Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kairuki: Sekta ya Mawasiliano yapiga hatua kubwa Ndani ya Siku 100 za Uongozi wa Awamu ya Pili ya Rais Samia



KAIRUKI: SEKTA YA MAWASILIANO YAPIGA HATUA KUBWA NDANI YA SIKU 100 ZA UONGOZI WA AWAMU YA PILI YA RAIS SAMIA.

Na  Mwandishi wetu Dodoma 

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Angela Kairuki, amesema Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeendelea kukua kwa kasi kubwa ndani ya siku 100 za utekelezaji wa kipindi cha pili cha uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKT. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Waziri Kairuki alisema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano, ikiwemo minara ya simu na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano.

“Takwimu zinaonesha kuwa laini za simu zilizosajiliwa zimeongezeka kutoka milioni 99.3 mwezi Oktoba 2025 hadi kufikia milioni 106.9 Januari 2026, sawa na ongezeko la asilimia 7.7,” alisema Waziri Kairuki.

Aliongeza kuwa idadi ya watumiaji wa intaneti imeongezeka kutoka milioni 56.3 hadi milioni 58.1 katika kipindi hicho, ongezeko sawa na asilimia 3.2. Aidha, watumiaji wa huduma za kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu wameongezeka kutoka milioni 71.7 hadi milioni 76.5, sawa na ongezeko la asilimia 6.7.

Gharama za Mawasiliano Zabaki Nafuu

Kwa upande wa gharama za mawasiliano, Waziri Kairuki alisema Serikali imeendelea kudhibiti bei ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa gharama nafuu.

“Gharama za kupiga simu ndani ya nchi zimeendelea kubaki Shilingi 29 kwa dakika, huku wastani wa bei ya data bila kifurushi ukiendelea kuwa Shilingi 9.35 kwa MB moja,” alisema.

Alisema mwenendo huo unaashiria kuongezeka kwa upatikanaji wa huduma za mawasiliano na TEHAMA hususan katika maeneo ya vijijini na yale ambayo awali hayakuwa na huduma, hali inayowawezesha wananchi kupata huduma za kifedha, afya, elimu na biashara kidijitali kwa urahisi na kwa haraka.

Ushirikiano na Sekta Binafsi

Waziri Kairuki alieleza kuwa Wizara imeendelea kushirikiana kwa karibu na Sekta Binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akitolea mfano ujenzi wa minara ya mawasiliano ambapo Sekta Binafsi huchangia asilimia 60 ya gharama huku Serikali ikigharamia asilimia 40.

“Ushirikiano huu umeongeza kasi ya utekelezaji wa miradi na kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za mawasiliano nchini,” alisema.

Mafanikio Mengine Ndani ya Siku 100

Akizungumzia mafanikio mengine, Waziri Kairuki alisema Wizara imefanikiwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Katika Mwaka wa Fedha 2025/26, Wizara ilipangiwa kukusanya zaidi ya Shilingi bilioni 120 kupitia mauzo ya huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, lakini imefanikiwa kukusanya zaidi ya Shilingi bilioni 132, sawa na asilimia 109.9 ya lengo.

Alisema mafanikio hayo yametokana na matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika ukusanyaji wa mapato, hatua iliyoongeza ufanisi, uwazi na kupunguza upotevu wa mapato ya Serikali.

Ujenzi wa Minara Nchini

Katika hatua nyingine, Waziri Kairuki alisema Wizara kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imekamilisha ujenzi wa minara 758 katika kata 713 nchini kwa gharama ya Shilingi bilioni 126, ambapo wananchi takribani milioni 8.5 wanatarajiwa kunufaika.

Aidha, Wizara imekamilisha kuongeza uwezo wa minara 304 kutoka teknolojia ya 2G kwenda 3G na 4G kwa asilimia 100.

Kuhusu ujenzi wa minara vijijini, Waziri alisema ujenzi wa minara 636 (621 ya simu na 15 ya redio) umefikia asilimia 78 ya utekelezaji, ambapo minara 371 tayari imewashwa na kutoa huduma kwa wananchi zaidi ya 67,000.

Alisisitiza kuwa kukamilika kwa miradi hiyo kunachangia upatikanaji wa huduma za kifedha kwa njia ya simu, biashara mtandaoni, elimu, afya pamoja na kupunguza pengo la kidijitali kati ya vijijini na mijini.

Kwa mujibu wa Waziri Kairuki, mafanikio hayo yanaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kujenga uchumi wa kidijitali na kuhakikisha maendeleo jumuishi kwa wananchi wote.



Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...