulu, Hussein Mohammed, Rais Ruto amemhamisha Amos Gathecha kutoka wizara ya utumishi wa umma na kumteua kuwa Naibu Mkuu wa Huduma za Umma.

Prof Edwin Kisiangani, ambaye alikuwa akihudumu katika Wizara ya ICT, sasa atahudumu kama mshauri na mwanachama wa baraza la washauri wa kiuchumi wa rais.

Makatibu wapya 14 wanaohusishwa na Raila ni pamoja na Dkt Jane Kare Imbunya (Idara ya Utumishi wa Umma), Bi Regina Akoth Ombam (Idara ya Biashara), Cyrell Wagunda Odede (Idara ya Uwekezaji wa Umma katika Hazina ya Kitaifa na Mipango ya Uchumi.

Dkt Caroline Wanjiru Karugu ambaye alikuwa mwanachama wa kampeni ya Raila katika uchaguzi mkuu wa 2022 na ule wa uenyekiti wa Tume ya Muungano wa Afrika (AUC) Idara ya Masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) naye Dkt Oluga Fredrick Ouma akisimamia Idara ya Huduma za Matibabu, Wizara ya Afya.

Bi Judith Pareno ambaye aliwahi kusimamia bodi ya uchaguzi ya ODM na Mshirika mwingine wa Bw Odinga atasimamia Haki za Binadamu na Masuala ya Katiba katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na Idara ya Haki huku Carren Ageng’o Achieng akisimamia Idara ya Huduma za Ustawi wa Watoto katika Wizara ya Kazi na Ulinzi wa Jamii.

Bw Ahmed Abdisalan Ibrahim aliteuliwa kuwa Katibu wa Idara ya Uratibu wa Serikali ya Kitaifa katika Ofisi ya Mkuu wa Mawaziri.

Dkt Bonface Makokha atakuwa Katibu wa Idara ya Mipango ya Uchumi katika Hazina ya Kitaifa na Mipango ya Uchumi naye Prof Abdulrazak Shaukat atasimamia Idara ya Sayansi, Utafiti na Ubunifu, Wizara ya Elimu katika wadhifa huo huo.

Rais William Ruto pia alimteua Bw Stephen Isaboke kuwa Katibu, Idara ya Utangazaji na Mawasiliano ya Simu, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Uchumi wa Kidijitali kuchukua nafasi ya Profesa Edward Kisiang’ani ambaye ameteuliwa mshauri na mwanachama wa baraza la kiuchumi la rais.

Bw Michael Lenasalon aliteuliwa katibu Idara ya Ugatuzi, Afisi ya Naibu Rais kuchukua nafasi ya Terry Mbaika ambaye alihamishiwa Idara ya Maendeleo ya Anga na Usafiri wa Angani, Wizara ya Barabara na Uchukuzi.

Bw Fikirini Katoi Kahindi Jacobs atakuwa Katibu, Idara ya Masuala ya Vijana, Wizara ya Masuala ya Vijana na Michezo huku Bw Aden Abdi Millah akiwa Katibu, Idara ya Uchukuzi wa Baharini na Masuala ya Majini, Wizara ya Madini, Uchumi wa Majini na Masuala ya Baharini.

Aliyekuwa katibu wa uhamiaji Prof Julius Bitok alihamishwa kutoka Idara hiyo hadi Idara ya Elimu ya Msingi, Wizara ya Elimu akibadilishana na Dkt Belio Kipsang.

Bw Ismael Madey naye alihamishwa kutoka Idara ya Masuala ya Vijana na Uchumi wa Ubunifu hadi Idara ya mipango Maalum, Wizara ya Utumishi wa Umma.

Aliyekuwa katibu wa Huduma za Matibabu katika wizara ya afya Harry Kimtai alihamishwa hadi Idara ya Madini, Wizara ya Madini. Kimtai alimpisha Dkt Oluga, mshirika wa Bw Odinga.

Aliyekuwa Waziri wa Afya, Susan Nakhumicha, alirudi katika serikali, miezi tisa baada ya kupoteza wadhifa wake wakati huu akiwa Balozi wa Kenya katika Shirika la Makao la Umoja wa Mataifa(UN-Habitat) jijini Nairobi.

Mbali na Nakhumicha, Rais pia aliwateua James Buyekane Muhati na Abdi Dubat Fidhow kuwa mabalozi wa Kenya katika Guangzhou, China, na Arusha, Tanzania, mtawalia.

Bw Peter Tum aliteuliwa kuwa Balozi wa Kenya katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), huku Alfred K’Ombundo akiteuliwa kuwa Naibu Mkuu wa Ubalozi wa Kenya nchini Ubelgiji.

Katika taarifa rasmi, Ikulu ilisema waliteuliwa kwa mujibu wa Kifungu cha 132 (2) (e) cha Katiba.

Kulingana na Hussein Mohamed, majina yao tayari yamewasilishwa kwa Bunge la Taifa kuthibitishwa inavyohitaji sheria.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...