Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rc Kheri James Awataka Wahandisi wa Umwagiliaji Kutanguliza Uzalendo na Weledi Kulinda Fedha za Serikali


📍*NIRC Iringa.*

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James, amewataka Wahandisi wa Mikoa na Wasimamizi wa miradi ya Umwagiliaji nchini kufanya kazi kwa uzalendo wa hali ya juu na weledi ili kuhakikisha uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali unaleta tija iliyokusudiwa kwa wananchi.

Mhe. James ameyasema hayo mkoani Iringa wakati akifunga mafunzo ya siku tano ya kuwajengea uwezo watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) yaliyohusu Usimamizi wa Mikataba, Sheria za Ununuzi, Uhandisi wa Geoteknolojia (Utafiti wa Miamba) na ubadilishanaji wa uzoefu.




Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. James amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa miongozo na fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha sekta ya Umwagiliaji , akibainisha kuwa miradi hiyo ni tegemeo kubwa katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kukuza uchumi wa taifa.

“Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza fedha nyingi; ni matarajio yetu kuwa miradi hii itatekelezwa kwa wakati, kwa viwango na ubora unaotakiwa. Mafunzo haya yamekuja wakati mwafaka ili kuwawezesha kusimamia rasilimali hizi zinazotokana na kodi za wananchi,” alisema Mhe. James.


Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa ameipongeza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji chini ya Mkurugenzi Mkuu, Raymond Mndolwa, kwa kuimarisha weledi na kudhibiti migogoro inayokwamisha miradi.

Amesisitiza kuwa bila msimamo wa kusimamia weledi, miradi mikubwa ikiwemo ile ya mabilioni ya fedha kama mradi wa Mkombozi ingebaki kuwa hadithi badala ya kuleta matokeo.

“Sisi ndio 'trigger' ya mabadiliko kupitia kilimo. Kupitia kazi yenu, mnakwenda kutengeneza ajira za vijana na kuitambulisha Tanzania kwenye biashara ya chakula duniani. Msifanye viongozi wawe na kigumizi mbele ya wananchi; wapeni ujasiri kwa kutimiza majukumu yenu kwa wakati,” alisisitiza.


Pia amewataka wahandisi hao kutanguliza uzalendo katika utekelezaji wa miradi ya umwagiliaji, akisisitiza kuwa miradi hiyo ni mali ya Watanzania wote na inapaswa kukamilishwa kwa uaminifu na kujituma.

RC James amesema uzalendo wa wahandisi unaonekana katika kusimamia miradi kwa umakini, kuzingatia muda wa utekelezaji na kuhakikisha thamani ya fedha za umma inalindwa katika kila hatua ya mradi.

"Na Serikali ina maono makubwa ya kuimarisha kilimo cha umwagiliaji, hivyo mafanikio ya maono hayo yanategemea sana dhamira ya wahandisi katika kukamilisha miradi kwa viwango vinavyotakiwa," amesema RC James. 

Mkuu huyo wa mkoa wa Iringa amewakumbusha washiriki kuwa mipango yote ya maendeleo ina muda maalum wa utekelezaji, na uzalendo wa kweli unaonekana pale watumishi wanapohakikisha miradi inakamilika kwa wakati bila visingizio.

Mkuu huyo wa mkoa wa Iringa amewakumbusha washiriki kuwa mipango yote ya maendeleo ina muda maalum wa utekelezaji, na uzalendo wa kweli unaonekana pale watumishi wanapohakikisha miradi inakamilika kwa wakati bila visingizio.

Hata hivyo, Mhe. James ameahidi kuwa uongozi wa Mkoa wa Iringa utaendelea kushirikiana kwa karibu na Tume hiyo kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa mkoani humo inakamilika na kuwanufaisha wananchi kama ilivyopangwa.

Mafunzo hayo yaliwashirikisha Wahandisi wa Umwagiliaji wa mikoa, Menejiment, Wataalamu wa kada mbalimbali na Wasimamizi wa miradi kutoka maeneo mbalimbali nchini, yakiwa na lengo la kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kilimo cha umwagiliaji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Raymond Mndolwa amesema Tume imejipanga kusimamia miradi ya umwagiliaji kwa karibu ili kuhakikisha inakamilika kwa ufanisi na kuleta tija kwa wakulima na taifa kwa ujumla.

Mndolwa amesema NIRC inaendelea kujenga mabwawa ya Umwagiliaji, kuvuna na kuhifadhi maji pamoja na kutekeleza shughuli za uhifadhi wa mazingira, akieleza kuwa hatua hizo ni sehemu ya uzalendo wa kulinda rasilimali za Taifa ili kufikia adhima ya kuongeza uzalishaji wa mazao na kujitosheleza kwa chakula cha ndani na kuilisha Dunia.

"Na katika kulinda mazingira ya miradi, Tume imefanikiwa kupanda miti mingi katika maeneo mbalimbali na ujengaji wa mabwawa, hatua inayolenga kuhifadhi vyanzo vya maji na kuhakikisha miradi inadumu kwa muda mrefu," amesema Mndolwa 

Washiriki wa mafunzo hayo akiwemo Mhandisi Umwagiliaji Mkoa wa Morogoro Juma Matanga amesema washiriki  hao wamepata uelewa mpana kuhusu wajibu wao kama kwa mikoa yote nchini, wakiahidi kutumia maarifa waliyopata kukamilisha miradi ya Umwagiliaji ipasavyo kwa kuzingatia weledi, uwajibikaji na uzalendo.
















Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...