Waziri wa Ulinzi na Jkt Apokea Ndege Kwa Ajili ya Oparesheni za Kijeshi,Huku Jwtz Likisema Lipo Tayari Wakati Wowote

GEORGE MARATO TV
0


 Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa DK. STERGOMENA TAX amepokea ndege ya usafirishaji ya kijeshi iliyotolewa na jeshi la falme za kiarabu kwaajili ya kuimarisha sekta ya ulinzi ndani na nje ya nchi,huku JWTZ likisema lipo tayari kwa lolote na wakati wowote kutekeleza majukumu yake.

Dkt TAX amesema ndege hiyo pia itasaidia JWTZ katika oparesheni mbalimbali za kijeshi na kiraia ikiwa dhamira ya Rais na Amiri mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan za kuimarisha jeshi la wananchi la Tanzania ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiusalama.

Amesema ujio wa ndege hiyo pamoja na mafunzo ya wataalamu ni matunda yanayotokana na mahusiano mazuri kimataifa yanayofanywa na Rais DK. SAMIA SULUH HASSAN kwani amendelea kuwa mstari wa mbele katika kuimarisha kwa kuhakikisha sera ya mambo ya nje yanatafsiriwa kwa vitendo.

Aidha amewataka wataalamu waliopatiwa mafunzo kuhakikisha wanafanya kazi kwa kujiamini kwani serikali ya awamu ya sita inathamini mchango wa jeshi na wakati wote itaendelea kuimarisha utendaji wao.

Pia Waziri TAX ameishukuru serikali ya falme za kiarabu kwa kutoa mafunzo kwa waatalum wa jeshi la anga nchini pamoja na ndege hiyo kwani itasaidia kuimarisha masuala ya kiusalama pamoja na kudumisha mahusiano ya nchi hizo mbili yaliyodumu kwa muda mrefu sasa.

Nae Mnadhimu mkuu wa JWTZ luteni jenerali SALUM HAJI OTHMAN Akimwakilisha mkuu wa majeshi nchini JENERAL JACOB JOHN MKUNDA ameushukuru umoja wa falme za kiarabu kwani ujio wa ndege hiyo pamoja na mafunzo yaliyotolewa kwa wataalamu wa anga wa JWT kwani itaendelea kuwa kichocheo cha kutakabili majukumu ya kijeshi ndani na nje ya nchi na kwa hatua hiyo itasaidia kuendelea kuliweka taifa la Tanzania katika hali amani.

Amesema jeshi la wananchi ni chombo katika vyombo vya serikali ambavyuo vimekua vikinufaika na mahusiano na majeshi ya nchi za nje na kuahidi kuwa kwa wakati wote jeshi litaendelea kufanya kazi zake ndani na nje ya nchi kwa ari uhodari na weledi zaidi na kwamba lipo tayari wakati wowote kutekeleza jukumu lake.

Nae mkuu wa kamandi ya jeshi la anga meja jenerali SHABAN BARAGHASH MANI amesema katika kuimarisha ulinzi na usalama hususani upande wa anga ndege hiyo itasaidia kuendesha oparesehni mbalimbali zikiwemo uokoaji, usafirishaji wa watu na mizigo wakati wa vita na hata wakati amani.

Mwakilishi wa jeshi la falme za kiarabu kanal SAID ABDULLAH amesema ndege hiyo pamoja na mafunzo hayo ya kitaalamu waliyotoa kwa marubani na wataalamu wengine wa ndege hiyo yatasaidia kuongeza ufanisi katika majukumu ya kijeshi.







Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top