Rais wa Femata atoa siku 6 kufanyika kwa viongozi wapya wa Mkoa wa Geita

GEORGE MARATO TV
0

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo Nchini  (FEMATA), John Bina, ameagiza uongozi wa Mkoa wa Geita kuhakikisha wanatekeleza uchaguzi wa viongozi wapya ndani ya siku sita. Agizo hili limetolewa kutokana na Mkoa wa Geita kuwa wa mwisho katika kuandaa wawakilishi watakaohudhuria Mkutano Mkuu wa FEMATA unaotarajiwa kufanyika Mkoani Tanga.

Bina alitoa agizo hilo wakati wa ziara yake mkoani Geita iliyolenga kusikiliza na kujadili changamoto zinazowakabili wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu. Alisisitiza umuhimu wa viongozi waliopo kutumia muda uliosalia kuitisha mkutano wa wanachama wa Chama cha Wachimbaji Wadogo wa Madini Mkoa wa Geita (GEREMA), ili kufanya uchaguzi wa viongozi wapya.

Kwa upande wao, baadhi ya wanachama wa GEREMA, wakiwemo Misana Nyabange na Godfrey Miti, wameelezea hitaji la kuharakisha mchakato wa uchaguzi ili kuanza maandalizi ya uchaguzi katika ngazi za wilaya na matawi mengine ya wachimbaji wadogo.

Uchaguzi huu unatajwa kuwa muhimu kwa kuhakikisha wachimbaji wadogo wanapata wawakilishi ambao wataweza kutetea maslahi yao katika Mkutano Mkuu wa FEMATA na kusaidia kuendeleza sekta ya uchimbaji mdogo wa madini nchini.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top