Na Mwandishi wetu
Mwanza
Akitoa elimu ya mazingira na mabadiliko ya tabia nchi bi Ester Kusekwa amewataka vijana ambao ni wanufaika wa elimu hiyo kuwa mabarozi wazuri kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa maana uchafuzi wa mazingira unaathari kubwa ndani ya jamii ikiwemo miripuko ya magonjwa ambayo yanaweza yakasababisha vifo na kupoteza nguvu kazi ya Taifa.
Ester Kusekwa ambae ni mratibu miradi kutoka shirika lisilo la serikali la Mwanza Youth And Children amesema ili dunia iendelee kuwa salama ni lazima kila mwananchi ndani ya jamii ahakikishe anatunza mazingira vizuri kwa kufanya usafi katika eneo lake analoishi na kupanda miti ya kutosha.
Miongoni mwa maada zilizo tolewa kwa vijana katika kongamano hilo ni fursa za kiuchimi kwa vijana pamoja na uzalendo
Kwa upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge ndugu Godfrey Mzava amewata viongozi wilayani Magu kuongeza idadi ya makongamo walau yafike manne ili vijana wapate elimu kwa kina