Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kampeni "Kiduchu Fresh Tunasonga" na uendelevu wa utoaji mikopo ya elimu


Na: Dk. Reubeni Lumbagala

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ina jukumu la kutoa mikopo kwa waombaji ili waweze kutimiza malengo yao ya kupata elimu katika taasisi mbalimbali za elimu kama vyuo vya kati na vyuo vikuu. 

Pia, HESLB inawajibika kukusanya mikopo kutoa kwa wanufaika wake ili kuwezesha waombaji wengine waweze kupata mikopo ili nao waweze kupata elimu. Kwa zaidi ya miaka 20 sasa, serikali kupitia HESLB, imewezesha vijana wengi wa Kitanzania kutimiza malengo yao ya kielimu kwa kuwakopesha mikopo ya elimu.

Wengi wa vijana hao ni wale wanaotoka familia zenye changamoto za kiuchumi ambazo pengine bila kuwezeshwa mikopo, wasingeweza kumudu kupata elimu kutokana na gharama kubwa za elimu zilivyo huko vyuoni. Hii ndiyo kusema, baadhi yao wasingeweza kutimiza ndoto zao za kusoma fani na taaluma mbalimbali kama wasingepata mkopo wa elimu.

Kwa kuwa tayari fedha nyingi zimewekezwa kwa kukopesha vijana wengi, HESLB inayo kazi kubwa ya kukusanya mikopo hiyo kutoka kwa wanufaika wake hasa waliohitimu masomo na kuwa na kipato katika sekta rasmi au isiyo rasmi.

Kwa wanufaika ambao wameajiriwa serikalini au sekta binafsi kumekuwa na urahisi wa kuwapata kutokana na waajiri kutuma taarifa za wafanyakazi wao kwa HESLB ili waweze kukatwa asilimia 15 ya mshahara kwa mujibu wa sheria.

Lakini kwa wanufaika ambao wamejiajiri wenyewe kama mama na baba lishe, bodaboda, wamachinga, mafundi wa fani mbalimbali, wajasiriamali, kumekuwa na ugumu wa kuwapata, kwani wao wanapaswa kujitokeza wenyewe ili kuanza kurejesha mikopo yao kwa hiari, lakini ukimya wa baadhi yao unasababisha HESLB kukosa marejesho kutoka kwao.

Baadhi ya wahitimu wana mtazamo kuwa ni mpaka waajiriwe na serikali au katika sekta binafsi, ndipo wanapaswa kuanza kurejesha mikopo yao, yaani wanadhani ni mpaka wawe na mshahara ndipo waanze kulipa.

Iko hivi: Muhimu ni kuwa na kipato tu, iwe ni kuajiriwa au kujiajiri, mnufaika mhitimu anapaswa aanze kulipa ili waombaji mikopo wengine wenye sifa nao wakopeshwe kama wao walivyokopeshwa walipokuwa wanafunzi vyuoni enzi hizo.

HESLB ina malengo ya kujijenga katika namna ambayo kutakuwa na uendelevu wa utoaji wa mikopo yaani wakopeshe wanafunzi, lakini wanafunzi hao wanapohitimu na kuwa na kipato, waanze kurejesha mikopo hiyo ili wengine nao wakopeshwe.

Mnamo Aprili 17, 2026, katika ofisi za HESLB, Kanda ya Mashariki, Jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, alizindua kampeni maalum ya kuhamasisha wanufaika hasa waliojiajiri wenyewe kuanza kulipa mikopo yao ya elimu.






Kampeni hiyo ijulikanayo kwa jina la "Kiduchu Fresh Tunasonga," inahamasisha mnufaika mhitimu mwenye kipato kidogo kuwa anaweza kuanza kurejesha mkopo wake ulioiva kwa kuanza na kiasi cha shilingi 5,000 na kuendelea, ili hata yule mwenye kipato kidogo sana aweze kumudu kiwango hicho rafiki.

Katika hotuba yake, Naibu Waziri Wanu amewasihi wanufaika waanze kulipa mikopo yao kidogo kidogo ndiyo maana Bodi imeweka kiwango hicho kidogo ili wengi waweze kumudu.

"Kiduchu ni kidogo ya kidogo … na upekee wake ni kuwafikia wanufaika wengi wenye kipato cha chini ili waweze kurejesha mikopo yao kulingana na uwezo wao, msisubiri hadi muwe na fedha nyingi, anzeni na kiduchu mlichonacho leo. Kila mchango hata uwe mdogo kiasi gani, una mchango mkubwa katika kujenga Taifa letu," alisema Wanu.

Takwimu zinaonesha kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2025/2026, serikali imeshatoa shilingi trilioni 3.6 kwa wanafunzi mbalimbali.

Lengo la kampeni ya “Kiduchu” ni kuwafikia  wanufaika 135,186 wanaodaiwa jumla ya shilingi bilioni 920. Kurejeshwa kwa fedha hizi, kutawezesha uendelevu wa kuwagharimia waombaji wengi zaidi wenye uhitaji, na hatimaye kuwa na raslimaliwatu wenye ujuzi, maarifa na stadi stahili katika kujenga uchumi na maendeleo ya Taifa letu.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Dk. Bill Kiwia amewasisitiza wahitimu wenye kipato kulipa mikopo yao kwani madeni yaliyoiva yamefikia shilingi trilioni 2.78 ambapo trillioni 1.84 zimekusanywa kutoka kwa wanufaika 539,103, huku bilioni 920 kutoka kwa wahitimu 135,186 zikiwa bado hazijakusanywa.

Kwa kuhitimisha makala hii, nitoe wito kwa wanufaika wahitimu wenye kipato kuwa na uzalendo kwa kujitokeza wenyewe ili kuanza kulipa mikopo yao ili kuwezesha  kujenga uendelevu wa utoaji wa mikopo kwa waombaji wenye sifa wanaojiunga na vyuo vya kati na vya elimu ya juu. 

Upo umuhimu kwa wanufaika wa mikopo ya elimu waliokwishahitimu, kufahamu kuwa wanapaswa kuaza kurejesha mikopo hiyo pindi wanapopata kipato hata kama wamejiajiri wenyewe.

Dhamira njema ya serikali ya kusomesha wananchi wake itazidi kutimia endapo wanufaika watalipa kiduchu walichonacho kwa moyo wa upendo na uzalendo ili Taifa letu lizidi kusonga mbele zaidi kimaendeleo. Tafakari.

Maoni : 0620 800 462.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...